Nashauri watoto waache ishu ya kusalimia watu wazima kwa kuwashika kichwani

Red Giant

JF-Expert Member
Mar 9, 2012
15,658
20,889
Wakuu baada ya kula ugali, nyanya chungu, bamia, dagaa, kabichi, maharage, nyama roast na kushushia pepsi big nimepata wazo.

Hili suala la mtoto kumshika mtu mzima wakati wa kusalimia naona kama halijakaa sawa. Naona kama linamjengea mtoto tabia ya kutojiamini, uoga na kumshusha thamani.

Pia ni usumbufu mtu kuanza kuinama usalimiwe.

Nasikia wenzetu wamasai huwa mkubwa ndiyo anasalimia kwa kumshika mdogo kichwani, hii kidogo imekaa poa. Hata baraka hutolewa kwa kushikwa kichwani sasa inakuwaje mtu mzima kupewa baraka na mdogo badala ya mkubwa ndiyo kumpa mdogo baraka?

Napendekeza tusalimiane na watoto kwa kushikana mikono au kwa kuwashika kichwani kama wanavyofanya wamasai. Au nakosea ndugu zangu?
 
Shikamoo ni salamu imeundwa kitumwa zaidi. Mimi watoto wangu hunisalimia bila kunishika kichwani, lkn kwa ujumla tu salamu ya shikamoo sipendi. Natamani mtu aseme tu "amani" nami nijibu "amani".
 
Kila watu wana utamaduni wao.Huwezi lazimisha utamaduni unaotaka wewe.Kuna nchi flani kumsalimia kiongozi mkubwa hata kama wewe ni mwanaume unachuchumaa mfano Malawi.Hata hapa kwetu mfano unapokuwa kwenye mkutano na raisi akikuambia simama unasimama nakuuliza jambo flani hadi akuambie kaa chini kisha unainama kama unamsujudia hizo ni taratibu za watu tu.Kumbuka hata YESU na utukufu wake aliosha watu miguu siku ya pasaka.Acha la kusalimia mfano hili la kuitana majina mfano wewe ni mtu mzima majina yako matatu ni Juma Pesambili Mramba.Hilo jina la tatu ni surname la ukoo mtu ambaye hana rika na wewe hawezi kukuita Mr Juma atakuita Mramba.Wanaoweza kukuita kwa jina la kwanza ni uliosoma nao na watu wa rika lako.Tuchukulie mfano mhe raisi mstaafu Mrisho Jakaya Kikwete ukimu address huwezi kumuita Bwana Mrisho unakuwa umemkosea heshima utasema Kikwete.Hata JPM alikuwa anaitwa Magufuli huwezi kumuambia John.Huu ni utaratibu wetu watanzania.
Kwa wazungu raisi wa Marekani walikuwa wana mu adress kwa jina la Barack.Ni vigumu kubadili utamaduni usiouzoea
 
Back
Top Bottom