Nassari, Lema wadai kutishiwa kifo

inaonyesha jinsi gani hii nchi ina umafia sana..unaua watu kwa sababu jimbo limeangukia kwa upinzani? kwa hiyo yale majimbo ya ccm wapinzani nao waanze kuwachinja wenyeviti wa wilaya wa ccm? aisee huku tunakoelekea ni kubaya...l

America kiongozi wa chama/MBUNGE au wa nchi akitishiwa maisha FBI wanaingilia...UK viongozi wa nchi au wa vyama wakitishiwa maisha scotland yard wanachunguza..hapa bongo viongozi wa vyama wanatishiwa ilitakiwa usalama wa taifa or polisi makao makuu kuchunguza hili swala ila badala yake nasikia eti wameenda polisi huko meru kureport.....IT CAN ONLY HAPPEN IN BONGO :angry:

Huo unafanana kama mwandako wa Justine Nyali! (Just thinking aloud!}
 
Kuna namba mpya zinazoweza kutumika kwa hadi mwezi mzima bila kusajiliwa na i hope hiyo loophole iliondolewa na kama ilisajiliwa basi itakuwa rahisi kuwadaka hawa mawakili wa shetani kama polisi watataka kufanya hivyo maana na wenyewe huwa hawaeleweki sometimes....

Polisi wakitaka wanaweza!
 
Nimeshangazwa sana na vitisho hivi. Juzi mke wangu aliota ndoto kwamba mbunge mmoja wa CDM ameuwawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana lakini kutoka katika kundi fulani hivi la kisiasa. Mke wangu ndoto zake kwa 98% huwa za kweli. Nilikuwa niandike hapa ndani ili kutoa taadhari lakini nikaona inaweza isieleweke vizuri lakini kwa kuwa imetokea basi ni vema viongozi wote hasa wa CDM wakachukua taadhari kwa ulinzi. Lakini pia kwa wale wanaoweza kuomba basi ni vema wakawaombea viongozi hawa kwani kwa Mungu yote yanawezekana!

Maombi yana nguvu sana. Ebu tuliombee kwa kumaanisha. ni vizuri hata kuwashirikisha watu wengine wanaojua kuomba na kuwaonyesha jinsi jambo hili linavyoweza kuvuruga amani ya nchi. Wakiomba utasikia wauaji wamekamatwa kama kuku!
 
Hizi ni propaganda za CHADEMA tu ili waonewe huruma........ kwani wameanza kushinda majimbo mwaka huu?? mbona wabunge wao wote wapo hai??? suala la kuuawa kiongozi wa chama, hata CCM aliuliwa mwenyekiti wa wilaya kule mbeya hivi karibuni, je? CHADEMA ndio walimuua?? suala la kuuana arusha halijaanza leo

Kwa hiyo wewe unajua kinachoendelea, tuendelee kuuana kwa sababu za kisiasa. Jibu mwenyewe maswali unayouliza tukuelewe.
 
Hizi ni propaganda za CHADEMA tu ili waonewe huruma........ kwani wameanza kushinda majimbo mwaka huu?? mbona wabunge wao wote wapo hai??? suala la kuuawa kiongozi wa chama, hata CCM aliuliwa mwenyekiti wa wilaya kule mbeya hivi karibuni, je? CHADEMA ndio walimuua?? suala la kuuana arusha halijaanza leo
Watu wanapoteza uhai we unasema ni propaganda?Na taarifa kama hizo za vitisho vilianza kwa marehemu mwenyekiti wa usa river watu wakachukulia poa angalia nini kilichompata.
Du bongo ni ziadi ya afganstan.
 
Hizi ni propaganda za CHADEMA tu ili waonewe huruma........ kwani wameanza kushinda majimbo mwaka huu?? mbona wabunge wao wote wapo hai??? suala la kuuawa kiongozi wa chama, hata CCM aliuliwa mwenyekiti wa wilaya kule mbeya hivi karibuni, je? CHADEMA ndio walimuua?? suala la kuuana arusha halijaanza leo

Hapo kwenye red unajua ni kina nani walikamatwa na mpaka sasa wapo rumande Ruanda Mbeya?
 
