Nataka kujitolea kufundisha computer subjects

mashizo

Member
Feb 24, 2009
43
32
wadau kuna plan nafikilia kuja kufundisha masomo ya computer hasa kwa vijana wetu wa shule za msingi,nitaanza mwakani nikiwa hai,nitafundisha bure bila ya malipo,na vilevile nina mpango wa kuzitengenezea baadhi ya shule za msingi websites ambazo maelezo muhimu kuhusu shule husika yatakuwepo hii ni kuendana na teknolojia ya karne ya ishirini na moja

nawaomba wale watanzania wenzangu ambao mpo fiti kwenye suala zima la computer,mnishauri je huu mpango mzuri au wadau mnanishauri nn kuhusu ili suala?

nakaribisha maoni yenu wakuu
 
Ushauri tena mkuu wakati umeshaamua na naona kama umedhamiria?

Kwa kifupi kufanya any volunteer work (kind of pro bono publico) ni jambo zuri na la kuigwa.

Nakutakia kila la kheri, ila usikimbili kwenye English Medium school anza na hizi za kina Kanumba hapo ndo utakuwa umesaidia kweli
 
Basically mpango ni mzuri, ila ungetoa details tungekushauri zaidi. Utaufanikisha vipi huo mpango? Machine, sehemu ya kufundishai utatoa wapi? Utaugharamia vipi huu mpango?
 
wadau kuna plan nafikilia kuja kufundisha masomo ya computer hasa kwa vijana wetu wa shule za msingi,nitaanza mwakani nikiwa hai,nitafundisha bure bila ya malipo,na vilevile nina mpango wa kuzitengenezea baadhi ya shule za msingi websites ambazo maelezo muhimu kuhusu shule husika yatakuwepo hii ni kuendana na teknolojia ya karne ya ishirini na moja

nawaomba wale watanzania wenzangu ambao mpo fiti kwenye suala zima la computer,mnishauri je huu mpango mzuri au wadau mnanishauri nn kuhusu ili suala?

nakaribisha maoni yenu wakuu

Mpango mzuri binafsi nilishajaribu kufanya hiki kitu nikashindwa Nilianzia kwa walimu binafsi wa shule chache za msingi hawakuelewa somo nikhamia kwa kwa diwani nikampa somo kuwa nataka niwapige shule za jirani na uswazik aribu na ninapokaa kila jumamosi niwapige shule Basi zoezi likawa gumu utadhani nilikuwa natafuta ufaya kazi kwamalipo malipo.

Baada ya mwezi mzima kuonrnise mambo nikakata tamaa.....

Sasa sijui wewe utaanzaje Sijui uende kwa walimu wakuu bina fsi wa shule za msingi au uende manispaa au....

Yaaaani kwa kweli ha katika mazingira ya volunteering ni mgumu sana. But usikate tamaa jaribu mbinu utayofnnikisha utujulishe nasi labda inaweza kufanikisha .

Ukienda kwa walimu binafsi watakumbia hilo suala hawawezi mpaka wizara au halmashauri. labda utafute kamati ya wazazi wa shule fulani uwaeleze.

vile vile unaweza kuwalenga wanafuzi wa primary ukakuta hata walimu wao wako interested sijui itakuwaje. Maaana nilikutana na kesi hiyo.
 
kiufupi ni kwamba nina laptop zangu mbili,nitanunua projector moja,na nitafundisha hizi shule za kata maana ndio tulipotokea huko nazijua shida zao,na kuhusu masomo nitawafundisha basic computer programs,kwa mfano vijana wajue windows aina zote,simple software kwa mfano microsoft office,photoshop ikiwezekana itategemea na uelewa wao wa masuala haya ya computer,ila tatizo lipo kwenye umeme sijui kama hizi shule madarasani kuna sockets za umeme au umeme wenyewe kama vikiwepo basi itakuwa kheri sana.naomba ushauri zaidi wakuu
 
kiufupi ni kwamba nina laptop zangu mbili,nitanunua projector moja,na nitafundisha hizi shule za kata maana ndio tulipotokea huko nazijua shida zao,na kuhusu masomo nitawafundisha basic computer programs,kwa mfano vijana wajue windows aina zote,simple software kwa mfano microsoft office,photoshop ikiwezekana itategemea na uelewa wao wa masuala haya ya computer,ila tatizo lipo kwenye umeme sijui kama hizi shule madarasani kuna sockets za umeme au umeme wenyewe kama vikiwepo basi itakuwa kheri sana.naomba ushauri zaidi wakuu

