Nashindwa kuzipenda filam za bongo....

wanajua kuwa hawawezi kuuza filamu zao bila kuweka maeneo mengi ya mapenzi,wanajua wabongo wengi wanavutiwa na michezo ya ngono au ifananayo.Ukifanya utafiti utaona % kubwa ya hizi picha ni wadada wanakaa nusu uchi ili kuvuta hisia za watu wanaopenda ngono na kuangalia hii pia angali makava yao.Bora nyie mnaziangalia mimi kwa zile nilizoziona basi nimeziona kwenye basi ninaposafiri,vinginevyo ni heri nimsikilize jangala na mzee mundu ila sio kucheki uchafu
 
Wa-Tanzania tunakasumba ya kudharau vya kwetu,kweli bado tuko nyuma lakini ni ukweli usio katalika kuwa hapa tulipofikia tumepiga hatua tena sana,zamani ilikuwa unatazama film za kibongo kama huna lakufanya lakini sasa hivi ukisikia kuna mpya una shauku uione,na ushahidi kuwa tumeanza kukubalika wapo watu ambao si wa-Tanzania wanazikubali na huwa wanauliza kama kuna mpya,naamini wapo walioziona picha za kina Ray,Kanumba walipokwenda Rwanda mapokezi waliyopata. wenzetu wameanza zamani wanastahili kuwepo walipo fikia...Bongo flava ilianza kwa kuonekana kama muziki wa kihuni leo Akon anamkubali AY au Ali K kufanya kazi na R kelly ni ushahidi kuwa tunakoelekea kuna matumaini..basi ipo siku hata kama sio Kanumba basi katika mtiririko wa filamu za bongo yupo mtu atakuja kututoa kimasomaso,kwani wao waweze wana nini na sisi tushindwe tuna nini.​
 
wanajua kuwa hawawezi kuuza filamu zao bila kuweka maeneo mengi ya mapenzi,wanajua wabongo wengi wanavutiwa na michezo ya ngono au ifananayo.Ukifanya utafiti utaona % kubwa ya hizi picha ni wadada wanakaa nusu uchi ili kuvuta hisia za watu wanaopenda ngono na kuangalia hii pia angali makava yao.Bora nyie mnaziangalia mimi kwa zile nilizoziona basi nimeziona kwenye basi ninaposafiri,vinginevyo ni heri nimsikilize jangala na mzee mundu ila sio kucheki uchafu
Watu wa TGNP Hili Hawalioni.? Wanajifanya kutetea Haki za WANAWAKE Lakini wanaunga mkono WANAPO JIDHALILISHA Kwa kweli hata mimi naona kichefuchefu.
 
kama ulianzaga kuangalia move za holwood toka zamani kisha uje uanze kuangalia zetu za kibongo itakuchukua muda kuzipenda.
Hii yote ni kutokana na teknologia ingawa wengi wasema stori nk, kiu kweli kasoro zipo na zinazidi kupungua siku hadi siku lakini mwisho wa siku watu wanafanisha film yenye bajeti sawa na bajeti ya tanzania na filim ya ray yenye bajeti ya 10milioni

Bajeti sio issue, kuna makosa kibao ambayo hayahitaji hata sent tano kuyarekebisha, movie zao zote zina majina ya kizungu ndani wanaongea kiswahili, na hata wakijaribu hicho kizungu ni full broken, siku nilikuwa hospitali mapokezi namsubiria ndugu yangu apate matibabu, basi pale walikuwa wameweka sinema ya kibongo, duhh kweli ilibidi nitoke nje kwa aibu, maana sinema zetu bila ngono haijawa movie, yaani huwezi kuangalia na familia nadhani mnanielewa, pale palikuwa na watoto na watu wengine walonizidi umri, actor alikuwa Ray na kanumba, wakawa wana act kama mtu na ndugu yake, sasa eti Ray akawa anatembea na demu wa baba yake, Kanumba akawa hakubaliani na hilo, sasa kilichonikera ni wahusika kutofanana na husika zao. Mijitu mikubwa eti in act kama watoto wa kishua, kingereza kibovu cha kuiga slang ambayo hawaiwezi, kwa kifupi ni upuuzi, siwakatishi tamaa ila waongoze bidii sana tu na wasilewe sifa mapema otherwise they are wasting their time.
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Wa-Tanzania tunakasumba ya kudharau vya kwetu,kweli bado tuko nyuma lakini ni ukweli usio katalika kuwa hapa tulipofikia tumepiga hatua tena sana,zamani ilikuwa unatazama film za kibongo kama huna lakufanya lakini sasa hivi ukisikia kuna mpya una shauku uione,na ushahidi kuwa tumeanza kukubalika wapo watu ambao si wa-Tanzania wanazikubali na huwa wanauliza kama kuna mpya,naamini wapo walioziona picha za kina Ray,Kanumba walipokwenda Rwanda mapokezi waliyopata. wenzetu wameanza zamani wanastahili kuwepo walipo fikia...Bongo flava ilianza kwa kuonekana kama muziki wa kihuni leo Akon anamkubali AY au Ali K kufanya kazi na R kelly ni ushahidi kuwa tunakoelekea kuna matumaini..basi ipo siku hata kama sio Kanumba basi katika mtiririko wa filamu za bongo yupo mtu atakuja kututoa kimasomaso,kwani wao waweze wana nini na sisi tushindwe tuna nini.​

