Nataka kumrusha mtoto darasa

Nataka kumrusha mtoto darasa

Shuleni waalimu wake wanashauri vipi? Nafikiri wao wana mchango mkubwa hasa katika kutaarisha maombi maalum ya matakwa yako kama kweli mtoto ana uwezo au la. Na pia kama itawezekana kifanya hivyo, basi mtoto apatiwe mtaala maalum kwa ajili yake ambao utamwezesha kufundishwa masomo ya darasa la 5, 6 na 7 katika kipindi cha mwaka mmoja, halafu afanye mtihani wa mwisho.
 
Unaweza kumrusha... Isitoshe yanayosomwa la 5-7 ni hayohayo ataenda kuyasoma form one.

Nimeshuhudia watoto wengi tu wamerushwa madarasa.

Ila tatizo naloliona ni wanakua 'wanakua (growth)' wadogo kiakili za maisha wakati wamemaliza madarasa mengi. It's like you robe their childhood life

Mtazamo wangu tu kwa navyoona..... Kuna mtoto hapa alirushwa kutoka lanne hadi form one. Now ana miaka tisa yupo form two. Yaani ukimtoa darasani ni mtoto mdogo kabisa kiakili, anacheza na watoto wenzake wa 5/6 years. Anaendesha magari, katuni anazoangalia anazi apply hata nje (ufahamu wa kikubwa hana). Unaweza kumkuta anajenga nyumba ya matope anakwambia "The Pirates are coming".

Kama ni madarasa tu inawezekana, mrushe. Ila angalia na akili yake pia.... Kusoma darasa moja baada ya lingine kunaenda sambamba na ukuaji wa mtoto, kumjenga ufahamu wake nje ya masomo n.k

Asante sana kwa ushauri. Kuhusu akili nje ya darasa, siwezi kulizungumzia sana hilo lakini ninavyo muona, anajitambua.. Hofu yangu ipo kwenye ishu ya cheti cha darasa la saba. Kwamba, anaweza kusumbuliwa huko mbeleni. Inaweza kufika mahali, kikahitajika cheti chake cha darasa la saba. Hilo unalizungumziaje mkuu?
 
Shuleni waalimu wake wanashauri vipi? Nafikiri wao wana mchango mkubwa hasa katika kutaarisha maombi maalum ya matakwa yako kama kweli mtoto ana uwezo au la. Na pia kama itawezekana kifanya hivyo, basi mtoto apatiwe mtaala maalum kwa ajili yake ambao utamwezesha kufundishwa masomo ya darasa la 5, 6 na 7 katika kipindi cha mwaka mmoja, halafu afanye mtihani wa mwisho.

Hilo linawezekana kaka?
 
Bora afike LA 5 alafu ndio umreshi form one kiini chote cha Elimu kpo LA 5
Asante sana kwa ushauri bro. Vipi kuhusu suala la cheti cha darasa la saba? Haiwezi kumsumbua huko mbeleni?
 
english media??????
kwa jinsi ulivoandika inajulikana kabisa wala mtoto wako sio kichwa kiasi cha kurushwa madarasa.
kama ni kichwa basi sijui amerithi akili za nani?
unafanya vizuri darasani wewe halafu arushwe mtoto? kivipi?
mtoto anarushwaje toka darasa la nne hadi form 1? are you siriaz meen?
au mtoto si wako manake kwa hija unazojenga sidhani kama mtoto ana akili kiasi hicho

Hahaha bro hizo ni typing error tu mkuu. I meant to say English Medium
 
At least hyo anaweza akasom la tano kidogo aalf ukamrusha la sits mwaak huo huo, hapo afadhal maanakwa ufahamu wangu mimi ni kwamba la saba ndio hujenga msingi wa form 1, nakushaur lazima asome la 7
Mambo ya msigi yapo class six, lazima asome hilo darasa then amalizie la saba.
 
Usithubutu kufanya hivyo. Acha mtoto asome kwa hatua. Kila hatua ina maana yake. Background kubwa ya form one ni grade 5 na 6. Seven ni kukazia maarifa. Kama yuko bora kichwani akimaliza grade 6 rusha. Na atakuwa na 11 to 12 years. Mine 10 years grade 5 na yuko vizuri mvulana na sina Mpango wa kurusha hata darasa moja.
 