Kwa experince ndogo japo sikufanikiwa anza na walimu kwanza wa primry kwanza. Nadhani ukiwalenga walimu complication zitapungua. then utahami kwa waafunzi may be wa class six and seven. carriculum inayofaa usichague wewe. tafuta carricum wanazofundishwa age group husika kwa shule za majuu.

Maana caricullum mtu amabye hajui computer aliyamaliza form four ni tofauti na mtu amabye hajui computer ambaye hajamaliza la saba. Na carriculm y mwalimu wa shule ambaye hajawai kugusa komyuta nayo ni tofauti na hao wawili niliowataja mwanzo.
 
Basically mpango ni mzuri, ila ungetoa details tungekushauri zaidi. Utaufanikisha vipi huo mpango? Machine, sehemu ya kufundishai utatoa wapi? Utaugharamia vipi huu mpango?
Kwa Mawazo yangu mimi nionavyo itabidi apate Wafadhili kwani huo mpango anaokusudia ni wa bure lakini una gharama sana sasa atakuwa akifundisha shule moja? au atakuwa akienda kila shule Kufundisha?Na tena mji gani aliokusudia kufundisha? hayo ndio maswali yangu ninauliza.......
 
Kwa Mawazo yangu mimi nionavyo itabidi apate Wafadhili kwani huo mpango anaokusudia ni wa bure lakini una gharama sana sasa atakuwa akifundisha shule moja? au atakuwa akienda kila shule Kufundisha?Na tena mji gani aliokusudia kufundisha? hayo ndio maswali yangu ninauliza.......

Wafadhili wa kazi gani tena mkuu, hii low self-esteem inatoka wapi tena?
 
Endelelea na wito wako kama unaona upo ndani ya uwezo wako mkuu. Kila la kheri.
 
Kwa experince ndogo japo sikufanikiwa anza na walimu kwanza wa primry kwanza. Nadhani ukiwalenga walimu complication zitapungua. then utahami kwa waafunzi may be wa class six and seven. carriculum inayofaa usichague wewe. tafuta carricum wanazofundishwa age group husika kwa shule za majuu.

Maana caricullum mtu amabye hajui computer aliyamaliza form four ni tofauti na mtu amabye hajui computer ambaye hajamaliza la saba. Na carriculm y mwalimu wa shule ambaye hajawai kugusa komyuta nayo ni tofauti na hao wawili niliowataja mwanzo.

Kwa hao wa primary hakuna haja ya kwenda majuu kutafuta hiyo mitala ya computer,watafute wadau wa elimu wa hapa bongo watakupa mitala ya kibongo.....kama sijakosea watoto hao wanasoma maswala ya CTI!
 
Hili suala jana usiku nilipita mezani nikakutana kajomba kangu anasoma darasa la sita mara nakagua vitabu vyake nakutana na kitabu kimeandikwa TEHAMA nikamuuliza nini hii akasema anko computer.Baada ya kufunua ndani nikakutana programu andishi sasa hapo kuanzia word,excel na masuala ya printa yamechambuliwa hapo ila lugha imebadilishwa kiswahili ya kuna maneno mageni sana kama chatazi,pau n.k kwa hiyo mdau nakushauri tafuta kwanza mitaala hii kwanza then kamua ndo uende huko la sivyo utabaki kusema highlight word badala ya kuumbiza neno {lol!!}.
 