Hatulazimiki kupenda upuuzi kwa kuhofia kuonekana hatupendi vya kwetu, tunayasema haya ili warekebishe makosa, kuoendwa rwanda sio uthibitisho kuwa sinema zetu zina viwango, wengi wanataka kuona utupu wa hao mademu tu.
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Hatulazimiki kupenda upuuzi kwa kuhofia kuonekana hatupendi vya kwetu, tunayasema haya ili warekebishe makosa, kuoendwa rwanda sio uthibitisho kuwa sinema zetu zina viwango, wengi wanataka kuona utupu wa hao mademu tu.
Ipo namna ya kumkosoa mtu ili afanye vizuri hilo halikataliki, na mpenda maendeleo siku zote yuko tayari kukosolewa na ndio maana kuna baadhi ya maofisi mahoteli na kwa wenzetu wa mbele mpaka mabasi yana kisanduku kama una maoni au malalamiko ya huduma unatoa mchango wako,ukitazama kwa makini utaona wengi ukosoaji wao wanaashiria kuwa hawawezi na wala hawatoweza,ni kweli hatulazimiki kupenda upuuzi kwa namna yeyote ile,na juu ya hayo huo utupu ninao uelewa mimi kwa kiswahili changu kibovu haupo ktk hizi filamu,na isitoshe nimetaja Rwanda km mfano wapo watu wako mbele na sio wabongo wanathamini filamu zetu.walipo sipo walipoanzia huu ni uthibitisho kuwa wanapiga hatua mbele.
 
Naona mzuka kwa watu unaongezeka

kuhusu hizi filam za bongo.....kwenye media na watu..

Sasa mimi najiuliza.kwa nini nashindwa kuzipenda hizi
filam za bongo????

Yaani nashindwa hata kutazama dakika ishirini tu ya filam hizi...
Nikiangalia naona kichefuchefu mwishowe naishia kutapika,heri Kingwendulile,Mtanga,Asenga na Mzee majuto mara alfu moja,hao wengine kazi kupiga kelele kama wapiga debe kwenye vituo vya daladala ,ovyoooo
 
Ipo namna ya kumkosoa mtu ili afanye vizuri hilo halikataliki, na mpenda maendeleo siku zote yuko tayari kukosolewa na ndio maana kuna baadhi ya maofisi mahoteli na kwa wenzetu wa mbele mpaka mabasi yana kisanduku kama una maoni au malalamiko ya huduma unatoa mchango wako,ukitazama kwa makini utaona wengi ukosoaji wao wanaashiria kuwa hawawezi na wala hawatoweza,ni kweli hatulazimiki kupenda upuuzi kwa namna yeyote ile,na juu ya hayo huo utupu ninao uelewa mimi kwa kiswahili changu kibovu haupo ktk hizi filamu,na isitoshe nimetaja Rwanda km mfano wapo watu wako mbele na sio wabongo wanathamini filamu zetu.walipo sipo walipoanzia huu ni uthibitisho kuwa wanapiga hatua mbele.

Nimekuelewa mkuu, hata hivyo mdogomdogo tutafika tu.
 
