Natafuta mbwa watatu wa kukodi

Natafuta mbwa watatu wa kukodi

Daktari wa Meno

JF-Expert Member
Joined
Sep 5, 2019
Posts
509
Reaction score
1,617
Happy Boxing Day wana JF.

Naomba niende moja kwa moja kwenye lengo la uzi wangu. Najihusisha na ufugaji huku kanda ya ziwa ila nina changamoto ya chatu katika eneo langu hali iliyosababisha mifugo 5 kuuliwa ikiwemo mbwa wangu wawili aina ya Germany Shepherd ambao walimezwa katika kipindi cha miezi 6 iliyopita.

Mbuzi wangu wawili pamoja na kondoo watatu wamemezwa na chatu pia ndani ya mwaka mmoja uliopita. Sasa naona hali inazidi kuwa mbaya zaidi na ninatafuta mbwa watatu ili nione kama wataweza kupambana na chatu huyo.

Hivyo natafuta mbwa wenye nguvu watatu ambao nitawatumia ili nione kama nitafanikiwa kumuua huyu chatu.

Kama una mbwa wenye sifa hizo njoo PM tuone namna ya kufanya biashara.

Muda wa kukaa nao ni ndani ya siku 6 hadi wiki moja moja. Kama watakuwa wamemezwa basi tutarudi kwenye meza ya mazungumzo tuone tunafanya nini.

Karibu wakuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli watu sasa weshachanganya mambo. Hivi wajua hakuna mdudu rahisi kuua ka chatu aliyemeza kitu?? Sasa kama alimeza kondoo, mbuzi, mbwa huku wewe unamuangalia tu, unategemea aondoke hapo??
Elewa; Chatu akimeza kitu, huongezeka urefu na ukubwa kila amalizapo mlo wake tumboni. Sasa kama alimeza akiwa na unene wa futi 1, mlo wa kwanza, si ajabu sasa ana unene wa futi 2.
Ushauri; Huna haja ya kutafuta mbwa wa watu kuja kuliwa/kumezwa. Kumbuka, mbwa hana ujanja mbele ya chatu, Hutoa harufu fulani inayomlewesha mbwa anajipeleka mwenyewe kumezwa. Endapo atameza kondoo au mbuzi mwingine ngoja akiisha kumuingiza mdomoni tu, hata kabla hajamalizia kummeza, wewe nenda tu na hata panga uanze kumkatakata. hataweza kukimbia wala kumtema kwani meno yake huzuia kisitoke mdomoni bali kiingie ndani. Utakuwa umemuua chatu wako. Ukifanikiwa mrejesho hapa ni muhimu na malipo kwangu nilyekufundisha mbinu hii
 
Mkuu kama unaogopa tafuta watu wa kumuhamisha tena sio kumuuwa
Napenda sana viumbe hao
Inabidi uwasiliane na maliasili ili waje kumbeba kama utajua alipo au kama ukimuona kashiba ni rahisi sana kumdhibiti maana hana ujanja tena

tafuta wasaidizi na pipa tu mdumbukize humo na kazi imeisha



Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Mkuu kama unaogopa tafuta watu wa kumuhamisha tena sio kumuuwa
Napenda sana viumbe hao
Inabidi uwasiliane na maliasili ili waje kumbeba kama utajua alipo au kama ukimuona kashiba ni rahisi sana kumdhibiti maana hana ujanja tena

tafuta wasaidizi na pipa tu mdumbukize humo na kazi imeisha



Sent from my iPhone using Tapatalk
Nitajaribu kuzungumza na maliasili ila kuna nyakati nilitaka usaidizi wao wakauliza una shilingi ngapi. Nikaona acha nikomae naye pekee yangu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nitajaribu kuzungumza na maliasili ila kuna nyakati nilitaka usaidizi wao wakauliza una shilingi ngapi. Nikaona acha nikomae naye pekee yangu.

Sent using Jamii Forums mobile app

Ni maajabu tu ya hivi yanatokea kwenye nchi masikini kuomba hela wakati ni kazi yao
Katika miaka ya 1900 aliekuwa Rais wa USA Roosevelt alitoa dau la $1000 kwa yeyote atakaefanikisha kumkamata nyoka mkubwa wa kufikia urefu wa zaidi ya 30ft
Baadae dau lilipanda na kufika 5000 halafu 15,000 mwaka 1978
Na mnamo mwaka 1980 bila mafanikio dau likapanda mpaka $50,000
Hapo watu zaidi walichangamkia fursa na kwenda mpaka Amazon kupambana na Anacondas ili wapate huo mchongo ambapo watu wengi walipoteza maisha kwa tamaa na bila mafanikio
Sasa sisi huku badala ya idara kusaidia watu wao ndio wanatafuta madili



Sent from my iPhone using Tapatalk
 
We jamaa unajua unene wa futi moja kweli wewe? Hakuna nyoka wa hivyo duniani bana
Walami utawajua tu. Yaani mmezaliwa clinic mkakulia mtaani. Hata shamba la muhogo hujawahi kuliona. Sasa, nenda huko mikoani. Chatu anammeza ndama bila hata taabu yeyote. Wadhani anakuwa na unene gani kama sio futi 4?? Sikujaliwa kubishana na wasioamini
 
Uzi huu ulinifanya nipekue nione kana kuna nyoka mnene huo wa foot moja, nikagundua kuwa hupimwa kwa uzito na urefu, ambapo inakadiriwa nyoka mkubwa zaidi ana 222kg na urefu wa feet 30 sawa na mita 9.1.
Pia nikaona na dau sliloweka rais Roosevelt la $1000 na mwisho kabisa $50,000
Ni maajabu tu ya hivi yanatokea kwenye nchi masikini kuomba hela wakati ni kazi yao
Katika miaka ya 1900 aliekuwa Rais wa USA Roosevelt alitoa dau la $1000 kwa yeyote atakaefanikisha kumkamata nyoka mkubwa wa kufikia urefu wa zaidi ya 30ft
Baadae dau lilipanda na kufika 5000 halafu 15,000 mwaka 1978
Na mnamo mwaka 1980 bila mafanikio dau likapanda mpaka $50,000
Hapo watu zaidi walichangamkia fursa na kwenda mpaka Amazon kupambana na Anacondas ili wapate huo mchongo ambapo watu wengi walipoteza maisha kwa tamaa na bila mafanikio
Sasa sisi huku badala ya idara kusaidia watu wao ndio wanatafuta madili



Sent from my iPhone using Tapatalk

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom