Gsana
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 4,383
- 1,340
Mkuu, umesema watu wa kanda ya ziwa wanakosa upendo kwa ndugu zao lakini naona hoja yako imejikita sana kwa mkoa wa Kagera peke yake, ebu tuambie watu wa Mwanza, Shinyanga, Tabora, then itakuwa vizuri ukatueleza watu wa wapi wana upendo na ndugu zao na uweke vielelezo kama ulivyoweka
ndugu Dume ukisoma mada vizuri utaona pale mwisho nimeeleza kuwa bado sijagusia mwanza,mara,shinyanga na kwingineko. Ukweli ni kwamba mada mleta mada kaweka wazi kuwa kanda ya ziwa wanasahau hali ya ndugu zao. No research no right to speak,kwa iyo sijagusia musoma au mara kwa kuwa sijaizunguka nzima naongea ninachokijua,sitaki kujadili nisichojua,hata ivo apo juu mchangiaji kashauliza kuhusu mikoa kama tabora ambayo ina viongoz wa juu kama spika wa zaman lakini bado hamna cha maana,Tabora ina mchumi wa kimataifa,ndugu Prof.Haruna Lipumba,lakini safiri leo uione Tabora!utalia machozi,nenda kule Sokomatola kwa ndugu Waziri mkuu Pinda,hata taa zilizowekwa barabarani zina miezi kadhaa kwa kukosa uwezo wa kulipa bill ya umeme! Iyo inakufurahisha?achana na iyo,kuna vituo vya afya hata juz Tbc1 walionesha vifaa vya hospital vinachemshwa kwa kuni,magunzi na wengine uambiwa waende hospital na kopo moja la mkaa la kuchemsha vifaa ya upasuaji,apo Pm Pinda uenda kuhutubia akiwa ndani ya V8 ya sh.200mil. Alaf ndo mtoto wa mkulima. Masilingi alishawahi kumsema Prince Bagenda ambaye ana ofisi pale London,juzi amerudi ccm,uyu mtu kwao shamba limegeuka kichaka,nduguze wanaishi kwa kuuza miogo na viazi jumapili pale soko la Rubya,iyo ni akili,upendo au uchumi? Twende shinyanga,pale wilaya ya kishapu imedaiwa mkurugenzi kafisadi karibu mil200,yan mpaka wilayani ni vumbi ambalo hutimuka kama kuna mtu anaswaga ng'ombe,huduma za kibenk kama crdb mpaka ufanye safari ya kuja uku shinyanga. Juzi tu watu wameanza kufa kwa njaa na ukame umeshika kasi,yan ata mifugo kama ng'ombe wamekonda na wengine wanakufa. Tunaitaji nini mpaka walau hata ngombe wa shinyanga wapate kuishi ili tupate nyama,maziwa mbolea na ngozi?tutafute wazungu wawekeze au? Leo hii watu wa Zanzibar wanalipiwa na bodi ya mikopo kuanzia certificate,diploma,digrii,mpaka masters,leo hii mtoto wa mzee wa karibu na mgodi wa Barrick anajilipia mpaka cheti,wanawatega fom6,wapate div.3 wakose mkopo warudi makwao. Huu ni uuaji na usaliti kielimu. Jaman tuelewane kuwa kanda ya Ziwa inahitaji special attention imesahaulika!