Mi mtanisamehe kwakwel hata mimi zinaniboa.mi ni mzalendo na ninapenda asili yangu ila kwenye ukweli pasemwe. Yani kwani wale wanaofungua geti kwy muvi za kibongo lazima wa-act kama machiz.?
Mtu akiact anshangaa basi ataruka juu ka kan'gatwa na nge na macho katoa SOO fake wakat ktk hali ya kawaida mtu hawez kushangaa hivyo
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Mimi siamini kwamba movie za mapenzi pekee ndizo rahisi, mbona kuna visa vingi kwenye vitabu ambavyo vinasisimua sana na vinaweza kuigizwa?? tatizo ni wangapi wana muda wa kuvisoma kuvielewa na kuvitengenezea sinema? angalia movie moja ya Ki Nigeria inaitwa SUICIDE MISION, hakuna cha vita wala nini lakini story na mkasa mzima unasisimua na kuhuzunisha sana!! Ki ukweli mimi huwa nawasikia tu wasanii akina Kanumba lakini ukiniambia movie zao sijui hata moja kwani huwa siziangalii kabisaaaa!!

Wakuu ni nani na mwenye sifa zipi ndio anapaswa kuigiza move? nakubali tatizo lipo lakini hizi lawama zingine hazina ukweli wowote.
Nina mdogo wangu wa kike walikuja kuniomba fund ya kuproduce move, nikaomba kwanza nione story script kwanza, ilikuwa ya mapenzi, nikauliza kulikoni mapenzi tu, niliambiwa na wataalamu kuwa wanatamani kuacti mambo mengine lakini kamera, teknolojia, bajeti, utaalamu na mtu wa kufinance na ategemee rejesho la pesa yake ndio utata unapokuwa.
Kwa mazingira ya kamera zilizopo, wataalamu wa it, bajeti ningumu kutengeneza move za action, vita nk
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Mi pia sizipendi kwa sababu
1. scenes zinachukua muda mrefu sana, zingine hazina connection na story yenyewe.
mfano wanaweza kuonesha mtu anatoka ndani ya nyumba, anamsalimia mfanya kazi, anamuuliza habari za nyumbani, anapanda gari, anafunguliwa geti, anatoka getini reverse, anabadili gia, anaeda forward,
anatembeza gari, wanaonesha sehem mbali mbali za dar, anafika aliko kua anaenda, anapiga honi, anafunguliwa geti, anamuuliza askari kama mama yupo, anapewa jibu, anapaki gari,
anapiga hodi, anafunguliwa, wanaulizana habari, anakaribishwa, anakaribishwa tena, anapewa kiti, anaulizwa atakunywa nini, anajibu, analetewa kinywaji etc...
Hii yote inaonesha wanataka kuongeza scenes ili wauze part one, part two na part three for the budget ya movie moja. Kuna rafiki yangu hua anazipiga editing, alafu ndio analeta tuangalie. movie tatu zinatosha in 120 min.
2. Story nyingi ni za kijinga. mapenzi, uchawi, roho mbaya ya watu fulani etc. hakuna entertainment yoyote!
3. wanatumia soundtrack visivyo. yaani unakuta wanapiga "my heart will go on" wakati huo hu wanaonesha mtu kawehuka anatembea hovyo barabarani... sasa vinahusiana vipi? hawawezi kupiga instrumentals? au wapige za kiafrica basi...Hovyoooo
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Mi mtanisamehe kwakwel hata mimi zinaniboa.mi ni mzalendo na ninapenda asili yangu ila kwenye ukweli pasemwe. Yani kwani wale wanaofungua geti kwy muvi za kibongo lazima wa-act kama machiz.?
Mtu akiact anshangaa basi ataruka juu ka kan'gatwa na nge na macho katoa SOO fake wakat ktk hali ya kawaida mtu hawez kushangaa hivyo

Hili ni tatizo kubwa sana. Naliona hata katika filamu za Nigeria japo nashangaa kuna wadau wanazisifia kweli. Wabongo na Wa-Nigeria wana(tuna) tabia ya ku-act extremes: mtu akilia basi ni kulia kupindukia, tukitaka kuonesha mama ananyanyasa mtoto wa kambo basi mama huyo atakuwa shetani! Ila watazamaji wengi wa sinema hizi wanadhani uigizaji wa namna hii ni sahihi. Ukimkosoa Ramsey Noah utarushiwa mayai viza na utaulizwa movie yako iko wapi. Aisee, safari bado ni ndefu sana.
 
Mimi siamini kwamba movie za mapenzi pekee ndizo rahisi, mbona kuna visa vingi kwenye vitabu ambavyo vinasisimua sana na vinaweza kuigizwa?? tatizo ni wangapi wana muda wa kuvisoma kuvielewa na kuvitengenezea sinema? angalia movie moja ya Ki Nigeria inaitwa SUICIDE MISION, hakuna cha vita wala nini lakini story na mkasa mzima unasisimua na kuhuzunisha sana!! Ki ukweli mimi huwa nawasikia tu wasanii akina Kanumba lakini ukiniambia movie zao sijui hata moja kwani huwa siziangalii kabisaaaa!!