Hatutaki umwagaji wa damu isiyokuwa na hatia, ndugu zetu Wanaarumeru kaeni pamoja ninyi ni watu wa lugha moja, kabila moja, mnaishi eneo moja kwanini mnataka kuuana mnataka kuturudisha miaka ile ya tisini?? Wakati ule ilikuwa dini leo ni siasa, ndivyo mnavyotaka?? Sikubaliani na hilo. Serikali kupitia jeshi la polisi na kampuni ya simu husika yaani Vodacom watupe majawabu ya uchunguzi haraka iwezekanavyo kuwa ni nani kahusika na vitisho ili sheria ichukue mkondo wake.
 
Haya yote yanaletwa na TCRA Kutokuwa makini mtu atasajili simu bila vitambulisho.
 
Hizi ni propaganda za CHADEMA tu ili waonewe huruma........ kwani wameanza kushinda majimbo mwaka huu?? mbona wabunge wao wote wapo hai??? suala la kuuawa kiongozi wa chama, hata CCM aliuliwa mwenyekiti wa wilaya kule mbeya hivi karibuni, je? CHADEMA ndio walimuua?? suala la kuuana arusha halijaanza leo

Siasa iachwe kwa wanasiasa ,
 
Kwani tulitegemea nini toka kwa hawa wahuni na wahalifu waliojipa kutawala na sasa wako madarakani?

- Wao wamejiapiza kutawala ni haki yao (kama vile ni haki ya kuzaliwa).
- Wao ndio wenye haki na sababu za kuendelea kufaidika na kila chema ambacho MUUMBA aliipa ardhi ya Tanganyika.
- Wao tu ndio wana haki ya kuishi
- Kwa gharama yoyote ni lazima maisha na interests zao zilindwe
- Neno "maslahi" linamaanisha ni wao na maswahiba wao (selected few) na sio kwa taifa au jamii ya watanganyika.

Ndugu zangu hii ni vita kamili, of coz haikuwahi kuwa tofauti tokea pale kwanza.
 
Hiyo ni blackmail, je Mh Nassari ameripoti polisi??

Au anaendelea ku report kwenye magazeti kwa ajili ya kujiongezea umaarufu?
 
Hizi ni propaganda za CHADEMA tu ili waonewe huruma........ kwani wameanza kushinda majimbo mwaka huu?? mbona wabunge wao wote wapo hai??? suala la kuuawa kiongozi wa chama, hata CCM aliuliwa mwenyekiti wa wilaya kule mbeya hivi karibuni, je? CHADEMA ndio walimuua?? suala la kuuana arusha halijaanza leo

Wewe hata kama huna akili huwezi kuazima kwa wenzako? Ujumbe ambao umetumwa kwa wahusika umewekwa hapo juu na tena ujembe unataja na kifo cha mwenyekiti wa CDM - Usa River, bado unasema kuwa wanataka waoenewe huruma? Dr. Mwakyembe alitishiwa hivyo hadi akafungua jalada Polisi na mwisho wa siku tulishuhudia alivyofika India. Wewe ungepokea ujumbe wa aina hiyo ungekaa kimya? Hakuna anayetetea kuwa wakiuawa CCM ni sawa wala CDM, lakini tunachotaka ni uhai wa watu ulindwe iwe wa viongozi wa CDM au CCM.

Kwamba hizi ni propaganda za CDM ni upuuzi wako. Tafadhali kila jambo lichukulie kwa uzito wake. Unavyotuandikia mawazo kama hayo humu unatutia kinyaa na unaonesha jinsi usivyojali utu wa binadamu.
 
Vyovyote vile but its better tahadhari ichukuliwe........ Na hili neno "kuchinja" mbona watanzania tunafika mbali sana. Mungu atubariki
 
Haya yote yanaletwa na TCRA Kutokuwa makini mtu atasajili simu bila vitambulisho.

