Natamani kumsamehe baba mzazi

Natamani kumsamehe baba mzazi

mdoe

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
433
Reaction score
103
Mimi ni Kijana wa miaka 30. Nimezaliwa katika familia masikini, mkoani Kilimanjaro. Nimeanza kujitambua nikiwa na umri wa miaka mitano nikiwa mikononi mwa bibi wa mama yangu. Sikujua ni kwanini niliishi na bibi wa Mama lakini Baada ya muda, Mama alikuja kunichukua na Nikaenda kuishi nae wilaya nyingine mkoa wa Kilimanjaro ambapo nilianzishwa masomo ya elimu ya chekechea na msingi. Mama yangu ana watoto wane, mimi nikiwa wa pili.

Mtoto wa mwisho ni mtoto wa baba yetu mlezi, ambae nilikuja kubaini kuwa Yule sio baba yangu mzazi, ila ni mlezi kufuatia vijimaneno vya mjomba na Mama yangu mdogo aishie kijijini. ( Wewe mu-uru, . Wewe mkibosho, nk. Wakati Baba tuliekua nae ni Mzigua) Nilikuja kubaini hilo nikiwa kidato cha nne.

Nikaanza kupata Kiu ya kumjua baba yangu mzazi.
Baada ya kumaliza kidato cha sita, hamu ya kumjua baba yangu mzazi ilizidi. Nikamfuata mama yangu mdogo (R.I.P. mama mdogo), ambae alikua akiishi moshi maeneo ya Pasua.

Sikutaka kumbughudhi Mama yangu kwasababu niliona tabu zote alizopitia katika kutulea na kutusomesha. Nilijua wazi Mama mdogo atakua anamjua vizuri dada yake (Mama yangu), na anaweza kuwa na clues muhimu kumpata baba yangu. Alikataa sana, ila mama ni mama.

Nilijua niseme nini na nimshawishi vipi na hatimae alinipa details za baba yangu japo hakujua alikoishi. Kutokana na details nilizopata, ikiwa ni pamoja na sehemu alizofanya kazi, nilifanikiwa kumpata mtu ambae alinipeleka moja kwa moja mpaka nyumbani kwake.

Nilimuona na nikajitambulisha. Niliposema tu nilipotokea alinijua mimi ni nani. Akanitaja jina. By then I was around 16. Nilikaa kidogo na akanipa namba za ndugu zangu kibao niwatafute. Niliwatafuta baadhi na nikajenga nao ukaribu. Nilidhani baba, pamoja na kutokua na uwezo (Amestaafu), angetambua uwepo wangu.

Ila zaidi ya mimi kwenda kumsalimia na kuwa kama mgeni yeyote tu wa kawaida anaekuja na kuondoka, hapakua na la ziada. Hakutaka kujua naishije, niliishije, nini malengo yangu, … no dad to son talk at all. Mategemeo yangu ya kumuona na kuongea na Baba yalipotea kabisa. Nilimtembelea kama mara tatu na baada ya hapo nikakaa kimya kuona kama atanikumbuka japo kwa ku beep.

Baada ya muda, niliamua kumchunguza mama taratibu kujua kulikoni. Nilianza kwa kumuambia kuwa namjua Baba yangu mzee …(Nikamtaja jina). Alishtuka kidogo hatimae akaniambia kua ni kweli, huyo ndie baba yako. Baada ya siku kadhaa, Mama aniliita faragha.

Akaanza kunisimulia mambo ambayo baba alimtendea, iliniuma sana. Ilifika kipindi mama anaomba ridhaa kwa barua kwa baba kuwa tupelekwe jando (Ikumbukwe kuwa walishaachana miaka mingi nyuma), baba anajibu kwa barua kuwa "Hao watoto ni zawadi yako nimekupa. Fanya chochote unachotaka".

Sijui nini chanzo cha ugomvi wao, sijui nini kilipelekea wao kuachana, sijui ni kwa nini tuliishi maisha ya shida sana na mama aliteseka sana peke yake kutulea na wakati baba alikua na uwezo, ila kwa vyovyote vile, baba alitakiwa kuonyesha kuwa altujali wanae.

Ameniona mimi tu, Mdogo wangu alienifata nae ni mwanae, ila wala kumuulizia hamuulizii. Niliwahi kumuuliza kuwa anamtambua mdogo wangu kuwa ni mwanae akajibu kuwa Anamtambua.

Mada ambayo wana Jamiiforums nataka wani shauri ni uamuzi ninaotaka kuuchukua sasa.
Nimemchukia baba yangu ever since nimemuona. Ila inawezekana kuna mengi mengine ambayo siyajui kati yake na mama yangu. Nafikiria kwenda kuongea nae aniambie mambo mengi sana kati yao na kwanini ametususa kiasi hicho.

Japo sidhani kuwa ni uamuzi sahihi kwani niko na baba mlezi ambae kwangu mimi amebeba thamani yote ya neno Baba. Natamani nimsamehe ila sina pa kuanzia. Namuona kama womanizer kwasababu ana watoto sita nje ya ndoa yake, mimi na mdogo wangu tukiwa wamoja wapo.