Nakumbuka filamu hii ya SUICIDE MISSION, ni ya Richard Moffe kama sijakosea. Nimepata kutazama sinema yake nyingine ya THE PRICE. Zilikuwa nzuri. Tatizo Wa-Nigeria wakaanza kuigiza mambo yale yale, ikawa ni uchawii tuu kila filamu, ni makanisa tuuu kila filamu. Kuna sinema inaitwa KAJOLA, wao wanisema kuwa ni filamu ya kwanza ya CGI (Computer Generated Imagery) / CG (Computer Graphics) ya kwanza nchini kwao. Lilikuwa jaribio zuri japo nadhani kimauzo ilifanya vibaya kwa sababu kuna technicalities kadhaa ziliwasumbua. Walijaribu.
 
Na hizo wanazosema script mi sidhan kama huwa wanaziheshim. Huwa naangalia behind the scene/making the movie za hollywood wenzetu kama kwy script muhusika anatakiwa kusema "...the elephant was huge" atasema maneno hivo hivo na sio kubadilisha "the elephant was big" sentens zina maana moja lakin director anamake sure script hazichakachuliw coz mkifanya hivo muhusika hatawakilishwa ilivotakiwa
 
Mi pia sizipendi kwa sababu
1. scenes zinachukua muda mrefu sana, zingine hazina connection na story yenyewe.
mfano wanaweza kuonesha mtu anatoka ndani ya nyumba, anamsalimia mfanya kazi, anamuuliza habari za nyumbani, anapanda gari, anafunguliwa geti, anatoka getini reverse, anabadili gia, anaeda forward,
anatembeza gari, wanaonesha sehem mbali mbali za dar, anafika aliko kua anaenda, anapiga honi, anafunguliwa geti, anamuuliza askari kama mama yupo, anapewa jibu, anapaki gari,
anapiga hodi, anafunguliwa, wanaulizana habari, anakaribishwa, anakaribishwa tena, anapewa kiti, anaulizwa atakunywa nini, anajibu, analetewa kinywaji etc...
Hii yote inaonesha wanataka kuongeza scenes ili wauze part one, part two na part three for the budget ya movie moja. Kuna rafiki yangu hua anazipiga editing, alafu ndio analeta tuangalie. movie tatu zinatosha in 120 min.
2. Story nyingi ni za kijinga. mapenzi, uchawi, roho mbaya ya watu fulani etc. hakuna entertainment yoyote!
3. wanatumia soundtrack visivyo. yaani unakuta wanapiga "my heart will go on" wakati huo hu wanaonesha mtu kawehuka anatembea hovyo barabarani... sasa vinahusiana vipi? hawawezi kupiga instrumentals? au wapige za kiafrica basi...Hovyoooo

Mkuu umenifanya nicheke sana ulivyoeleza jinsi wanavyo refusha muda,
Hii ni kweli mkuu lakini mimi bado naamini kabisa kama mtu ulikuwa muangaliaji mzuri wa film za hollwood kwakweli itakuchukua muda kujua kuwa akina ray na kanumba wanajaribu walau kuikuza hii industry katika mazingira magumu ikiwemo kutokubalika kwa kazi zao na watu kama sisi tuliokuwa addicted na movies za hollwood,
Kamera na ujuzi wa kiteknolojia nalo ni tatizo lingine, kamera wanazotumia ni za matumizi ya nyumbani na hamna utundu wowote wa kucheza na teknolojia kwa kutumia kamera hizo,
Wataalamu waliosomea nalo ni tatizo ingawa baada ya kazi zao kuanza kukubalika kidogo na kupata visenti naona wapo walioenda kozi inagawa fupi south afrika na ndio maana kwa sasa kiukweli movies zetu zipo sawa kiwango na za wanajeria.
Scrip writer na story writer hapa ndipo pana mtihani,|na tatizo hili hata wanaijeria wanalo, bado hakuna magwiji kwa maana ya kusomea hii kitu ili ifanyike kwenye mtiririko wako.
Mazowea au mapokeo: hili nalo ni tatizo kudhani kuwa nafasi fulani ni za watu wa aina fulani tu,thia wrong kwamba mlinzi gatini lazima awe komedian mtanga, bambo,masanja nk. Katika kipindi cha bongo movie Ant ezekiel anahojiwa anasema mimi ukinipa nafasi ya house girl sichezi haina hadhi yangu, huu ni ulimbukeni wa kutokujua tu kuwa muhusika mkuu anaweza kuwa house girl au mchimba choo au hata muhudumu mochwari.
Pamoja na mapungufu hayo bado tunajitahidi sana na kwa nchi za east afrika ikiwemo kongo zambia,malawi nadhani sisi bado tupo juu kwenye hii tasnia ya film kuliko wenzetu.
Tunapokuwa tunazihukumu hizi film zetu hebu tuzi hukumu kwa mazingira ya kibongo bongo na si kuzi fananisha na movies za avatar na lord of the ring zilizotumia taknolojia ambayo hatuna ndoto ya kuifikia leo wala kesho
Tuwaungeni mkono kwa nunua kazi zao na mapato yao ndio yataboresha kazi zao kwa kutumia watu compitent zaidi
 
