Kichwa Ndio Mtu
JF-Expert Member
- Jan 17, 2014
- 3,079
- 1,719
Natamani sana kuoa lakini sioi kwa sababu aina ya wanawake naotaka hawapo au wote wameolewa.
Ukiacha sifa za kwanza za mke mfano awe na upendo, mzuri, mvumilivu, mtafutaji, muelewa nk.
Mimi nataka mwanamke mwenye sifa za ziada kidogo maana sifa hizo hapo juu sehemu kubwa ya wanawake wanazo.
Nataka mwanamke mwenye ufaham wa wastani au zaidi wa mambo mengi mfano uchumi, sheria, tekinolojia, sayansi, siasa, dini, falsafa.
Mwanamke anaeweza kujenga hoja, kupambanua mambo mengi vizuri.
Mwanamke anaejua muziki, filamu na mapenzi tu simtaki, hanifai.
Mabinti wengi wa siku hizi wanajua mapenzi, filamu na muziki, mambo mengine hawajui na hawataki kujua, ukileta hoja nje ya hayo anayoyajua atabakia kuitikia tu "ndio mzee" maana hajui.
Wanawake wa ndio mzee mimi siwataki.
Hicho ndio kinasababisha nashindwa kuoa ingawa natamani. Wewe kwa nini huoi, huolewi. (najua kuoa au kuolewa sio lazima)
Ukiacha sifa za kwanza za mke mfano awe na upendo, mzuri, mvumilivu, mtafutaji, muelewa nk.
Mimi nataka mwanamke mwenye sifa za ziada kidogo maana sifa hizo hapo juu sehemu kubwa ya wanawake wanazo.
Nataka mwanamke mwenye ufaham wa wastani au zaidi wa mambo mengi mfano uchumi, sheria, tekinolojia, sayansi, siasa, dini, falsafa.
Mwanamke anaeweza kujenga hoja, kupambanua mambo mengi vizuri.
Mwanamke anaejua muziki, filamu na mapenzi tu simtaki, hanifai.
Mabinti wengi wa siku hizi wanajua mapenzi, filamu na muziki, mambo mengine hawajui na hawataki kujua, ukileta hoja nje ya hayo anayoyajua atabakia kuitikia tu "ndio mzee" maana hajui.
Wanawake wa ndio mzee mimi siwataki.
Hicho ndio kinasababisha nashindwa kuoa ingawa natamani. Wewe kwa nini huoi, huolewi. (najua kuoa au kuolewa sio lazima)