Je bado Una maoni hayo hadi sasa? Je bado mwala au ndo mshaliwa? Hatukutilia shaka hao matapeli bali tulijua kabisa hatima ya ponzi ni wachache kufaidi vijisenti na wengi kupoteza mamilioni ya fedha zao. Kifuatacho sasa ni kwenda polisi kushtaki kampuni ambayo haijulikani ilipopotelea na kulaumu Benki Kuu. Kumbuka tamaa mbele mauti nyuma.Usilolijua ni kama usiku wa Giza. Nyie endeleeni kuwa na mashaka wakati wenzenu twala, tena kiulaini bila jasho wala bughdha.
Yaani kuitilia shaka Kaylanda ni sawa na wapinga chanjo ya CORONA ambao hadi leo wanasubiri waliochanja wageuke mazombi.