Mkuu umenifanya nicheke sana ulivyoeleza jinsi wanavyo refusha muda,Hii ni kweli mkuu lakini mimi bado naamini kabisa kama mtu ulikuwa muangaliaji mzuri wa film za hollwood kwakweli itakuchukua muda kujua kuwa akina ray na kanumba wanajaribu walau kuikuza hii industry katika mazingira magumu ikiwemo kutokubalika kwa kazi zao na watu kama sisi tuliokuwa addicted na movies za hollwood,Kamera na ujuzi wa kiteknolojia nalo ni tatizo lingine, kamera wanazotumia ni za matumizi ya nyumbani na hamna utundu wowote wa kucheza na teknolojia kwa kutumia kamera hizo,Wataalamu waliosomea nalo ni tatizo ingawa baada ya kazi zao kuanza kukubalika kidogo na kupata visenti naona wapo walioenda kozi inagawa fupi south afrika na ndio maana kwa sasa kiukweli movies zetu zipo sawa kiwango na za wanajeria.Scrip writer na story writer hapa ndipo pana mtihani,|na tatizo hili hata wanaijeria wanalo, bado hakuna magwiji kwa maana ya kusomea hii kitu ili ifanyike kwenye mtiririko wako.Mazowea au mapokeo: hili nalo ni tatizo kudhani kuwa nafasi fulani ni za watu wa aina fulani tu,thia wrong kwamba mlinzi gatini lazima awe komedian mtanga, bambo,masanja nk. Katika kipindi cha bongo movie Ant ezekiel anahojiwa anasema mimi ukinipa nafasi ya house girl sichezi haina hadhi yangu, huu ni ulimbukeni wa kutokujua tu kuwa muhusika mkuu anaweza kuwa house girl au mchimba choo au hata muhudumu mochwari.Pamoja na mapungufu hayo bado tunajitahidi sana na kwa nchi za east afrika ikiwemo kongo zambia,malawi nadhani sisi bado tupo juu kwenye hii tasnia ya film kuliko wenzetu.Tunapokuwa tunazihukumu hizi film zetu hebu tuzi hukumu kwa mazingira ya kibongo bongo na si kuzi fananisha na movies za avatar na lord of the ring zilizotumia taknolojia ambayo hatuna ndoto ya kuifikia leo wala keshoTuwaungeni mkono kwa nunua kazi zao na mapato yao ndio yataboresha kazi zao kwa kutumia watu compitent zaidi
Kaka yangu, mi nimezichambua kufatana na mazingira, audience na kadhalika.Sijasema tunataka Lord of the ring sababu audience haita penda hizo. Lazima zikae zime fanana na mazingira yetu. Hapo sibishi. Ila critics nimetoa ni za kawaida sana, ni vitu vidogo ambavyo vinatufanya kushindwa kui-promote hii industry ya nyumbani kwa kweli. Umesema tumewafikia wanaijeria, Hivi ndio lengo kweli? mbona wanaijeria wenyewe ni grimaces after grimaces? movies zao hovyo vile vile!Ona Mali, Senegal, South Africa, nchi za kiarabu... ona hata sa latin america (zile za kina maria clara, na marimar sijui). Ingawa script zinaweza kuonekana kua za kijinga, angalau unaelewa kua kuna editing ya nguvu inafanyika ili kumfurahisha atakae angalia picha. kama hupendi ni we mwenyewe tu. Ila hizi za nyumbani hatujui kama ni romance, action, comedy au ni kitu gani hasa!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom