Natafuta baba mlezi

Natafuta baba mlezi

ninaujauzito miez 8 mhusika kaukataa kwa madai kuwa anamchumba wake anampenda sana na hata muelewa akimwambia kama anamtoto kwani anajua hana. tena kaniambia nisimtafute kabisa na namba kabadilisha najua nimetenda dhambi na nawaza sana mtoto wangu inamaana hatakuwa na baba? binafsi sina uwezo wa kumtunza.
najua kuna watu hum wanatafuta watoto hawana kuliko kutoa mimba bora kwa atakae kuwa tayari kumtunza amchukue.
wapo watakao nishangaa kwa hili lakin kuliko kutoa mimba bora nimpe baba yoyote mwenye shida na mtoto asanten jaman

Duuuu!Dada yangu nakushauri jikaze na uvumilie tu yatakwisha na yana mwisho usichukue maamuzi magumu kiasi hicho utakuja juta!!!!

Mimi ni mjamzito kama wewe pia, toka nipate ujauzito nimepata misuko suko mingi sana kiasi kwamba siwezi hata kuielezea,na kwa bahati mbaya huyo baba kijacho yuko mkoa tofauti na mimi hivyo mateso ninayoyapata kutokana na hili tumbo nayafeel vilivyo!!!Kutokana na mateso ninayoyapata kweli nimeapa sintokuja kumgawa mwanangu kamwe maishani hata nitesekeje ntakufa na mwanangu mikononi,na pia nimeapa kutompa mtu yeyote mwanangu anilelee labda nife mana mi ndo najua mateso ninayoyapata kutokana na ujauzito huu ila navumilia mana huwa nawaza huenda hata mama yangu alipobeba ujauzito wangu aliteseka akavumilia,sasa kwa nini mimi nisivumilie?!navumilia na hapo bado sijui uchungu wa leba mana ni mwanangu wa kwanza lakini nimeshakuwa na mapenzi ya dhati na kijacho wangu na namuomba mungu anisaidie niwe na afya ili niweze kumlea mwanangu kwa mapenzi yote!!!!!!!!!!

Jipe moyo utashinda na jivunie kuwa mama kijacho na upige moyo konde mana wewe sio wa kwanza kufanyiwa hivyo,muombe mungu akufungulie milango ya riziki ili uweze kulea mwanao,jivunie kuwa mama mtarajiwa na kuwa na roho ya huruma kwa mwanao dada yangu!!!!unajuaje kama utapata mwingine baada ya huyo?fikiri kabla ya kutenda usije juta baadae!!
 
Hivi wewe mleta mada kwa akili yako unategemea utapata wa kumtupia mzigo wako??
 
pole sana.ila kwanza futa hayo mawazo ya kutafuta baba mlezi.aliyekwambia mtoto ili akue lazima alelewe na baba nani?wapo wengi wamelelewa na mama zao tu na leo hii wana maisha mazuri tu.na baba zao haohao walioqakana wanawapigia magoti kuomba msaada.nakushauri fungua uzi mwingine humuhumu jf omba msaada wa kuwezeshwa mtaji na vitu vinginevyo ili kujikimu kimaisha uweze kujifungua salama na kulea mwanao.tupo tutakaokuchangia.mtoto mtamu mno kamwe usiwaze kumgawa.
 
Kwa sisi waafrika mtoto ni muhimu sana ndio maana hatuna utamaduni wa kuadopt watoto yaani hata kama mtu ni maskini vipi lakini anataka mtoto wake amlee mwenyewe, sijajua una hali mbaya kiasi gani mpaka uone kama huna uwezo wa kumlea huyo mtoto kama una uwezo wa kuwa na access na internet mpaka kupost hii ishu kuna watu ni maskini sana huko vijijini hawajui hata internet ni kitu gani lakini huwasikii wanatafuta mtu wa kuwalelea watoto wao so nashindwa kukuelewa ni mama gani wa kiafrika anayetafuta mtu wa kumsakizia mwanae
 
We una matatizo au unadhan mtoto atakubanaa eeee
 
Lord!Even as you get closer to your due date you do not love your baby enough to want to do anything to provide for him?
 
Mpenzi hivi umewaza kwamba what if huyo mtoto utakayemzaa ndo akawa mtoto wako wa pekee? What if ukiolewa baadaye afu ukashindwa kuzaa? Utarudi kumtafuta mtoto uliyemgawa? Utamwambia nini huyo mtoto hadi akuelewe sababu ya wewe kumgawa? Unadhani mtoto atakuwa na upendo na wewe kama mama as long as amekulia mikononi mwa mama mwingine ambaye yeye anaamini ni mama yake mzazi? Chochote kibaya kikitokea kwa huyo mtoto ndani ya hiyo familia, mwanao atakulaumu milele
Please my dear, kama umeweza kulea mimba hadi muda huu, basi na mwanao utamlea tu. Mungu ni wa ajabu, atakuinulia watu wa kukusaidia hadi utashangaa. Mungu ni muaminifu, atakupigania tu. Usitupe baraka yako (mtoto wako)
 
Kwa sasa nakushauri omba msaada watu wakusaidie fedha ya kujiandaa na uzazi baada ya hapo omba msaada wa mtaji wa biashara ufanye biashara ulee mwanao. Acha kuwaza kumtoa mtoto huwezi jua Mungu anamakusudio gani kukupa hilo jariba. Huenda huo mtoto akawa mkombozi wako maishani baadaye ukiwa mzee. Acha mawazo ya starehe jikubali ishatokea anza maisha mapya.
 
ninaujauzito miez 8 mhusika kaukataa kwa madai kuwa anamchumba wake anampenda sana na hata muelewa akimwambia kama anamtoto kwani anajua hana. tena kaniambia nisimtafute kabisa na namba kabadilisha najua nimetenda dhambi na nawaza sana mtoto wangu inamaana hatakuwa na baba? binafsi sina uwezo wa kumtunza.
najua kuna watu hum wanatafuta watoto hawana kuliko kutoa mimba bora kwa atakae kuwa tayari kumtunza amchukue.
wapo watakao nishangaa kwa hili lakin kuliko kutoa mimba bora nimpe baba yoyote mwenye shida na mtoto asanten jaman
Hii ni Singham return
Aata mahji satakli....... Mala Raag Yetoye!!!!


https://www.youtube.com/watch?v=NwOEM-Y1Vqc
 
11.jpg

Kuchanganyikiwa Lazima
 
Back
Top Bottom