Nataka kumrusha mtoto darasa

Nataka kumrusha mtoto darasa

sasa unamkimbiza wapi na wakati ajira zenyewe hakuna?
 
Apana mrushe hadi la saba afanye mtihani wa la saba ili maana pia unafaida... fikiria iktokea uhakiki uko mbele na cheti chake cha la saba kkatakiwa si atakulaumu?
 
Inategemea kichwa cha mtoto, Mimi kijana wangu Alisoma mpk la 5 nikamrusha kidato cha 1 sasa hivi yupo kidato cha 2 na anafanya vizuri tu, mwache asome la 5 kisha mrushe kama yupo vizuri
 
Apana mrushe hadi la saba afanye mtihani wa la saba ili maana pia unafaida... fikiria iktokea uhakiki uko mbele na cheti chake cha la saba kkatakiwa si atakulaumu?

Waziri mwenye dhamana ameshasema cheti cha la 7 hakina maana, sababu ni watoto wengi kwa sasa hawafanyi huo mtihani kwa ajili ya kurushwa kidato, na pia kuna miaka hapo katikati vyeti vilikuwa havitoki. So hiyo haina tatizo
 
Katika mlolongo wangu wa maisha sijawahi kuulizwa cheti cha darasa la saba ila unachoweza kufanya ni kuchukua barua kutoka shule aliyosoma ikianisha kwamba alisoma hapo na namba yake ya usajili.
Asante sana bro nitafanya hivyo
 
Waziri mwenye dhamana ameshasema cheti cha la 7 hakina maana, sababu ni watoto wengi kwa sasa hawafanyi huo mtihani kwa ajili ya kurushwa kidato, na pia kuna miaka hapo katikati vyeti vilikuwa havitoki. So hiyo haina tatizo
Mkuu asante sana kwa taarifa
 
At least hyo anaweza akasom la tano kidogo aalf ukamrusha la sits mwaak huo huo, hapo afadhal maanakwa ufahamu wangu mimi ni kwamba la saba ndio hujenga msingi wa form 1, nakushaur lazima asome la 7
Mkuu la saba sio issue sana, mwanangu hakusoma kabisa darasa la saba, alipomaliza la sita nikamtafutia shule ya sekondari na alifanya vizuri tu huko mbele ya safari...
 
Mimi ni tofauti kidogo na mwanao ,mimi nilipofika la Sita shule iliniombea kibali cha kufanya mtihani wa la Saba maana nilikuwa nipo vizuri sana kwenye masomo na nilikuwa shule ya msingi za kayumba sio kama ya mwanao,lakini nilifanya mtihani wa la Saba nikafaulu nikaenda form one nikakaza msuri tena nilipofika form three nikaomba mtihani wa form four pia nao nikafaulu baada ya hapo nikaendelea kama kawaida mpaka chuo lakini dalasa la saba na form four sijasoma, ili mambo haya yote yanawezekana ikiwa ataombewa kibali kutokana na uwezo wake.
Sa hiz uko wap
 
Hilo la kumrusha si kushauri Hata Kama anafanya vizuri.
Ni vema ukamwacha akamaliza la Saba maana darasa la sita limebeba mambo mengi saana ni Bora akayasoma ili asisumbuke mbeleni.
Hiyo ya kurusha ni changamoto Ambayo tunaipata ambao tuna shule za English medium. Nashauri umwache amalize
 