Hili suala jana usiku nilipita mezani nikakutana kajomba kangu anasoma darasa la sita mara nakagua vitabu vyake nakutana na kitabu kimeandikwa TEHAMA nikamuuliza nini hii akasema anko computer.Baada ya kufunua ndani nikakutana programu andishi sasa hapo kuanzia word,excel na masuala ya printa yamechambuliwa hapo ila lugha imebadilishwa kiswahili ya kuna maneno mageni sana kama chatazi,pau n.k kwa hiyo mdau nakushauri tafuta kwanza mitaala hii kwanza then kamua ndo uende huko la sivyo utabaki kusema highlight word badala ya kuumbiza neno {lol!!}.

Kichakata matini, puku, programu endeshi, wavu wa walimwengu (www) KISARA (kioneshi sanifu rasilimali - url hiyo), mwambaa kazi, rambaza, teua, kitambazo, kisuduru, kichakata mikro, diski tepe, n.k
 
Kaka kwanza nikupongeze kwa kufikiria jambo kama hili, kwa ushauri wangu ungeanza na kuandika plan kamili ya project kuanzia unapotaka kuanza hadi unapokusudia kufika hata kama ni baada ya miaka mitano, hii itakusaidia kuwa na vision na malengo, badala ya kuanza shagahala baghala halafu ndio baada ya mwezi unaacha kwa vile hujui wapi unataka kufikia.

Baada ya hapo ungetafuta jinsi ya ku-finance "mradi wako" baada ya kutoka kwenye phase ya "laptop mbili" kwenda phase ya pili. Pia kama ungependa uwe ni mradi wa kuendelea fikiria kuwa utahitaji watu kwani huwezi kufundisha shule 10 peke yako, ni vipi utaweza kuwapata sahihi wakushirikiana nao huku wakitambua lengo nini.

Nisingependa kukuchosha kuandika sana, ila fikiria sana kufanya contact na walimu wa mashuleni, wafanyakazi wa wizara ya elimu na sehemu nyingine husika ili ujue nafasi ya jambo kama hili, waliokushauri masuala ya nini utafundisha wametoa ushauri wa msingi sana badala ya kufikiria kufundisha "basic programmes" kama ulivyosema mwenyewe.

Mwisho kabisa naomba nikusisitize kuhusu Plan, kuna msemo kwamba "if you fain to plan you are planning to fail". kwa hiyo jitahidi sana plan yako iwe viable na iyenye kuweza kutekelezeka bila ya kutaka mambo makubwa yasiyowezekana, plan ni muhimu na huenda ikawa sababu ya kuvutia wafadhili na watu wakujitolea kuendeleza wazo lako. Nakutakia kila la kheri.
 
Computer inahitaji mazoezi so hao wanafunzi ukisha wasomesha na laptop zako then ukachomoka nazo, itakuaje na shule hamna PC-u must me sponsored i thnk-GOOD WORK BY THE WAY
 
jamani mkusanyieni hiyo misamiati na tafsiri yake ili aanza kuzizoea.... Hiyo tafsiri ya URL nimeipenda!
 
wadau kuna plan nafikilia kuja kufundisha masomo ya computer hasa kwa vijana wetu wa shule za msingi,nitaanza mwakani nikiwa hai,nitafundisha bure bila ya malipo,na vilevile nina mpango wa kuzitengenezea baadhi ya shule za msingi websites ambazo maelezo muhimu kuhusu shule husika yatakuwepo hii ni kuendana na teknolojia ya karne ya ishirini na moja

nawaomba wale watanzania wenzangu ambao mpo fiti kwenye suala zima la computer,mnishauri je huu mpango mzuri au wadau mnanishauri nn kuhusu ili suala?

nakaribisha maoni yenu wakuu
kuna Mzee mmoja wa Arusha namfahamu nae ana wazo zuri kama lako mkuu, endeleeni na moyo huo huo mtazidishiwa na Mola...
 
Back
Top Bottom