Natamani hata kuondoa uhai wangu

Natamani hata kuondoa uhai wangu

Wadau habari zenu,

Wadau mimi nikijana (28) nilikuwa nafanya kazi kampuni fulani ila ikafika muda tukapunguzwa kazini, lakini pia nilikuwa nimesave kiasi cha kama laki 7 kwenye account yangu benki, ikumbukwe pia kipindi chote hicho sikuwa na hata pakuishi hata simu niliyokuwa natumia ilikuwa ya batani maana nilikuwa na katecno.

Ila katika harakati za kutafuta kazi basi ilibidi nikauze ili kupata nauli ya kufatilia michongo ya kazi, maana nilikuwa jobless tu kitaa na pia wazazi nao hawakuwa vizuri kiuchumi hivyo nilikuwa napiga tu mishe kwa kujitegemea.

Sasa baada yakupunguzwa kazini kutokana na ukata wa kampuni huku nikiwa na mawazo mengi kichwani nikafatilia pesa yangu benki huku nikijua ndio mwisho wa kazi. Nikasema wacha ninunue hata ka smartphone ka laki 2, ikabaki laki 5 ili zingine zinisaidie kwenye michongo yangu, hapa ndipo balaa lilipoanzia

Nikajikuta nimekuwa mlevi kupindukia ndani ya siku 5 kwenye account nikicheki salio ni elfu 10 tu ndio imebaki. Sijui pakuanzia tena na pesa imeisha, yaani nimetumia almost laki 5 kwa siku 5 duh! Hapa nilipo nimechanganyikiwa, kazi sina pesa zimeisha mpaka natamani kujimaliza tu maana mawazo tele kichwani.

Ndugu zangu, huku JF sijaingia muda nikasema mkinikosa jua nimeshafanya maamuzi magumu tu ya kujitoa uhai

NB: Sina uandishi mzuri na nimepaniki mno hapa nilipo maana mawazo hayaishi.
Acha ujinga wewe hela umelewea halafu unataka ujiue,nikahisi sijui ulipatwa na janga gani,Nilitaka nikukonekt na dogo yuko chuga Kuna mchongo kumbe hali si hali lol
 
Cheki chuma ichooooo
20230313_102141.jpg
 
Wadau habari zenu,

Wadau mimi nikijana (28) nilikuwa nafanya kazi kampuni fulani ila ikafika muda tukapunguzwa kazini, lakini pia nilikuwa nimesave kiasi cha kama laki 7 kwenye account yangu benki, ikumbukwe pia kipindi chote hicho sikuwa na hata pakuishi hata simu niliyokuwa natumia ilikuwa ya batani maana nilikuwa na katecno.

Ila katika harakati za kutafuta kazi basi ilibidi nikauze ili kupata nauli ya kufatilia michongo ya kazi, maana nilikuwa jobless tu kitaa na pia wazazi nao hawakuwa vizuri kiuchumi hivyo nilikuwa napiga tu mishe kwa kujitegemea.

Sasa baada yakupunguzwa kazini kutokana na ukata wa kampuni huku nikiwa na mawazo mengi kichwani nikafatilia pesa yangu benki huku nikijua ndio mwisho wa kazi. Nikasema wacha ninunue hata ka smartphone ka laki 2, ikabaki laki 5 ili zingine zinisaidie kwenye michongo yangu, hapa ndipo balaa lilipoanzia

Nikajikuta nimekuwa mlevi kupindukia ndani ya siku 5 kwenye account nikicheki salio ni elfu 10 tu ndio imebaki. Sijui pakuanzia tena na pesa imeisha, yaani nimetumia almost laki 5 kwa siku 5 duh! Hapa nilipo nimechanganyikiwa, kazi sina pesa zimeisha mpaka natamani kujimaliza tu maana mawazo tele kichwani.

Ndugu zangu, huku JF sijaingia muda nikasema mkinikosa jua nimeshafanya maamuzi magumu tu ya kujitoa uhai

NB: Sina uandishi mzuri na nimepaniki mno hapa nilipo maana mawazo hayaishi.
Wenzako wanakuja kuomba ushauri wakiwa na mitaji, wewe unaomba wakati umekula mtaji? Utakula ulikopeleka mboga
 
Usichague kazi
Pita mitaani kuna wanaotaka kufuliwa, kulimiwa majani, kubebewa mizigo, kupiga boda boda na zingine nyingi. Hutajuta
 
Shetani amepita
Hiyo ndo inaitwa ng'ombe wa maskini hazai na akizaa huzaa kilema.
Ila pambana utapata zaidi ya hizo
Be positive
 
Pole sana. Unataka kujiua kwa sababu hauna pesa au umekuwa mlevi? Ndugu zako wapo wapi hata wazazi? Kwenu kwanini hauendi ili uniweke sawa tena kimawazo na kuanza upya?
 
Qualification zangu mkuu mimi nilisoma diploma chuo fulani(Public administration and management)na sikupata ajira kwa zaidi ya miaka 5 sasa ndio nikaamua kujichanganya kwenye kampuni ndio ikawa hivyo
daah hatari sana ila na wew ULIANZAJE KUNYWA POMBE ZA LAKI 5??? yani unajua ushafukuzwa kazi alafu unachezea hela
 
Back
Top Bottom