(Hakuwa amemwoa mama, inavyosemekana alimdanganya, akamzalisha kumbe ameoa). Je, ni uamuzi sahihi kwa mtoto kum face baba yake na kuhoji ukweli wa yaliyojiri kati ya baba na mama?

Kwanini he was irresponsible kwetu tukiwa wadogo? Lengo ni kupata sababu yakumsamehe ili nafsi iwe na Amani kila nikimkumbuka, Badala ya chuki na hasira.

Niwieni radhi kwa uzi mrefu na mchanganyiko wa lugha.
 
Pole sana....maswali mengine mama angekusaidia kwa sababu yy ndo alikua akimjua vizur kuliko wewe.

Me naona hakuna haja ya kumfata ikiwa ulifanya mwanzo sahihi wa weww kumtafuta na hakuonesha hata kushtuka kukuona ni waz hata ukimfata hatakupa ushirikiano madhubuti. Mim nachokuomba msamehe kwa kila baya mwenye jukumu la kusamehe au kuacha analo mungu pekee usimhukumu atahukumiwa na mungu ila umtambue tu kua ni baba n.mzaz wako hata ufanyaje. Na had umefikia hapo hakuwah hata kukuulizia bas wewe cha msingi ushamfahamu baba haina haja ya kumfata tena lolote laweza tokea. Msamehe moyini mwako na muombee msamaha kwa mama ako mama amsamehe kwan tayar wote kila mtu ana maisha yake.
 
Aise usimtafute ukamuuliza, mimi nina experience na mambo haya, wewe soma upate kazi au ujiajiri upate pesa yeye ndo atakuja mwenyewe.
 
Pole sana.
Nina jamaa yangu yupo Dar anakaa T/Mikoroshini na Baba yake yupo Mwenge hamjari kwa lolote na Kisa ni kama chako.

Tulimshauri tu kwa kuwa ni Mtu mzima na Baba yake hamtaki afanye yake zaidi ashirikiane na ndg wenye mapenzi mema.
 
Msamehe...bhna
 

Attachments

  • 1413610957546.jpg
    1413610957546.jpg
    13.1 KB · Views: 2,061
Msamehe sio kwa sababu anastahili, au kwa sababu ameomba msamaha; bali msamehe kwa ajili ya afya ya moyo wako, msamehe kwasababu ni kitu sahihi kufanya, msamehe kwa sababu nawe wahitaji kesamehewa makosa yako na Mungu wako, msamehe ili kumfundisha na kufundisha wengine, msamehe kwasababu wewe ni zaidi ya chuki, hasira na visasi, msamehe kwa sababu UNAWEZA.
 
Aise usimtafute ukamuuliza, mimi nina experience na mambo haya, wewe soma upate kazi au ujiajiri upate pesa yeye ndo atakuja mwenyewe.

Tayari mimi nina maisha yangu. sihitaji chochote kutoka kwake zaidi ya attention ya baba kwa mtoto
 
Pole sana.
Nina jamaa yangu yupo Dar anakaa T/Mikoroshini na Baba yake yupo Mwenge hamjari kwa lolote na Kisa ni kama chako.

Tulimshauri tu kwa kuwa ni Mtu mzima na Baba yake hamtaki afanye yake zaidi ashirikiane na ndg wenye mapenzi mema.

Ninapokaa mimi na anapokaa yeye ni umbali wa kilometa 9. nauli ni sh 400. ila kila nikifikiria kwenda kumsalimia napata hasira naahirisha
 
Kitu ambacho wazazi wanaotelekeza, watoto wao esp wa kiume ni kwamba, hata akue azeeke hata kaa awe na mapenzi tena na huyo mzazi, bora ma binti wameumbiwa moyo mwepesi wa kusamehe na kusahau, vijana wa kiume husamehe but hawasahau.
 
Daah mkuu mimi nakushauri achana na habari za kumaind sijui mshua anatakiwa kuwatambua wadogo zako sijui na wewe mwenyewe..cha msingi fanya mambo yako na wadogo zako onesha uwezo wewe mtoto wa kiume kwamba hata kama hana time na nyie, mmeweza kusimama kimaisha na kufanikiwa kwa watoto akifika umri flani mambo ya dad to son talk or whatever hua yana katila nashangaa wewe bado unayo aisee...belive that i know what am saying and saying what i know...Over..!!
 
me nakishauri achana nae. kabisa endelea na maisha yako usimkazimishe jambo lolote .mwache malipo ni duniani
 
Ninapokaa mimi na anapokaa yeye ni umbali wa kilometa 9. nauli ni sh 400. ila kila nikifikiria kwenda kumsalimia napata hasira naahirisha

mkuu achilia samehe tu.
 
pole sana ila kuwa muangalifu,usikute mama yako alishakujaza maneno fulani,ambayo pangine na baba yako anafahamu.
Ushauri.
Msamehe halafu endelea na maisha yako.
Wewe nimtu mzima sasa.
Don't live with the past.
 
Grudges make us walk with burdens in our hearts like a noose around the neck.Ask God to give you thestrength to forgive.
 
mimi nahisi ningemtafuta kumfanyia kitu roho yangu iridhike.........revenge its good for health
 
Back
Top Bottom