Natafuta Mume Umri 38-43

Natafuta Mume Umri 38-43

Habari wakuu, naingia leo jukwaa hii kutafuta mtu ambaye naweza kumuamini akawa mtu wangu wa karibu maishani. Natafuta mwanaume ambaye anaweza kuwa rafiki na mume.
Sifa zangu: Umri kati ya 35 na 38, Ninafanya kazi, Dini mkristo, Elimu zaidi ya degree ya kwanza. Nipo Dar es Salaam, nilishawahi olewa, na sina mtoto.
Sifa zake: Awe mkristo, Awe na shughuli halali inayomwingizia kipato, Umri 38-43, akiwa na mtoto sio tatizo. Elimu at least degree ya kwanza. Kwa walio serious tu. Karibuni.


sababu za kuachika? na mie navyojua ndoa ya kikristo hawachani. ex husband yupo alive? huna mtoto je unapanga kukaa maisha yote bila kuzaa?
 
Wewe Una Ukazi Na Nyumba? Maana Umesema Vigezo Na Masharti Yako
 
sababu za kuachika? na mie navyojua ndoa ya kikristo hawachani. ex husband yupo alive? huna mtoto je unapanga kukaa maisha yote bila kuzaa?
Sababu ataambiwa aliye interested, Ndoa ilikuwaje pia ataambiwa aliye interested, napanga kuzaa. Thanks.
 
sababu za kuachika? na mie navyojua ndoa ya kikristo hawachani. ex husband yupo alive? huna mtoto je unapanga kukaa maisha yote bila kuzaa?

Kumbuka sio kila unachopanga lazima kitimie, mingine mipango ya Mungu.
Nimedakia tu.
 
Mtu wa kanda ya ziwa, shule yangu ndefu kuliko unavyodhani.

Shule na ndoa ni vitu viwili tofauti...ndo maana hata MUNGU hakuhusianisha ndoa na shule,sijui kwa nn watanzania hua wanakosea hapa kwenye hili
 
Hapa jf sina hakika kama utafanikiwa dada yangu. Labda km unataka kutumika the wakudump.
 
Hapa jf sina hakika kama utafanikiwa dada yangu. Labda km unataka kutumika the wakudump.
Usijali nipo makini, ahsante. Naamini Mungu anatumia njia nyingi kuwakutanisha watu hii ni mojawapo.
 
Shule na ndoa ni vitu viwili tofauti...ndo maana hata MUNGU hakuhusianisha ndoa na shule,sijui kwa nn watanzania hua wanakosea hapa kwenye hili
Tunatofautiana mitazamo kaka yangu. Shule ina-matter sana tu, hasa katika mawasiliano ndani ya familia. Mkitofautiana sana inakuwa issue. Thanks.
 
Tunatofautiana mitazamo kaka yangu. Shule ina-matter sana tu, hasa katika mawasiliano ndani ya familia. Mkitofautiana sana inakuwa issue. Thanks.

Nakutakia mwendo mwema,majibu uyalete hapa pia baada ya kufanikiwa na usije ukadanganya chochote juu ya uliyempa,najua majibu yatachukua karibu miaka mitano au zaidi baada ya ujauzito na mtoto.
 
Kumbuka sio kila unachopanga lazima kitimie, mingine mipango ya Mungu.
Nimedakia tu.

acheni kumuonea MUNGU. wala hakupangii nini ufanye hapa duniani...amekupa uhuru wa kuchagua mema na baya...kazi ni kwako
 
Mimi nipo ninadiploma,nina 41,,nahitaji m2, if possible.UMRI WAKO PLS, dada take care huku kwenye mitandao,
 
acheni kumuonea MUNGU. wala hakupangii nini ufanye hapa duniani...amekupa uhuru wa kuchagua mema na baya...kazi ni kwako

Kama hajakubariki kupata mtoto je?
utasema mtu kachagua?
Kuna wanaume wagumba hujasikia? Wamechagua?
 
Back
Top Bottom