Ushauri wangu Kumrusha hadi Kidato cha kwanza sio vyema,Wakati mwingine huwa tunahadaika na hizi shule za Mfumo wa Lugha ya Kiingereza.Mtoto anaonekana anauelewa mkubwa sana bila kujua kuna baadhi ya Walim "Hupika"Matokeo ya watoto wetu na kuturubuni kuwa watoto wetu wanauelewa mkubwa lakini kumbe hakuna kitu.Au wakati mwingine mtoto akaonekana kweli anauelewa mkubwa akiwa na umri mdogo na kushawishika kumrusha darasa, pindi anapofika darasa tarajiwa mambo yanageuka na kumpoteza mtoto kabisa kwani anashindwa kuendana na masomo husika darasani na ukabaki kujuta imeshamtokea Shangazi yangu miaka ya huko nyuma.
Uko sahihi, walimu huwa wanawaharibu watoto sana na kutudanganya wazazi. Nilikuwa na mtoto shule A akawa anafaulu vizuri yeye ni kati ya wa kwanza hadi wa tatu na wastani wa A nikamhamishia shule B ufaulu ukashuka na kuwa na wastani wa C. Hata ukimfuatilia anaonesha kuwa na uwezo wa wastani hivyo tusijaji uwezo wa watoto kwa ufaulu wa mitihani
 
Nimeona vijana waliotoka darasa la tano english medium na kwenda kuanza kidato cha kwanza,na walifanya vizuri sana
 
Asante sana kwa ushauri. Kuhusu akili nje ya darasa, siwezi kulizungumzia sana hilo lakini ninavyo muona, anajitambua.. Hofu yangu ipo kwenye ishu ya cheti cha darasa la saba. Kwamba, anaweza kusumbuliwa huko mbeleni. Inaweza kufika mahali, kikahitajika cheti chake cha darasa la saba. Hilo unalizungumziaje mkuu?
Hakuna kitu kama hicho,hata kwenye ukaguzi wa vyeti cha darasa la saba wamekiondoa kwa sababu ya vijana walio rushwa
 
Jamaa usimrushe darasa lolote. Mwache mwanao a.excel his best ktk kila level ya elimu yake.
 
Habari wakuu,

Naombeni ushauri wenu.

Binti yangu ana miaka miaka Tisa yupo darasa la nne kwenye shule ya english media. Nafanya vizuri sana darasani, nataka mwakani baada ya matokeo ya darasa la nne nimpeleke kidato cha kwanza.

Wajuzi wa mambo mnaonaje hilo wazo langu?

Nini faida zake na hasara zake?

Kuna MTU amewahi kufanya hivyo?

With much thanx in advance

Academically, kumrusha darasa, your child may be able to cope; however, Socially, the child may not be able to fit in with the rest of classmates because of the age gap. Kwahivyo basi, nakushauri na hili ulifuatilie kwa makini. Social activities ni muhumu saana kwa watoto; otherwise, mtoto ana weza ku-lose interest ya kwenda shule/kusoma.
 
Uko sahihi, walimu huwa wanawaharibu watoto sana na kutudanganya wazazi. Nilikuwa na mtoto shule A akawa anafaulu vizuri yeye ni kati ya wa kwanza hadi wa tatu na wastani wa A nikamhamishia shule B ufaulu ukashuka na kuwa na wastani wa C. Hata ukimfuatilia anaonesha kuwa na uwezo wa wastani hivyo tusijaji uwezo wa watoto kwa ufaulu wa mitihani
Kwenye baadhi ya shule za english medium kuna mchezo mbaya hufanywa ambapo mzazi usipokuwa makini unapotezwa. Wanafanya hivi: Wao hucheza na akili ya mzazi, wanajua bila shaka kila mzazi angependa kuona mwanae anafanya vizuri ili aone fedha nyingi anazolipa kwa ajili ya elimu ya mwanae zinafanya kazi. Kama mwanao hana uwezo kuna wakati humpandishia ufaulu kwa lengo hilo ovu.

Mtoto wangu alikuwa katika shule moja ya english medium iko katika manispaa ya Temeke, alikuwa anaongoza darasani, kipindi hicho shule ile ilikuwa ikivuma sana hivyo wazazi wengi walikuwa wakipeleka watoto wao pale. Kuna term moja mtoto wangu akaja kunilalamikia kuwa mtihani wake wa somo moja hauonekani! Kwanza nilijua labda tu utakuwa umepotea kwa bahati mbaya, lakini mwananngu kitendo hicho kilimkosesha amani kabisa, hivyo nikaamua mimi mwenyewe kwenda kule shuleni.