Unapita mtaani unamkuta dada kashika mwamvuli anakwambia anasajili simu, unamuonesha kitambulisho ulichotengeneza kwenye kiofisi uchwara cha stationery anakusajili!
 
Hizi ni propaganda za CHADEMA tu ili waonewe huruma........ kwani wameanza kushinda majimbo mwaka huu?? mbona wabunge wao wote wapo hai??? suala la kuuawa kiongozi wa chama, hata CCM aliuliwa mwenyekiti wa wilaya kule mbeya hivi karibuni, je? CHADEMA ndio walimuua?? suala la kuuana arusha halijaanza leo

Ndugu yangu Mizizi, hebu zanisha mizizi uone haya kwa kina. Napenda nikupe mifano miwili moja ni hadithi za kale na moja ni kutoka katika kitabu kitakatifu yaani Biblia.

Naanza na hadithi, hii ilisomeka MTEGO WA PANYA KUINGIA WALIOKUWEMO NA WASIOKUWEMO. Katika hadithi hii mtu moja alikuwa amekusudia kutega panya maana walimsumbua sana nyumbani mwake, alipoutega ule mtego panya akauona kuwa ni hatari kwake lakini hakuwa na wezo wa kuutegua, mara akapita jogoo, panya akamwambia, tafadhali saidia kutegua huu mtego maana naona umekaa vibaya unaweza kuingai waliokuwemo na wasiokuwemo, jogoo akamjibu 'mimi wanihusu nini, umetegwa wewe unayeiba chakula ghalani mie napewa' akaondoka zake. Mara akapita mbuzi, panya akaomba vile vile na majibu yakawa yale yale, akaja ng'ombe akaombwa kwa kuwa wewe ni mkubwa hebu saidia kutegua hiki kitu ni hatari kwetu wote majibu yakawa yale yale. Panya akaamua kukaa mbali na mtego ule maana alijua hakuna msaada. Mara akapita nyoka juu ya mtego nao ukafyatuka na kumbana. Mwenye nyumba kwa kudhani aliyekamatwa ni panya akaenda kwenye giza akipapasa ili amtoe huyo panya labda kwa makusudi ya kuutega tena. La haula! kumbe nyoka yule akamgonga yule baba na baada ya muda mfupi akafariki na ndipo shida ilianza. Usiku huo watu wacahche walikuja kulala msibani na ili wale usiku huo jogoo alifanyika kitoweo. Kesho yake watu waliongezeka ikaonekana anayefaa kwa mboga ni mbuzi, akachinjwa na siku ya kuanua tanga watu wengi walifika ikaonekana kitoweo anayefaa ni Ng'ombe akachinjwa. Mtego wa panya ukaingia walookuwemo na wasiokuwemo. Panya akawa anaangalia yote yale na alibaki salama. Mtega panya na wapambe wote walikumbwa na kifo.

