Nataka kwenda Kenya Kutembea

Nataka kwenda Kenya Kutembea

Ukiwa mombasa nenda Cassabalanca hoteli ukajifariji au magongo night.Au vepe?
 
Wasi wasi wangu ni hapo unapoanzia kufika kenya yaahani mombasa then malindi alafu wewe mgeni na sijui kama huyo anayekupokea ni ndugu yako au mshikaji,kama ni stranger uende kwa tahadhari kwa sababu safari yako yaweza kuwa hatarishi.
 
[QUOTE="Gojaga Nize, post: 15476867, member: 2

niko siku ya tatu sasa
 
Unatafuta mawaidha kutoka kwa watz kuhusu safari ya Kenya?Watakuzingua bureee!Mada yako ungeiweka Kenya forums wakenya wangekukaribisha vizuri tu!Usiskize hizo hadithi za vijiweni.Kenya utafika na kutoka ukiwa mzima,Mombasa raha utataka kurudi tena.Kama ulivoambiwa paspoti,kadi ya yellow fever tu,hapo sawa.Ukifika usiwe na wasiwasi bora usiombe vitu unapoagiza,iwe mkahawani au dukani.Fanya kama mkenya,sema nipe soda moja,haraka!Au ukipenda uwe nyang'au kabisa sema wewe mathe(dada) au we buda(kaka)!Leta Soda na kaimati haraka,chap chap!Haha!Usiogope kujitambulisha kama mtz,wakenya wanapenda watz achana na utani wa hapa jf.Utapata rafiki wapya kwa wingi tu,bora usiwe mtu wa kunyamaza sana.Cheka,furahia ongea na watu,hata usiowajua.Karibu Kenya!
Ni kweli,nilikaa Nairobi kama wiki mbili hivi nilikua nakaa KENYA COMFORT HOTEL iko karibu na Nakumat supermarket,Wakenya wanawapenda sana watanzania,wanapenda kiswahili cha huku na wanapenda sana miziki ya Tanzania
 
Weee Malindi? Huko si kule wanakotafuta watu wa kwenda Al shabaab?
Inabidi ufuatiliwe kwa karibu.
 
Wasi wasi wangu ni hapo unapoanzia kufika kenya yaahani mombasa then malindi alafu wewe mgeni na sijui kama huyo anayekupokea ni ndugu yako au mshikaji,kama ni stranger uende kwa tahadhari kwa sababu safari yako yaweza kuwa hatarishi.

kwa uwezo wa Mungu nilifika Salama Mombasa saa moja kasoro,nikapanda tuktuk (bajaji) mpaka bakstan nikapanda Matatu nikasubiri mpaka ikajaa tukatoka saa mbili kamili mpaka Malindi

Kuna jamaa anafanyakazi Mombasa alikua anaenda MALINDI kwa short holiday alipenda kuzungumza na mimi sana nikua nimechoka mno,nilimsoma nikamuelewa nikamuomba amtext jamaa yangu kuwa niko njiani kwenda MALINDI ilikua kama saa tatu hivi ,jamaa yangu fast akapiga simu nikaongea nae na nikamueleza eneo ambalo tulikua tunapita,bahati mzuri jamaa jirani yangu baada ya kuteremka pale stage alinifikisha alipo mwenyeji wangt kama saa ne na dk20 usiku.Nashukuru niko Salama hadi sasa Nafurahia mandhari ya MALINDI nimetembea sehemu kadhaa ikiwemo NAKUMAT
 
Ni kweli,nilikaa Nairobi kama wiki mbili hivi nilikua nakaa KENYA COMFORT HOTEL iko karibu na Nakumat supermarket,Wakenya wanawapenda sana watanzania,wanapenda kiswahili cha huku na wanapenda sana miziki ya Tanzania
Umefanya vizuri sana kusema hivo,kwa sababu ya utani mwingi hapa jf,watz wengi wanaona ni kama hali ndo ilivo huku kwetu Kenya.Nikisema wakenya wanapenda watz wataniona muongo tu bila uthibitisho wa watz kama wewe walotembea Kenya.Karibuni Kenya,kutembea kwingi ndo kuona mengi.
 
