Nashindwa kuelewa mtazamo wangu

Nashindwa kuelewa mtazamo wangu

Amos David Mathias

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2022
Posts
1,575
Reaction score
3,109
Mimi ni mwanachama niliyeingia juzi Kati Jamii Forums lakini baada ya kuingia huku nimekuwa nikisoma Uzi nyingi za mapenzi, nyingi zinalenga kuonesha wanawake walivyo wabaya Kwa wanaume.

Kila mtu anaekomenti kuhusu tukio la mwanamke anatoa comment iliyojitesheleza kuonesha wanawake walivyo na tabia Mbaya, hawafai, namna ambavyo wanawanyanyasa wanaume na kero zao.

Sasa na Mimi naona nimeanza kuwachukia na kuwadharau wanawake.Hii roho ya kuchukia wanawake inakuwa Sana kadri navyoingia jukwaa la mapenzi na siwaoni kama Tena marafiki Bali maadui . Nyinyi mnaonaje ndugu kaka na Dada zangu.Nipo peke yangu au tupo wengi.Mtazamo wangu Kwa wanawake umebadilika vibaya Sana.
 
Ewe ndugu Amos David Mathias , maisha ya humu achana nayo, usisikilize ama kuweka maanani Kila kinachozungumzwa humu ndani, humu ni ulimwengu wa kipekee sana, wote tuna magari na majumba ya kifahari, tunakula Bata na kutafuna kuku Kila uchwao, viwanja vya starehe ni Kila siku usisahau mavacation yetu ni Dubai, alafu na passport zetu zishachafuka Safari za mamtoni ukija kushangaa kapuku unajikuta mwenyewe tu 🤣🤣
 
Bila shaka huyu mleta mada atakuwa ni mgeni JF.
Kumbe kuna watu huwa hawajiongezi kwenye kutafakari

Yaani vile wanaume humu wanajitanabaisha kuwa maplayer na wazee wa michepuko ndo tuwachukulie hivyo waume zetu nyumbani?

Mmh Kama unasombwa na mafuriko ya social media pole sana
Ni suala la muda atajifunza "to take things easy "
 
Upo sahihi mkuu. Tatizo linakuja, wanaume walio kwenye mahusiano wengi wanapost mabaya ya wapenzi wao, walio kwenye ndoa pia wanapost, the same na kwa wanawake wanafanya ivo ivo.

Ila haina maana wanawake ni wabaya kihivyo. Unajua ni wanaume wangapi wanatendewa mazuri na wanawake ila hujawahi sikia wakisema. Kwahiyo sio wote. Still kuna materials nje uko.

Ratio ni kama kati ya wanawake 10, mizigo ni wawili hadi watatu hivi, the rest wako poa.
 
Mimi ni mwanachama niliyeingia juzi Kati Jamii Forums lakini baada ya kuingia huku nimekuwa nikisoma Uzi nyingi za mapenzi, nyingi zinalenga kuonesha wanawake walivyo wabaya Kwa wanaume.

Kila mtu anaekomenti kuhusu tukio la mwanamke anatoa comment iliyojitesheleza kuonesha wanawake walivyo na tabia Mbaya, hawafai, namna ambavyo wanawanyanyasa wanaume na kero zao.

Sasa na Mimi naona nimeanza kuwachukia na kuwadharau wanawake.Hii roho ya kuchukia wanawake inakuwa Sana kadri navyoingia jukwaa la mapenzi na siwaoni kama Tena marafiki Bali maadui . Nyinyi mnaonaje ndugu kaka na Dada zangu.Nipo peke yangu au tupo wengi.Mtazamo wangu Kwa wanawake umebadilika vibaya Sana.
Social media sio sehem sahihi kwako mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom