Natafuta plot Arusha Njiro au Moshono

Natafuta plot Arusha Njiro au Moshono

Na ukumbuke miundombinu yote ipo maji Umeme barabara na ulinzi.
 
Na ukumbuke miundombinu yote ipo maji Umeme barabara na ulinzi.
huko pia lazima nitatafuta mkuu. nalenga pia kuishi karibu na nitakapofanyia kazi, MAHAKAMA KUU.
 
ni sehemu ipi arusha ukijenga ni sehemu ya middle class, at least hakuna uswahili, kila mtu anajua yake? please watu wa arusha nisaidieni.
Cheki Tengeru, very accesible. Opposite na Mountain village. Viwanja vimepimwa. Huduma zote zimo
 
huko pia lazima nitatafuta mkuu. nalenga pia kuishi karibu na nitakapofanyia kazi, MAHAKAMA KUU.
Kama Mahakama Kuu nenda kanunue Sekei the other side of Mt. Meru hotel. Eneo halisumbui maji hata kidogo na ni Jirani na kazini kwako just a walking distance.
 
View attachment 643801
Wakuu, natafuta kiwanja cha kujenga Arusha eneo la Njiro au Moshono, kisipungue nusu eka, eneo linalofikika lenye huduma zote, offer mkononi ninayo 30m. kwa atakayekuwa nacho, kinahitajika haraka, na unatakiwa kuweka specification za kiwanja hizo zote hapa na uweke na picha na mazingira yalivyo. pia, kiwanja kiwe kina hati (kwani nitapita ardhi kuserch), kama una mke au mume, hakikisha wanandoa wote mnaridhia kuuza na wote mtaingia kwenye mkataba na transfer ya ardhi. thanks.
 
Wakuu, natafuta kiwanja cha kujenga Arusha eneo la Njiro au Moshono, kisipungue nusu eka, eneo linalofikika lenye huduma zote, offer mkononi ninayo 30m. kwa atakayekuwa nacho, kinahitajika haraka, na unatakiwa kuweka specification za kiwanja hizo zote hapa na uweke na picha na mazingira yalivyo. pia, kiwanja kiwe kina hati (kwani nitapita ardhi kuserch), kama una mke au mume, hakikisha wanandoa wote mnaridhia kuuza na wote mtaingia kwenye mkataba na transfer ya ardhi. thanks.

Kwa budget hiyo Njiro vilivyopimwa vizuri sana vimejaa, angalie usije uziwa mara 2 tu, ila vimejaa
 
t
Kama Mahakama Kuu nenda kanunue Sekei the other side of Mt. Meru hotel. Eneo halisumbui maji hata kidogo na ni Jirani na kazini kwako just a walking distance.
thanks mkuu.
 
Njoo olasiti mkuu hutajuta. Utakua Jirani yangu hamna squatters bei ni nzuri sio kubwa Sana za kutisha
 
Mimi nauza kiwanja kipo gomba estate-
Gomba estate ni uelekeo wa wapi, mimi sio mwenyeji hapo, nilishakuja kwa kupita tu kama mara tatu hivi, napajua kisongo kule kwa ngurumo, napajua njiro, maeneo mengine huwa napita sijui ni wapi, nasimuliwa tu.
 
thanks, sehemu nzuri ni wapi mkuu. hasa ambako sio uswahilini...actually, nahamia arusha soon na sitaki nipange zaidi ya mwaka mmoja, hivyo nafika na kuanza kujenga ndo maana nataka kununua kiwanja soon after arrival. ila jueni mimi ni mwanasheria, najua due diligence ya kueleweka kabla ya kununua kitu hasa ardhi.
Mkuu mbona mikwala mingi sana
 
Zingatia ushauri wa wadau sasa hasa njiro na moshono
yap, itabidi niwe makini, kuuziwa mara mbili huwa inasumbua sana....sehemu gani nyingine ni ushuani mkuu zaidi ya njiro?
 
yap, itabidi niwe makini, kuuziwa mara mbili huwa inasumbua sana....sehemu gani nyingine ni ushuani mkuu zaidi ya njiro?
Kimsingi arusha maeneo yaliyopimwa ni machache kama njiro.na sehemu wadau walikotumia fursa kama huko ngaramtoni kuelekea nairobi. Otherwise sehemu nyingi ni ustaarabu tu wa wenyeji kuacha njia na kutemgeneza mitaa na ulinzi. Ningeshauri ujipe.muda wa kama mwezi mmoja ufanye survey mwenyewe ujiridhishe.
 
Kimsingi arusha maeneo yaliyopimwa ni machache kama njiro.na sehemu wadau walikotumia fursa kama huko ngaramtoni kuelekea nairobi. Otherwise sehemu nyingi ni ustaarabu tu wa wenyeji kuacha njia na kutemgeneza mitaa na ulinzi. Ningeshauri ujipe.muda wa kama mwezi mmoja ufanye survey mwenyewe ujiridhishe.
ushauri mzuri, lakini ungetoa pendekezo wapi maeneo pendekezi kwa uzoefu wako pia ingependeza mkuu.
 
matejoo ipo kama kuelekea wapi? sorry
Huko matejoo hapana.
Ni uswahili mnoo, pameshonana balaa, ni zaidi ya Tandale kwa Dar.
Matejoo(pia kunajulikana kama Osterbay) pako karibu na katikati ya mji, huwezi kupata kiwanja cha nusu heka unless ununue nyumba ya mtu na kuibomoa ili ujenge.
 
ni sehemu ipi arusha ukijenga ni sehemu ya middle class, at least hakuna uswahili, kila mtu anajua yake? please watu wa arusha nisaidieni.
Hali halisi iko hivi kwa Arusha.
Sehemu kubwa zilizotulia(Kama Njiro na Mushono) ni matokeo ya ustaarabu wa watu waliofika mapema na kujenga, baadhi zimepimwa(kila mtu binafsi kwa wakati wake) na nyingi hazijapimwa.

Sehemu pekee za uhakika wa kishua katika ujenzi uliopangika ni kama Safari City ambako ni mji mpya kabisa unaojengwa kwa vigezo na viwango huku huduma zote zikiwekwa.

USHAURI WANGU.
1/Fika kwanza wewe mwenyewe Arusha na tembelea maeneo yote uliyoambiwa na watu humu na kisha ujionee mwenyewe kabla ya kuamua pa kununua.

2/Katika manunuzi ya viwanja hapa Tanzania usitangulize pesa mbele, maana biashara ya viwanja ni soko holela sana, hakunaga bei rasmi au elekezi. Ukishaweka pesa mbele tegemea kulizwa vibaya, madalali na matapeli wamejaa mjini na hizo ndio fursa zao za kuvuna pesa chap chap kwa watu wasiojua.

3/Ukitaka kununua kiwanja katika mji mgeni kwako ni vyema ukaongozwa na mtu wako wa karibu kama ndugu au rafiki yako mkubwa unayemwamini ambaye ana uenyeji wa kutosha katika eneo husika. (Katika hili, ninakushauri kwa sasa usiwaze kabisa kukimbilia kununua kiwanja Arusha, Fika kwanza Arusha na uishi kama mwaka mmoja hivi ili uijue vyema Arusha na kuwa mjanja wa mji huo, na kutokea hapo utajua wapi pa kuishi wewe, bei za viwanja na Eneo unalolitaka)
 
Back
Top Bottom