Nataka kwenda kuchora Tatoo

Nataka kwenda kuchora Tatoo

LadyAJ

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2015
Posts
7,173
Reaction score
9,656
Najua ni haramu lakini nahisi nataka hicho kitu,nataka kuweka alama ya ukumbusho wa jina la mtu muhimu sana kwangu!! Hivyo nimevutiwa kwenda kuchora sehemu ya mwili wangu (mkononi) kama ishara yeye kuishi daima mwilini mwangu.
Wazoefu naomba mnipe location ya fundi mzuri wa Tatoo na approximation ya gharama zake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kila la kheri ila fikiria mara 2, anaweza kuja wa muhimu zaidi ya huyo na akakwazwa na iyo tatoo kwa kuona juhudi zake na kila kitu kwako si kitu ivo kukata tamaa ingali ww ukimuhitaji bado .
 
Hapa begani nimechora tatoo yenye maneno John 3:16 ambayo tafsiri yake haraka haraka ni Kwa maana Mungu aliupenda ulimwengu kiasi cha kumtoa Mwanae pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.. Alinichora jamaa mmoja anaitwa Pollo, nilimuita akanifata ninapoishi, saivi kawa staa kidogo sijui hata huduma yake ipoje, lkn ana ofisi Bamaga
 
Kuna jamaa nilimuona anatoa ushuhuda kanisani kwa nabii Magaya wa Zimbabwe kupitia Yadah tv anaeleze jinsi gani tatoo zilivyo demonic na ni dhambi na aliquote mstari kutoka mambo ya walawi

Yani jamaa alijichora kila sehemu ya mwili wake...na ye mwenyewe alikuwa mchora tatoo

So think twice

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna uzi wako hapa kuhusu Baba wa mtoto wako wa kwanza kama sikosei anaitwa Abedi ambaye sasa ni marehemu. Kama ni jina lake basi mie ushauri wangu usiweke maana hujui mumeo litamgusa vipi au umwambie nia yako huyu wa sasa ili uone reaction yake, lakini kama ni la mumeo huyu wa sasa ambaye alikuhudumia kwa hali na mali baada ya Abedi kufariki na wewe ukiwa mjamzito basi hakuna neno RUKHSA.

Najua ni haramu lakini nahisi nataka hicho kitu,nataka kuweka alama ya ukumbusho wa jina la mtu muhimu sana kwangu!! Hivyo nimevutiwa kwenda kuchora sehemu ya mwili wangu (mkononi) kama ishara yeye kuishi daima mwilini mwangu.
Wazoefu naomba mnipe location ya fundi mzuri wa Tatoo na approximation ya gharama zake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uko wapi? Mimi nachora na pasi ya umeme ni pm tafadhali nikuchore.

Usinisahau kwenye Baraza Jipya.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom