Nashangaa wabongo wanaowashobokea wayahudi

Nashangaa wabongo wanaowashobokea wayahudi

Status
Not open for further replies.
Genesis 27:29 haizungumzii Mkristo,Muislam,au dini yeyote
 
Idadi kubwa ya wanaunga mkono Israel wanaamini Israel ni taifa la kikristo
kumbe Israel Ukristo hautambuliwi

Wengine wanaamini Yesu alikuwa Mzungu....au Wayahudi ni wazungu
basi tu ili mradi watu na imani zao

Mbona hushangai Muhamad kuwa Mwarabu.Maana kuna mtu nilibishana naye anasema maandishi kwenye Quran sio ya kiarabu,bali ni lugha kutoka mbinguni.Watu wanasema kanzu sunna,ukiuliza kisa mtume alivaa.Kumbe waarabu walivaa kanzu kabla hata ya huyo mtume.Kila mtu amini anachoamini kuingilia imani za watu sio sawa.Unavyowashangaa wao kuwakubali wayahudi,nawe wanakushangaa kuwapapatukia waarabu.





Mbona hushangai Muahamad kuwa Mwarabu.Acheni
Idadi kubwa ya wanaunga mkono Israel wanaamini Israel ni taifa la kikristo
kumbe Israel Ukristo hautambuliwi

Wengine wanaamini Yesu alikuwa Mzungu....au Wayahudi ni wazungu

basi tu ili mradi watu na imani zao
 
Genesis 27:29
May nations serve you and peoples bow down to you. Be lord over your brothers, and may the sons of your mother bow down to you. May those who curse you be cursed and those who bless you be blessed."
 
Mbona hushangai Muhamad kuwa Mwarabu.Maana kuna mtu nilibishana naye anasema maandishi kwenye Quran sio ya kiarabu,bali ni lugha kutoka mbinguni.Watu wanasema kanzu sunna,ukiuliza kisa mtume alivaa.Kumbe waarabu walivaa kanzu kabla hata ya huyo mtume.Kila mtu amini anachoamini kuingilia imani za watu sio sawa.Unavyowashangaa wao kuwakubali wayahudi,nawe wanakushangaa kuwapapatukia waarabu.





Mbona hushangai Muahamad kuwa Mwarabu.Acheni


Waarabu na wayahudi ni mtu na binamu yake
 
Tatizo kubwa ni ujinga. Wangeelewa uyahudi ni nini wasingefanya hivyo. Tatizo unakuta kiongozi wa dini nae mjinga. Inasikitisha.
 
Idadi kubwa ya wanaunga mkono Israel wanaamini Israel ni taifa la kikristo
kumbe Israel Ukristo hautambuliwi

Wengine wanaamini Yesu alikuwa Mzungu....au Wayahudi ni wazungu

basi tu ili mradi watu na imani zao

Taratibu Naanza Kukujua Na Kujiandaa Kuingiwa Hofu Na Wewe.
 
Mtoa mada unachanganya mambo.
Kweli wapo wakristo wasiojielewa vizuri wenye kushabikia kila wanachofanya wayahudi. huu ni utumwa wa kidini.

kuhusu ubaguzi, kila mwanadamu ni mbaguzi, wahindi wanabaguana kwa kiwango cha juu, kuna wengine hata mtu masikini akigusa chombo chake kinatupwa ili wasiambukizwe umasikini, makaburu sina cha kusema, waarabu saudi arabia wamewachapa sana watu weusi juzi tu, marekani mzungu kamnyanyasa na kumbagua mweusi sana, huku wenyewe tunabaguana sana tu.

kikubwa:
wayahudi wanauwezo mkubwa, most elite race sio kwa sababu tu wamependelewa bali wanajituma sana na wanaishi katika mazingira magumu.
walitoka ulaya wakakuta parestina ni jangwa leo jangwa ni mahala safi.
walikuta katikati kuna mbu hatari kutokana na madimbwi walichonga mitalo kwa mikono leo hakuna mbu.
wanamiliki mabenk makubwa ulimwenguni. wakisema wachukue pesa sao zote dunia inasimama.


tukiacha wivu, kama ni ubaguzi hata wewe kuna watu unawabagua, hiyo hulka ya kibinafsi ni hulka ya binadamu wote.

hawa jamaa sio watu wakuwadhalau ila ni kuwachukulia kama somo la maisha.
 
Taratibu Naanza Kukujua Na Kujiandaa Kuingiwa Hofu Na Wewe.

Hahaa usiingie na hofu ukiona kitu naandika pointless unakipinga kwa pointi
mimi nina rafiki anaamini Israel iko Europe kijiografia..
nazungumza my experience...
 
Mleta mada kama ni mkristo acha kuabudu mungu wa wayahudi abudu miungu ya kiafrika aka mizimu. Tabu yetu waafrika tunaabudu miungu ya kabila zingine ndio maana hatuendelei tunalumbana tu.
 
Genesis 27:29
May nations serve you and peoples bow down to you. Be lord over your brothers, and may the sons of your mother bow down to you. May those who curse you be cursed and those who bless you be blessed."
this was written by some Jewish clown
 
Hahaa usiingie na hofu ukiona kitu naandika pointless unakipinga kwa pointi
mimi nina rafiki anaamini Israel iko Europe kijiografia..
nazungumza my experience...

Sijui Umekumbwa Na Nini Kwani Siku Hizi " Unatokota " Sana Tena KUNAKOTUKUKA.
 
Yakobo(Israel) na Essau ni watoto wa Isaka pia Kumbuka Isaka na Ismael ni watoto wa Ibrahim. Yakobo alioa kwao Alani(Iran) ambapo pia baba yake Isaka alioa,huku Essau alioa kwa baba yake mkubwa Ismael so hawa wote ni ndugu na niwaarabu kwa asili sema tu labda genetic differences kama Mhindi wa India na Bangladesh etc au Wahindi wekundu
 
Huko Israel kuna madhehebu ya kikristo mfano roman.hats kipindi cha yesu ubaguzi wa wafuasi wa yesu ulikuwepo kwa hiyo kuna waisrael ambao ni wakristo na wasio wakristo.
 
1. Issue sio uyahudi wao bali ni Ukristo wetu kwa maana ya kutii maandiko ya Biblia.

2. Mji wa Yerusalemu katika Israeli ni mji pendwa wa Mungu & umeshaharibiwa mara nyingi na kujengwa tena. Mungu ameahidi kupigana na mataifa yatakayotaka kuuharibu tena.

"Tena itakuwa siku hiyo, nitafanya Yerusalemu kuwa jiwe la kuwalemea watu wa kabila zote; wote watakaojitwika jiwe hilo watapata jeraha nyingi; na mataifa yote ya dunia watakusanyika pamoja juu yake. Hata itakuwa siku hiyo, ya kwamba nitatafuta kuwaangamiza mataifa yote watakaokuja kupigana na Yerusalemu." - Zekaria 12:3,9

3. Mungu anasema hao wayahudi ipo siku atawapa Roho ya utambuzi na Wataamini kupitia Yesu Kristo. That day is just near, kuna kitu anakiplot Mungu (Asomaye na afahamu).

"Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi, na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba; nao watamtazama yeye ambaye walimchoma; nao watamwombolezea, kama vile mtu amwombolezeavyo mwanawe wa pekee; nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa ajili ya mzaliwa wake wa kwanza." - Zekaria 12:10

4. Israeli na mji wake pendwa Yerusalemu umechaguliwa na Mungu kuwa lango la baraka na Udhihirisho wa Mungu kwa mataifa mengine. Ukiwa nao utabarikiwa & kinyume chake ni laana.

"Tena itakuwa, ya kwamba mtu awaye yote wa jamaa zote zilizomo duniani, asiyekwea kwenda Yerusalemu ili kumwabudu Mfalme, Bwana wa majeshi, mvua haitanyesha kwao." - Zekaria 14:17

Nina mengi ya kuelezea, ngoja niishie hapa kwa sasa. Next time nitakuja kuwaeleza "KWA NINI NI MUHIMU KUIOMBEA AMANI ISRAELI/YERUSALEMU" kama ilivyoamriwa kwenye MAANDIKO.
 
Biblia inasema Essau alikuwa mwekundu na vinyweleo vingi kama mwarabu ingawa ni pacha wa mdogo wake Yakobo
 
Tofautisha dini na imani,dini ina misingi yake,imani ina misingi yake.Dini ya Uzayuni na Ukristo wana misingi ya kiimani inayofanana mwanzo mwisho.Hivyo huwezi kutenganisha ukristo na uzayuni labda katika matumizi ya bible.Ukristo umegawanyika katika madhehebu na mbalimbali ila yenye misingi inayotofautia mfano waroma na wapentekoste bible wanazotumia zatofautiana kidogo.Dini ya uzayuni bible wanayotumia haitofautiana na ya wapentakosta,waanglikana na kkkt ila Waroma bible yao ni tofauti na hao wote.
Hakika hujui chochote kuhusu judaism, pole sana, the jews dont believe kuwa yesu ni true mesiah, hawaamini kuwa ni mwana wa Mungu either, hawaamini utatu wala hawatumii bible unayoijua wewe. Tafuta njia ya kweli usibebwe na mihemko, njoo Europe ushuhudie hali ya ukristo huku, mzigo wa ukristo mmeachiwa kusini mwa jangwa la sahara
 
Kwa mtazamo wangu huu mgogoro ni wa Kifamilia Isaka na Ishimael kisha Yakobo na Essau wote kesi kuu HAKI ya UZALIWA wa kwanza
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom