Ozzie
JF-Expert Member
- Oct 9, 2007
- 3,217
- 1,259
Habari wakuu,
Mimi nimekuwa nafanya kazi na wajerumani katika mradi fulani hapa Tanzania. Niliajiriwa nao pindi tu nilipomaliza degree ya kwanza, bahati nzuri baada ya kukaa nao kama miezi nane tu (2007) nikapata bahati ya kwenda kusomea degree ya pili kwa muda wa miaka mitatu (mambo ya Afya).
Nilipata udhamini wa DAAD, ( ambapo huyu mwajiri anawafahamu watu wa DAAD (Wajerumani wenzake) hivyo alinikingia kifua; Na nikapata nafasi ya udhamini kirahisi sana).
Kabla sijaondoka mwajiri aliniingiza kwenye mkataba wa kufanya nao kazi kwa miaka mitatu baada ya kumaliza masomo au kulipa kiasi kinacholingana na udhamini. Kwa kuwa nilikuwa desperate kwenda kusoma wala sikuhoji sana ule mkataba.
Mdhamini niliyempata alinilipia kila kitu cha shule kwa miaka miwili, mwaka wa tatu huyu mwajiri wangu alinilipia ada (kama 12,000,000/=), lakini 50% ikakatwa kwenye mshahara wangu na 50% alichangia mwenyewe.
Muda wote nikiwa masomoni, nilikuwa nikilipwa nusu mshahara na huyu mwajiri, akidai hiyo ndiyo policy yake ( lakini pale anapotaka kunibana kwa vitu vingine huwa anatumia policy za serikali.
Nimerudi kazini mwaka jana mwezi wa tisa, tukaanza kushindana kuhusu mshahara baada ya kuniongezea pesa kiduchu. Amekataa kabisa kuniongezea mshahara, akidai ananilipa sawasawa na scale yangu, japo kuna vijana wenye degree moja ambao walikuja kazini baada ya mimi kuajiriwa wanalipwa mara mbili yangu (Sielewi hiyo scale ikoje, maana sijawahi iona).
Wiki iliyopita nimemwambia ninataka ni resign, ambapo anaonesha kutokubali hata kidogo, japo mwisho wa siku itabidi iwe hivyo.
Kwa sasa anapiga hesabu ya kiasi anachonidai ili kuni release.
Kuna vitu kadhaa vinanipa utata:
1. Ilikuwa haki kwa mimi kulipwa nusu mshahara kwa miaka yote mitatu?
2. Ninaamini huyu jamaa atahesabia udhamini wa DAAD kwenye malipo anayotaka arudishiwe, je ni sahihi (naamini siyo sahihi) maana DAAD
sikuingia nao mkataba wowote zaidi ya kuji commit kufanya kazi Africa kwa miaka mitatu.
3. Hivi ninaweza daiwa hata huo nusu mshahara niliokuwa naupata kwa miaka mitatu nikiwa shule?
Wasalaam
Mimi nimekuwa nafanya kazi na wajerumani katika mradi fulani hapa Tanzania. Niliajiriwa nao pindi tu nilipomaliza degree ya kwanza, bahati nzuri baada ya kukaa nao kama miezi nane tu (2007) nikapata bahati ya kwenda kusomea degree ya pili kwa muda wa miaka mitatu (mambo ya Afya).
Nilipata udhamini wa DAAD, ( ambapo huyu mwajiri anawafahamu watu wa DAAD (Wajerumani wenzake) hivyo alinikingia kifua; Na nikapata nafasi ya udhamini kirahisi sana).
Kabla sijaondoka mwajiri aliniingiza kwenye mkataba wa kufanya nao kazi kwa miaka mitatu baada ya kumaliza masomo au kulipa kiasi kinacholingana na udhamini. Kwa kuwa nilikuwa desperate kwenda kusoma wala sikuhoji sana ule mkataba.
Mdhamini niliyempata alinilipia kila kitu cha shule kwa miaka miwili, mwaka wa tatu huyu mwajiri wangu alinilipia ada (kama 12,000,000/=), lakini 50% ikakatwa kwenye mshahara wangu na 50% alichangia mwenyewe.
Muda wote nikiwa masomoni, nilikuwa nikilipwa nusu mshahara na huyu mwajiri, akidai hiyo ndiyo policy yake ( lakini pale anapotaka kunibana kwa vitu vingine huwa anatumia policy za serikali.
Nimerudi kazini mwaka jana mwezi wa tisa, tukaanza kushindana kuhusu mshahara baada ya kuniongezea pesa kiduchu. Amekataa kabisa kuniongezea mshahara, akidai ananilipa sawasawa na scale yangu, japo kuna vijana wenye degree moja ambao walikuja kazini baada ya mimi kuajiriwa wanalipwa mara mbili yangu (Sielewi hiyo scale ikoje, maana sijawahi iona).
Wiki iliyopita nimemwambia ninataka ni resign, ambapo anaonesha kutokubali hata kidogo, japo mwisho wa siku itabidi iwe hivyo.
Kwa sasa anapiga hesabu ya kiasi anachonidai ili kuni release.
Kuna vitu kadhaa vinanipa utata:
1. Ilikuwa haki kwa mimi kulipwa nusu mshahara kwa miaka yote mitatu?
2. Ninaamini huyu jamaa atahesabia udhamini wa DAAD kwenye malipo anayotaka arudishiwe, je ni sahihi (naamini siyo sahihi) maana DAAD
sikuingia nao mkataba wowote zaidi ya kuji commit kufanya kazi Africa kwa miaka mitatu.
3. Hivi ninaweza daiwa hata huo nusu mshahara niliokuwa naupata kwa miaka mitatu nikiwa shule?
Wasalaam