Nataka kumrusha mtoto darasa

Nataka kumrusha mtoto darasa

Mkuu ushauri uliopewa ni mzuri ila kwa kuongeza tu kabla hujamrusha kaa na,walimu wake wa masomo yote wakupe maoni yao juu ya uwezo wa mwanao ukiachana na wewe mwenyewe kuuona uwezo wa mwanao,pia na kama mkikubaliana arushwe form one basi kwanza mrushe la saba uone maendeleo yake ukiona yupo vzur basi kabla hajamaliza unaweza kumrusha form one.ushauri wangu
 
Wee jamaa mbona unaharaka sana ya mwanao kumaliza shule? unataka ule mahari ya fasta fasta nini!

Na usawa huu wa Magufuli kulivyo hamna hela unaweza ozesha mtoto wa kike wa miaka 10 ili ule hela ya mahara
 
cheti cha darasa la 7 ni muhimu kwa nacho, huwezi jua mkuu huenda siku za usoni kukahitajika sana.
 
Atakua kilaza huko sekondari. Walioweka hizo step hawakua vilaza. Na shule zinazojielewa hawawezi mpokea. Subiri afike darasa ya sita labda ndo anaweza kwenda sekondari. Haraka ya nini? Unataka umuozeshe akiwa na miaka 18 au???
 
hakikisha anasoma la Saba ....mrushe la nne had la sita
Kwani la saba lina umuhimu gani? Mi naonaga ni marudio tu! Kuna msichana tulikua nae form one, aliishia la sita na alituburuza vizuri tu na kutoka na division one.
Kuna shule moja pia naijua wanafunzi wanaofanya vizuri wa la sita wanapelekwa kufanya interview za kuingia form one. Atakaefaulu anaendelea na sekondari yake.
 
Kama unaangalia hapo hapo ulipo, maana yake umeona CHETI CHA DALASA LA SABA si muhimu! Hapo unajidanganya, Cheti cha darasa la 7 ni muhimu sana kuliko hata cha form 4 hata kwenye majeshi wanaaulizia sana cheti cha darasa la 7 hii inamaanisha inaondoa utata kwenye masuala ya Uraia.

Acha kumuwekea misingi.mibovu mwanao na baadaye aje akulaani. Mwache amalize shule ya msingi.
Kumbe kuna vyeti vya lasaba? Mi sikupataga.
 
Mimi ni tofauti kidogo na mwanao ,mimi nilipofika la Sita shule iliniombea kibali cha kufanya mtihani wa la Saba maana nilikuwa nipo vizuri sana kwenye masomo na nilikuwa shule ya msingi za kayumba sio kama ya mwanao,lakini nilifanya mtihani wa la Saba nikafaulu nikaenda form one nikakaza msuri tena nilipofika form three nikaomba mtihani wa form four pia nao nikafaulu baada ya hapo nikaendelea kama kawaida mpaka chuo lakini dalasa la saba na form four sijasoma, ili mambo haya yote yanawezekana ikiwa ataombewa kibali kutokana na uwezo wake.
Aiseee ww jamaa ni kichwa sana
 
Kumrukisha madarasa mengi sio busara, mrukishe moja then baada ya 2yrs waweza mrukisha jingine
Ukimrukisha madara mengi, mtoto hatakua socially ila atakuwa mentally na maybe physically but atakuwa analack baadhi ya vitu socially na itamsababishia matatizo mbeleni
 
Nilishuhudia schoolmates wangu wakiishia darasa la tano to pre form one na kuna classmates wangu kama watatu waliishia std six nikawakuta secondary wakiwa wanafanya vyema tu kama kawaida na hawakuwa vipanga primary sababu hawakuwahi hata kunizidi kwenye mitihani.

USHAURI:Washirikishe walimu wake hasa wa maths na Science lakini to me nashauri asome la tano then aende kikubwa awe fluent kwenye ngeli.

Binafsi mother alikataa pamoja na kushauriwa na mwalimu wangu.
 
Back
Top Bottom