english media??????
kwa jinsi ulivoandika inajulikana kabisa wala mtoto wako sio kichwa kiasi cha kurushwa madarasa.
kama ni kichwa basi sijui amerithi akili za nani?
unafanya vizuri darasani wewe halafu arushwe mtoto? kivipi?
mtoto anarushwaje toka darasa la nne hadi form 1? are you siriaz meen?
au mtoto si wako manake kwa hija unazojenga sidhani kama mtoto ana akili kiasi hicho
Tutaibishana hadi lini wakuu?
Kukosea speli ndio kimo cha akili?
Je kuongea kiingereza kwa ufasaha au kuandika ndicho kipimo pekee cha akili?
Fikiri tena..mkuuu
Unaweza kuwa mkulima wa matikiti na hujasoma lakini una uwezo wa kupeleka mtoto shule
 
Asante sana kwa ushauri. Kuhusu akili nje ya darasa, siwezi kulizungumzia sana hilo lakini ninavyo muona, anajitambua.. Hofu yangu ipo kwenye ishu ya cheti cha darasa la saba. Kwamba, anaweza kusumbuliwa huko mbeleni. Inaweza kufika mahali, kikahitajika cheti chake cha darasa la saba. Hilo unalizungumziaje mkuu?
Ooh kama shida ni cheti haina shida kabisa. Kwanza ili kumrusha inakupasa kuongea na walimu wake shule. Shule watakupa tu cheti haina noma kabisa....
Kumbuka vyeti vinatolewaga na shule tu palepale
 
ameomba kurushwa?halafu cheti cha std 7 utampa wewe?...
 
Ooh kama shida ni cheti haina shida kabisa. Kwanza ili kumrusha inakupasa kuongea na walimu wake shule. Shule watakupa tu cheti haina noma kabisa....
Kumbuka vyeti vinatolewaga na shule tu palepale

Asante sana kwa taarifa kiongozi. Nilidhani vinatolewa na NECTA. Thanx alot bro
 
Mimi nakupa ushuhuda wangu binafsi. Katika elimu yangu ya shule ya msingi Nilisoma darasa la kwanza, la pili na kurukishwa hadi la nne (sijasoma darasa la tatu, tano, sita wala saba) nilivyofika darasa la nne nilifanya mtihani wa kujiunga na kidato cha kwanza na kufaulu kuingia kidato cha kwanza katika shule binafsi.

Nilifanikiwa kumaliza kidato cha nne na kuchaguliwa moja ya shule za serikali, nilimaliza kidato cha sita na kufaulu vizuri

Nilichaguliwa kujiunga chuo kikuu na kufanikiwa kumaliza kozi niliyokuwa nasoma bila tatizo.
Katika elimu yangu yote toka niruke hayo madarasa mpaka chuo kikuu sijawahi kufeli na kurudia darasa hata moja.

Kwa sasa nipo Katika moja ya taasisi ya serikali nawatumikia watanzania kwa moyo mkunjufu, kwa uwezo wangu na elimu yangu. Hapa kazi tu

Nategemea kuendelea kusoma shahada ya uzamili.


Changamoto
Katika elimu ya kidato cha kwanza hadi nne nilikutana na wanafunzi walionipita umri kwa kiwango kikubwa na mimi nilikuwa bado na akili ya kitoto.
Ila kwakuwa shule ilikuwa na maadili mazuri na walimu walikuwa wanalifahamu basi nilikuwa napata msaada vizuri.

N.B
Mtoto wako lazima akili yake iwe vizuri maana unaweza kuwa umemsaidia au umemuharibia.

Msingi wa elimu yake ya chini ni kitu muhimu kwa sababu vitu vingi vinajirudia katika elimu ya sekondari ila vinafundishwa kwa undani.

Tafuta shule yenye malezi mazuri, kuanzia darasani hadi kwenye maisha ya wanafunzi wanapokuwa nje kimasomo
 
Msubiri afike std 5 then umrushe' std 7...hapo tayar atakua amejengeka zaidi
 
NGOGO CHINAVACH : Nashukuru sana kwa maoni yako kiongozi. Vipi kuhusu ishu ya cheti cha darasa la saba? Maana ake kuna mdau ame raise issue ya darasa la saba hapo, anasema inaweza kuja kumsumbua hapo badae. Vipi kwa upande wako ilikuwaje?
 
NGOGO CHINAVACH : Nashukuru sana kwa maoni yako kiongozi. Vipi kuhusu ishu ya cheti cha darasa la saba? Maana ake kuna mdau ame raise issue ya darasa la saba hapo, anasema inaweza kuja kumsumbua hapo badae. Vipi kwa upande wako ilikuwaje?
Katika mlolongo wangu wa maisha sijawahi kuulizwa cheti cha darasa la saba ila unachoweza kufanya ni kuchukua barua kutoka shule aliyosoma ikianisha kwamba alisoma hapo na namba yake ya usajili.
 
Back
Top Bottom