moudgulf
JF-Expert Member
- Jan 23, 2017
- 156,142
- 770,237
Jitahidi uwe unaipitia Katiba mkuu.Wengi wanamcheka na kumkejeli baada ya hivi karibuni kupanda na kushuka kwenye vyeo tofauti.
Mimi naona huyu anakwenda kuwa Waziri Mkuu baada ya jamii kupoteza imani na aliyepo kutokana na kusema uongo na kutoa vijembe msikitini wakati JPJM akiwa katika hali mbaya na hatimaye kuiaga dunia.
Bashiru yuko makini sana na ni mfuatiliaji sana. Mnakumbuka alivyofuatilia mali za chama ambazo watu waligeuza ni mali zao binafsi. Huyu anatufaa. Yale maneno kusema hatapokea cheo kingine ni siasa tu hata hayati JPJM aliwahi kunukuliwa kukana kuutaka urais lakini baadaye akajitosa na kuukwaa.
Msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Au nasema uongo ndugu zangu?
Kwa mujibu wa Katiba ya sasa Bashiru hawezi kuwa Waziri Mkuu, labda mpaka uchaguzi mkuu ujao upite.
