Nataka kuwa Baharia

Nataka kuwa Baharia

Mkuu sidhani kama hilo jina lipo sahihi lakin ni koz inayotolewa kwa wiki sita inayohusiana na uangalizi upande wa engine(engine room).Kwenye hiyo kozi unakutana na basic mathematics,physics,workshop technology na masomo yanayohusiana na engine.Hiyo kozi unafanya mitihani aina mbili,wa kwanza wakuandika kwenye karatasi(ambayo tumezoe) wa pili maswali ya papo hapo au ana kwa ana(oral).Ili ufanikiwe kwenye huu mtihani(oral)lazima uwe na seatime angalau ya mwezi mmoja na kuendelea maana maswali yake yanahusiana na kaz unazofanya kwenye meli hasa kwenye chumba cha engine(Engine room).
Kweli Mkuu nimekosea jina la kozi, kozi inaitwa 'FORMING PART OF NAVIGATIONAL/ENGINEERING WATCH'
 
Wasiliana na Captain Philips anayo majibu yakukufaa
 
Sina ufahamu mkubwa sana kuhusiana na suala la ubaharia ila nimekua nikiifuatilia hii kazi muda mrefu kidogo na kwa ukaribu sana. Mara nyingi huwa napata information kupitia internet, kuwasiliana na watu ambao wanasomea ubaharia na pia nilishawai hata kwenda takriban mara tatu pale Dar es salaam Maritime Institute DMI mara ya kwanza ilikua mwaka 2009 kipindi hicho nipo form three kuulizia namna ya kujiunga na chuo chao. Kwa sasa ninakua nawasiliana na Rais wa serikali ya wanafunzi wa DMI huyu alikua ni classmate wangu kipindi tunasoma diploma ya electrical engineering MUST kwa sasa yeye yupo DMI anasoma degree ya Marine Engineering na mimi nimebaki MUST nasoma degree ya electrical engineering. Kwa suala mandatory course imeshaelezewa kwa ufasaha hapo awali. Tukiachana na hayo kama haujasomea long course yeyote ya marine ili maisha yawe mazuri katika meli na mshahara uwe wa kueleweka inatakiwa angalau uwe una fani nyingine mfano mechanical engineering,electrical engineering, electronics engineering, Telecommunication engineering, upishi,welding, mambo ya afya etc. Kwa sasa hivi DMI kuna course mpya inaitwa Electro Technical Officer ETO na nimejaribu kuangalia entry eligibility nimeshindwa kuipata kwani website yao kwa sasa inamiss baadhi ya taarifa. Ila cha ajabu hawa jamaa DMI ukiwatumia email hawajibu hata kidogo lakini ukiwafuata face to face ni watu wakarimu na kuliko hata vyuo vyote tz watakupa information yoyote unayoitaka. Kwa upande wa diploma na degree za dmi entry eligibility ni sawa na vyuo vyote tanzania. Kangu binafsi nimebase sana na ufuatiliaji upande wa ufundi mtu aliyesoma kunzia cert,dip na degree ya mechanical yeye huwa hana tofauti kubwa na mtu aliyesoma marine engineering with respect levels. Kwa upande wa mtu wa electrical anaweza pia kufanya kwenye upande wa engineering department kama specialist wa umeme ila unatakiwa usomee course ya electro technical officer ili uwe verified ship electrical engineer.
 
inategemea na level ya elimu uliyo nayo na kazi ambayo wewe utakua tayari kuifanya maan kuna kazi za fani mbali mbali katika meli za kisasa yani (mordern day ships) lakini kwa swala la kufanya kazi kwenye meli za njee ni swala nyeti kidogo maana kampuni nyingi za meli sasa hivi wana hitaji watu wenye experience au labda upate mtu wa kukushika mkono
 
Back
Top Bottom