goodmother
Senior Member
- Jul 21, 2012
- 108
- 80
Mkuu hii technology inaonekana inahitaji joto kati ya 17 mpaka 24 degree centigrade, vipi kwa ukanda huu wa pwani tunafanyaje??Kuhusu maji kama vile haiitaji maji mengi sana Mama Joe, nimeona walio kwenye eneo kama sana huko kenya wakifaidika na technologia hii.
Zipo Gwata mbili, mimi nazungumzia Gwata ya Kisarawe. Kama ukifika Mzenga, kuna njia inakwenda Mafizi kupitia Mwanamsekwa, Nyani hadi Gwata. Gwata pana watu wengi sana,wakulima na wafugaji,usafiri wa bus kuja Buguruni upo kila siku, usafiri wa tren upo. Ardhi ipo nzuri sana kando ya mto Ruvu. Lipo gulio kubwa kwa siku nne mfululizo,la mifugo zaidi. Biashara ya nyumba za wageni inalipa sana kuanzia alhamisi mpaka jumapili.
H/shauri ya Kisarawe wanataka kujenga mnada wa kisasa pale,viwanja vimepanda bei vibaya baada ya plan hiyo kuwekwa peupe. Mimi nilifuata ardhi ya kuotesha cocoa. Jamaa zetu Waarabu wamekomba mapande ya ardhi kinoma. Sijasikia ugomvi wa ardhi kule. Maji ni mto Ruvu, ni nguvu yako. Na migomba inamea pia.
Gwata ya pili iko Migindu huko Chalinze,
Swali lingine kaka!!!!!!!
Je Gwata ya kisarawe kuna umeme wa uhakika
Malila za sikukuu! Asante kwa ushauri, nimepata Msata, Chalinze. Tutakutafuta kwa ushauri zaidi, ngoja sikukuu iishe.
Msata,ipi.
Je ni Kihangaiko, au Madesa, au hii njia ya kuja Bagamoyo? Mimi niko Madesa kuelekea Mkoko. Siku twende pamoja dada.
Ni Mazizi kwa kweli ni njiapanda kijiji kiko kama km 3 kutoka njia panda ya Msata unakuwa unarudi Moro ukitokea Kiwangwa, kushoto. Nadhani patanifaa ingawa bado nafanya utafiti zaidi, udongo ni mzuri sana mitiki, migomba, mahindi, miembe na nanasi vimekubali. Na bei sio mbaya ila naangalia maji kwa mifugo kama yao ingawa kuna ngombe wengi mtu kafuga. Tutatafutana ukaone.
Wakuu natafuta shamba la kununua lenye ukubwa usiopungua hekari 30, kwa ajili ya project yangu ya kilimo mwaka ujao ninayotegemea kuifanya nje kidogo ya jiji la Dar es Salam, shamba hilo naomba liwe na sifa zifuataazo:
- Liwe na ardhi yenye rutuba kwa ajili ya kilimo hususani mahindi
- Liwe eneo lenye water-table iliyo karibu, eneo ambalo nikichimmba kisima cha ku-drill nitapata uhakika wa maji kuanzia lita 5,000 kwa siku, na iwe ni kwa mwaka mzima.
- Liwe pembezoni mwa mji lakini umbali usizidi km 50 kutoka Dar es Salaam.
- Liwe linafikika kwa urahisi kwa gari kwa ajili ya kusafirisha mazao yangu kutoka shambani
- Uwepo wa umeme japo si muhimu sana
Kwa mwenye kuwa nalo au yeyote mwenye kuuza naomba tuwasiliane hapa au kwa PM hususani kwa mambo kama bei, vibali na location.
Natanguliza shukrani
Pazuri pale,
Upande uliopata una bomba la maji la Wami. Ila nikukumbushe kitu mapema, jitahidi kupata eneo la kutosha kabisa.
Wakuu natafuta shamba la kununua lenye ukubwa usiopungua hekari 30, kwa ajili ya project yangu ya kilimo mwaka ujao ninayotegemea kuifanya nje kidogo ya jiji la Dar es Salam, shamba hilo naomba liwe na sifa zifuataazo:
- Liwe na ardhi yenye rutuba kwa ajili ya kilimo hususani mahindi
- Liwe eneo lenye water-table iliyo karibu, eneo ambalo nikichimmba kisima cha ku-drill nitapata uhakika wa maji kuanzia lita 5,000 kwa siku, na iwe ni kwa mwaka mzima.
- Liwe pembezoni mwa mji lakini umbali usizidi km 50 kutoka Dar es Salaam.
- Liwe linafikika kwa urahisi kwa gari kwa ajili ya kusafirisha mazao yangu kutoka shambani
- Uwepo wa umeme japo si muhimu sana
Kwa mwenye kuwa nalo au yeyote mwenye kuuza naomba tuwasiliane hapa au kwa PM hususani kwa mambo kama bei, vibali na location.
Natanguliza shukrani
Bei yako ikoje mkuu???Kuna 29 acres pale Viazi, less than 30 km from Dar city centre. lina sifa zote. Except umeme unahitaji bidii kidogo
Mkuu hilo halina sifa kabisa,zinahitajila hekali 30!Kuna shamba kisalawe lina hekali24 lina sifa zote ila lipo km,60 kutoka dar
Kuna 29 acres pale Viazi, less than 30 km from Dar city centre. lina sifa zote. Except umeme unahitaji bidii kidogo
Sio viazi ni vianzi,tatizo la jamaa wa vianzi wana uza kwa tamaa kuna jamaa alitaka aniuzie shamba ekali 2 kwa m8.....
Nenda Bupu au Tundu, huko unaweza kupata kwa laki tatu eka moja, tatizo ni usafiri wakati wa masika.Hakuendeki huko wakati wa masika.
Asante sana walinitajia kuhusu bomba ila sikuamini, ni kweli nimechukua kiasi ila nimeshika pande jingine pia naamini nitawezeshwa tu nimalizie. Barikiwa
Aisee Malaila na Mama Joe mmeufanya huu uzi uzidi kiwa wa maana sana, Mbarikiwe sana. Hayo maeneo Mama Joe mashamba bado yanapatikana, bei yao ikoje?