Nilipokutana na mwalimu wake wa somo lile, akaniambia yeye alisahihisha lakini akawa anasita kuniambia kama aliusahihisha alipata alipata alama ngapi. Nikamfuata mmliki, ambaye baadaye nilikuja kutonywa kuwa ndiye hucheza huo mchezo akiwashirikisha walimu, alikuwa amenizoea sana kwa kuwa nilikuwa ninaenda shuleni pale mara kwa mara. Baada tu ya kumweleza kilichonipeleka pale akanijibu haraka haraka tu kuwa jambo hilo atalishughulikia. Lakini mtihani wa kijana wangu haukuonekana, wala alama alizopata hazikujulikana....lakini baadaye ikaja kubainika kuwa aliwekewa alama za chini kiasi kwamba hata mwalimu wake alishangaa.

Baada ya kufanya uchunguzi wa kina nikaja nikabaini kuwa mkurugenzi wa shule alikuwa anafanya udanganyifu kwa kubadilisha alama za watoto kwa kushusha wengine na kupandisha wengine kwa lengo la kuwahadaa wazazi wenye watoto ambao uwezo wao uko chini, kwamba shule ina uwezo mkubwa wa kupandisha kiwango cha uelewa wa watoto. Nilipobaini huo mchezo mchafu nilimwondoa mwanangu na kumhamishia shule nyingine inayomilikiwa na kanisa.
 
Ushauri wangu Kumrusha hadi Kidato cha kwanza sio vyema,Wakati mwingine huwa tunahadaika na hizi shule za Mfumo wa Lugha ya Kiingereza.Mtoto anaonekana anauelewa mkubwa sana bila kujua kuna baadhi ya Walim "Hupika"Matokeo ya watoto wetu na kuturubuni kuwa watoto wetu wanauelewa mkubwa lakini kumbe hakuna kitu.Au wakati mwingine mtoto akaonekana kweli anauelewa mkubwa akiwa na umri mdogo na kushawishika kumrusha darasa, pindi anapofika darasa tarajiwa mambo yanageuka na kumpoteza mtoto kabisa kwani anashindwa kuendana na masomo husika darasani na ukabaki kujuta imeshamtokea Shangazi yangu miaka ya huko nyuma.

Isije ikawa mzazi anaangalia Mtoto ameshika NAFASI gani darasani.

Hizi Shule za English Media (um); nyingi zina udanganyifu Mkubwa. Kutokana na kwamba ziko kibiashara hufanya Matokeo yaonekane mazuri ili wapate wateja

Ikumbukwe kwamba Mtoto anaweza akawa wa kwanza kwa kufanyishwa mitihani mirahisi; kuwa kwenye kundi la watoto ambao uwezo wao ni Mdogo na hivyo kuonekana Kipanga ... Mtoto huyo huyo akihamishiwa Shule nyingine anaweza akaishia kushika mkia ....

Swala lingine ni umri, miaka 9, asome tena mwaka mmoja na kuanza form 1 akiwa na miaka 11? Je atakuwa na rika lake huko? Kuna mambo mengi ambayo hataendana na wenzake kwa hiyo Hata mazingira yanaweza kuchangia kumfanya arudi nyuma kitaaluma. Utakuwa umemnyima fursa ya kufanya mambo muhimu katika maisha yake Kama vile michezo ambayo huko sekondari haitakuwepo kulingana na umri wake ... Kimsingi atakomazwa na Atakuja kufanya mambo ya KITOTO kwenye umri Mkubwa .... Hahahaha ... Lakini wapo Wazee wa aina hiyo Leo.

Kwa hiyo tafakari kwa kina kabla ya kufanya uamuzi!!!
 
Hii nchi mambo yanabadilika sana this time kuna mtihan wa drs la nne wenyewe wanasema mtoto huko mbele ili afanye mtihan wa drs la saba inabidi awe amefanya kabla mtihan wa drs la nne so it seems kutakuwa na mfumo wa utunzaji wa taarifa za mwanafunzi so kama wako utamrusha naamin huko mbele itamletea shida. Ni ushauri tu
 
Back
Top Bottom