Natafuta mtu wa kunifadhili masomo yangu

Natafuta mtu wa kunifadhili masomo yangu

Pole sana.
Msomi wa Clinical Medicine.. (Japo sioni mahali uliyosema ni level ipi.. Certificate, diploma, advanced diploma au degree)..

Naomba nikushauri uandike vizuri aya zako ili tuzielewe.. Ainisha hitaji lako vizuri kwa mchanganuo.

Nakuombea mema hitaji lako na litimie.
Asante coupernicucci98 nimemaliza NTA level 4
 
Ulikuwa Unasoma chuo gani? Clinical Medicine ukimaliza Unakuwa nani?
Jibu haya ili anayefadhili ajue anasaidia nini.....!
Nilikuwa Victoria Institute of Health and Allied Science Mungu akinisaidia nikimaliza kwa level ya diploma nakuwa tabibu na nikijiendeleza na kupata degree nakuwa full Doctor
 
kwanini, umejitambulisha
[emoji117]Kuwa wewe ni msichana.
[emoji117]Halafu hujaweka Details za kutosha
(Jinsia itakubeba ila kuwa makini maana Jf wengi hawashoboekei wadada.)

Ushauri Wangu; Piga kazi, pata pesa, tunza pesa rudi chuoni. kuna mshikaji wangu naye yupo kitaa saizi ka stop anapiga job apate pesa then aendelee.
 
Hizi mishe za ada ziskieni tu, nilkua naskia skia juu juu ila since na mimi yamenikuta.. naelewa anachopitia sisteri hapo.. usikate tamaa Dada japo siku hizi watu ni wagumu.

Unajiuliza hivi ukoo wangu mzima wakiamua kujichanga 20 tu kwakila mmoja sipati ada!?.. mimi nlikosa 1.5 ya ada lakn ndugu yangu mmoja alinipa laki na nusu ya kupanga chumba ili nianze maisha lakin walishndwa kunichangia ada😅
 
Niongee kitu hapa ,hii familia im3shakua kua kubwa ni suala la wewe kujulikana uko wapi aidha kupitia Mods au jf member mwenzako ambaye yuko karibu nawe.
Baaada ya kuwabaini hapo ,hebu tulione hili wazazi wenzangu kwa kuangalia kila mmoja kwenye muamala wake wa siku moja ile mia mbili hamsini iliobaki 250Tsh tujitolee kuichanga tukiwa watu laki moja humu100000 mdogo wetu atasoma kwa faraja kabisa
Una uhakika ni mwanafunzi? Matapeli wana mbinu nyingi za kujipatia pesa zisizo halali
 
Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 23.

Shikamooni wa kubwa rikaa yangu habari zenu natumain wote ni wazima na mnaendelea vyema na jukumu la kulijenga taifa letu lenye kubarikiwa na Mungu TANZANIA...
Nakushauri mtafute Malisa au Msando tufanye mpango wa michango kupitia wao.

Ukiweza wasiliana na mbunge wako aanzishe fundraising itakuwa rahisi kukuchangia maana yawezekana unahitaji pesa haizidi milioni Saba ambayo ukiitumia watu wenye infuence atakupa support kuliko humu watu tunatumia fake IDs tutakukimbia.
 
Nilikuwa Victoria Institute of Health and Allied Science Mungu akinisaidia nikimaliza kwa level ya diploma nakuwa tabibu na nikijiendeleza na kupata degree nakuwa full Doctor
Tafuta watu wa karibu unaowafahamu, then waeleze shida yako vizuri, ikiwezekana wambie wakukopeshe uweze kumaliza masomo yako, ni ngumu sana hapa JF watu kukusaidia ukizingatia watu siku hizi wamebadirika, wasio na shida hujifanya kuwa na shida mwishowe wanawazibia misaada wale wanaostahili.
 
Nakushauri mtafute Malisa au Msando tufanye mpango wa michango kupitia wao.

Ukiweza wasiliana na mbunge wako aanzishe fundraising itakuwa rahisi kukuchangia maana yawezekana unahitaji pesa haizidi milioni Saba ambayo ukiitumia watu wenye infuence atakupa support kuliko humu watu tunatumia fake IDs tutakukimbia.
Nashukuru kwa wazo lako na mchango wako Mungu akubariki
 
Tafuta watu wa karibu unaowafahamu, then waeleze shida yako vizuri, ikiwezekana wambie wakukopeshe uweze kumaliza masomo yako, ni ngumu sana hapa JF watu kukusaidia ukizingatia watu siku hizi wamebadirika, wasio na shida hujifanya kuwa na shida mwishowe wanawazibia misaada wale wanaostahili.
Asante seniweba kwa mchango wako
 
Mungu wangu mimi sio tapeli nishida tuu izi ndo zinatufanya tuweke public privacy zetu lkn Mungu ndo anajua
Kuna tapeli amewahi kujisema?

Wengi wana sura za upole lakini ni hatari hao watu.

Kuna vitu nimeona wadau wanataka kujua kutoka kwako ili wafahamu wanaanzia wapi kukusaidia
 
Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 23.

Shikamooni wa kubwa rikaa yangu habari zenu natumain wote ni wazima na mnaendelea vyema na jukumu la kulijenga taifa letu lenye kubarikiwa na Mungu TANZANIA

Kama nilivyoeleza hapo juu ndugu zangu nimeona nililete hili kwenu kwa yeyote ataeguswa naomba anisaidie nimekwama kuendelea na masomo kwasabu ya kiuchumi mimi nilikuwa nasoma fani ya clinical medicine nimemaliza mwaka wa kwanza lakini niliacha kuendelea na masomo kwa sababu ya pesa na pia chuo nilichosoma ni cha private aliyekuwa anajichanga changa ili nisome kwa sasa hana pesa ni kwamba ameporomoka kiuchumi na nina mpango wa kutafuta chuo cha Government mwaka wa kwanza pamoja na kusoma kwa shida sana nilijitahidi nisipate sup, repeat module wala disco ili niendelee kumconvice mfadhili wangu aendelee kunilipia. Mungu alinisaidia nikapata GPA ya 3.0

Asanteni na Mungu awabariki
Kama upo siriazi naomba weka jina lako kamili na chuo ulichosoma, kilipo hiko chuo if possible mawasiliano ya chuoni na mwaka uliosoma tukijiridhisha tutachanga.Tukichanga hata 1000 kwa kila kichwa pasipo kujali watakaochanga zaidi, utarudi shule.Ila tuahidi hautadai rushwa ukipata ajira
 
Kama ni mkristo nakushauri kaongee na mchungaji wako akupe nafasi waumini wakuchangie..kama ni mwislamu nenda msikitini..

Humu wengi tuna comment tu ila swala la kumchangia mtu ni ngumu. Maana hatuna uhakika kama kweli ana shida ama ni msanii
Makanisani sikuhizi hata hawajali watu kama hawa wapo radhi wafanye harambee ya sherehe fulani kuliko kuchangia watu.So sad
 
Back
Top Bottom