Habari wakuu.
TPDC wametoa post za kazi, deadline 27 june. Mimi kufika hiyo tarehe nitakua nimeshamaliza chuo (Geologist) so nimependa ni apply nijaribu baht yangu. Ila nina maswali naomba mnisaidie:
-Watakubali provision results yenye matokeo ya semester 5?
-Kuna watu wanasema eti barua za application lazima zitumwe kwa EMS, je ni kweli? Wanadai kwa posta ya kawaida zinaweza kukaa ata mwezi mzima njiani.
-Ni mgeni ktk ku apply kazi, hivi unaruhusiwa kuomba zaidi ya kazi moja iwapo wametoa kazi tofauti tofauti? Yaani niandike barua ya kuomba kazi A, Kazi B au hadi Z?
Nitashukuru nikipata Majibu.