PAMELA MS nakuombea kwa mwenyezi Mungu ili uweze kumpata mtu ambaye hasa mtaendana naye. Unajua watu wengi sana hukurupuka katika maamuzi ya kumchagua mtu ambaye anatakiwa aishi naye kama mke na mme. Ndoa ni taasisi ya kwanza kabisa kuasisiwa kwa ajili ya wanadamu, tena muasisi akiwa ni Mungu mwenyewe. Lakini, Shetani kwa kufahamu nini hasa kilikusudiwa katika ndoa, ameuharibu mpango huo mtakatifu wa Mungu. Lakini jambo kubwa la kukumbuka ni kwamba kila binadamu anapoumbwa, anaumbwa na yule atakayekuwa mke/mme wake, rejea kile ambacho Mungu alikifanya kwa Adamu kwa kumuumba Hawa kwa ajili yake. Kwa hiyo hakikisha unamuomba Mungu ili aweze kukupatia mtu ambaye hasa aliumbwa kwa ajili yako.
.
"WASIOSOMA NI CHAKULA CHA WASOMI".
.
"WASIOSOMA NI CHAKULA CHA WASOMI".