Umefanya vizuri sana kusema hivo,kwa sababu ya utani mwingi hapa jf,watz wengi wanaona ni kama hali ndo ilivo huku kwetu Kenya.Nikisema wakenya wanapenda watz wataniona muongo tu bila uthibitisho wa watz kama wewe walotembea Kenya.Karibuni Kenya,kutembea kwingi ndo kuona mengi.

mkuu nimependa sana muongozo wako dhana niliyokua nayo kichwani sio uhalisia ulioko huku,nimepapenda kwa kweli kiasi kwamba mungu akijalia nikirudi salama kwetu naweza kuja tena na tena kama Sababu itakuwepo ya kufanya hivyo
 
mkuu nimependa sana muongozo wako dhana niliyokua nayo kichwani sio uhalisia ulioko huku,nimepapenda kwa kweli kiasi kwamba mungu akijalia nikirudi salama kwetu naweza kuja tena na tena kama Sababu itakuwepo ya kufanya hivyo
Mkuu umefata mke huko nini teh teh teh teh
 
Umefanya vizuri sana kusema hivo,kwa sababu ya utani mwingi hapa jf,watz wengi wanaona ni kama hali ndo ilivo huku kwetu Kenya.Nikisema wakenya wanapenda watz wataniona muongo tu bila uthibitisho wa watz kama wewe walotembea Kenya.Karibuni Kenya,kutembea kwingi ndo kuona mengi.
Kweli,niliishi maisha mazuri sana aise,ukiongea watu wanatamani uongee zaidi ili wafurahie.Nilikua na meet na washkaji pale Java house ABC place,tunapiga stori sana.Ila nilishangaa kitu kimoja.Mitaa ya Nairobi hawajui Shikamoo...hapo ndo nilikua nachoka,ukimsalimia mzee anakuangalia tu
 
Kweli,niliishi maisha mazuri sana aise,ukiongea watu wanatamani uongee zaidi ili wafurahie.Nilikua na meet na washkaji pale Java house ABC place,tunapiga stori sana.Ila nilishangaa kitu kimoja.Mitaa ya Nairobi hawajui Shikamoo...hapo ndo nilikua nachoka,ukimsalimia mzee anakuangalia tu
Kweli Nairobi nikwingine aisee.Hawajui shikamoo lakini haimaanishi wana ubaya wowote ule.Ata sisi wakenya ambao si wazaliwa wa nairobi pia tuliwashangaa hapo awali tulipodunda na heshima zetu na salamu zetu za mikoani lakini sasa tulishawazoea.Nairobi kila mtu na shughli zake!Nairobi ukianza mambo ya shikamoo mzee,utajibiwa mzee ni wewe!Hakuna mzee nairobi,wenyewe wanasema hivo.Mtaa wa wajanja!
 
mkuu nimependa sana muongozo wako dhana niliyokua nayo kichwani sio uhalisia ulioko huku,nimepapenda kwa kweli kiasi kwamba mungu akijalia nikirudi salama kwetu naweza kuja tena na tena kama Sababu itakuwepo ya kufanya hivyo
Safi sana jombaa,nilikwambia Malindi na Kenya kwa jumla utapapenda tu.Shida ni stori za uongo wanazoendeleza wanafik zinapokuingia akilini unajipata ukisafiri unafika kwa wenyewe ukiwa na dhana flani.Cha muhimu ni kuwa na fikra huru na ukifika kwa wenyewe uishi wanavoishi na uheshimu tamaduni zao pia.Navowajua wakenya ulipowaambia wewe ni mtz hawakutaka uondoke karibu nao,wakenya wanapenda watz si siri,mimi mwenyewe nilipoingia jf mara ya kwanza nilishangaa sana chuki mitandaoni imetoka wapi?Haya waalike wenzako wa huko malindi watembee tz pia.Ukirudi tz,safari njema aisee na karibu tena Kenya!
 
Back
Top Bottom