Katika BIBLIA: Nakupeleka katika Kitabu cha Esta. Hapa tuna mkuta Mfalme Ahasuero ambaye alimiliki toka Bara Hindi mpaka Kushi, juu ya majimbo mia ishirini na saba. Mfalme huyu alikuwa na Mkuu wa maakida wote aliyeitwa Hamani bin Hamedatha, Mwagagi. Mfalme Ahasuero alikuwa na mke wa kwa Kiyaudi aliyeitwa Esta. Hamani alitaka aheshimiwe sana kwa cheo chake, alipoona kuwa kuna mtu anayeitwa Modekai mjomba wake Esta hamweshimu kwa kumwinamia akafanya njama za kuliangamiza taifa la wayahudi. Mordekai alipopata taarifa hizi akamtaarifu mpwa wake Esta juu ya mambo mabaya yaliyopangwa juu yao. Esta kwa kuona kuwa yeye yumo katika nyumba ya Mfalme aliona yuko salama. Ndipo mjomba wake akamtumia ujumbe huu nanukuu kwenye Biblia
Esta: 4:13-14 Naye Mordekai akawaagiza wampelekee Esta jibu la kusema, Wewe usijudhanie kuwa wewe utaokoka nyumbani mwa mfalme, zaidi ya Wayahudi wote. Kwa maana wewe ukinyamaza kabisa wakati huu, ndipo kutakapowatokea Wayahudi msaada na wokovu kwa njia nyingine, ila wewe utaangamia pamoja na mlango wote wa baba yako; walakini ni nani ajuaye kama wewe hukuuijia ufalme kwa ajili ya wakati kama huo? (Mwisho wa kunukuu)
Ndugu yangu Esta alipata somo na kuchukua hatua na matokeo yake Hamani ndiye alitundikwa kwenye mti ulioandaliwa kwa ajili ya wengine na kuwa chakula cha ndege. Unaweza kujisomea mwenyewe sura yote ya 5 na 6 kwa ujumbe kamili.

Sasa ujumbe wangu kwako na wanaodhania kuwa wako salama ni huu

Tusifanye dharau kwa taarifa mbaya zinazolenga wengine, vinginevyo kibao kinaweza kugeuka wakaingia
waliokuwemo na wasiokuwemo. Mnadhani wanaokusudiwa ni viongozi wa CHADEMA, sawa lakini jua viongozi wa CHADEMA si viongozi wa chama ni viongozi wa watu, je watu watakubali hayo?

Hii fahamuni ni hatari sana kuliko unavyoweza kudhania, Viongozi wa CCM, Selikali na Vyombo vyake vyote vya usalama mnayonafasi ya kuzuia hili la sivyo ikitokea mjue mauaji yatakayofuata yatakuwa ya kutisha hakuna atakayebaki salama. Na hili siyo Arusha tu au Arumeru, ni kwa nchi nzima. Hebu tuzuie ufa kabla ya kafuta kujenga ukuta. Naongea hili kwa uchungu na ninawaomba CCM tusifurahie hili ni hatari kwetu kuliko mtu yeyote. Wewe angalia kwa sasa kupita mtaani na shati au Kanga ya CCM ni shida kwa kuzomewa, itakapokuwa kuchinjana tutaponea wapi?

Henyi makamanda, yaliyomkuta Hamani yanaweza kuwakuta ninyi pia, chukua tahadhali, najua kuwa ninyi mnafanya kazi kwa maelekezo ya chama sawa ila jua kuwa unaweza kufika wakati mkazikimbia kambi au mkatupa magwanda kwa hofu.

OMBI: Kila mtu kwa nafasi yake aliyopewa achukue hatua kuhakikisha kuwa haya hayatokei.
 
Hao jamaa wanachokoza Vita, Kumgusa Simba Kimuto kwa vyovyote vile ni kuiomba vita na wameru wa Sing'isi, na inajulikana wana Sing'isi walivo. Tofauti na hapo Simba anasapoti ya wameru wengi sana.

Tungoje tuone
 
hapa ndipo napoona faida ya kusajili namba ya simu. Hawa watu lazima watapatikana sababu jamaa wa voda wameshawasajili namba zao
kama wamesajili, ila kama hawajasajilije?
ingekua vizuri kua line haiuzwi kwa mteja
mpaka akubali kuisajili kwa details sahihi.
 
Ccm ndo chama kilichoshika dola,ni chama chenye serikali,kwa kuwa ni chama chenye serikali ndiyo inayo simamia idara zote za us
 
Ccm ndo chama kilichoshika dola,ni chama chenye serikali,kwa kuwa ni chama chenye serikali ndiyo inayo simamia ialama wa raia na mali zao na taifa kwa ujumla,kwa upande wa pili ndo chama ambacho kimejeruhiwa na siasa za upinzani kwa kukipoka nafasi maeneo mbalimbali.Sasa inapotokea mauaji kama hayadara zote za u.s
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom