Narudia mara kumi Nyerere sio Mungu

Narudia mara kumi Nyerere sio Mungu

Hauleweki hata hoja zako. Tanganyika mipaka yake inajulikana wazi, sema kuificha Tanganyika ndani ya Tanzania, pili,Ujamaa na KUJITEGEMEA kasome vizuri Azimio la Arusha hasa sura ya PILI Na TATU ukielewa njoo useme wapi alikosea. Tatu,mazingira yale baada ya kupata Uhuru unajua tulikuwaje Tanganyika? Na kwa nini alifanya hivyo. Mwisho naomba kichwa cha habari ubadilishe maana hata yeye alikiri kufanya makosa na akasema chukueni mazuri na mjifunze.

Mazuri kwa kubwabwaja tu, si onesha hayo mazuri.
 
Ukweli ukweli mtupu mleta uzi umeona mbali!!
 
Kosa lingine alitunyima elimu,na kuleta siasa ambazo hazina kichwa wala mguu wa ujamaa na kujitemea ambayo hakika ndiyo imewafanya watanganyika kuwa mazezeta mpaka leo watu hatujui hii nchi inafuta mfumo gani wa ujamaa au ubepari halafu kuuwa mpaha wa tanganyika hakika inanichoma sana na kuua pia jina la tanganyika hakika mimi binasfi sio kiongozi ninayemmind
 
huwezi kumchukia nyerere bila kuwa na moja ya hivi vitu.

1. uwe na matatizo ya akili.
2. uwe unalipwa.
3. uwe muislamu.
 
Ujamaa na Kujitegemea halikuwa kosa hata kidogo. Ni ujamaa huo uliojenga misingi ya Utaifa na Umoja wetu.
 
Ni kweli ulijenga misingi ya kitaifa lkn hata china wenyewe ambao walikuwa ni wajamaa sana walikuja kungundua wakati mwingine lazima wafungue mipaka na baada ya kufungua mipaka walifanyiwa sana, tatizo letu tanzania tulichelewa kufungua mipaka, na mwalimu aliliona hilo pia na hilo lilikua ni tatizo kubwa sana kiuchumi.Lengo la nyerere alikuwa baya lilikuwa zuri na moja ya malengo yake ni kusomeaha kwanza watu wake lkn pamoja na hayo bado wamemwangusha sana, ni afadhali angefungua mipaka mapema akiwepo angalao angetupeleka mbali
 
Tulikuwa na viwanda vingi sana kutokana na juhudi za huyu mzee ,hivyo viwanda ukivitafuta leo havipo ima waliofuatia waliviuza/walivibinafsisha na sasa vimegeuzwa magodown na vingine vimekuwa mstu na tulipofikia kwa sasa kama taifa hata njiti za kutolea uchafu katika vinywa vyetu tunaagiza kutoka nje.Tusimhukumu kwa sababu za kijinga kama hizi za mtoa mada ,apumzike kwa amani ndugu Jullius Kambarage Nyerere
 
Baba wa taifa Mwalimu Julias Kambarage Nyerere ni shujaa wa kukumbukwa daima, amefanya mambo mengi mazuri kwenye taifa lake la Tanzania.

Alikuwa mzalendo wa kweli, mpenda haki, alichukia rusha wazi wazi tena si kwa kuimba tu la asha alifanya kwa matendo lakini baba wa taifa hakuwa Mungu, hakuwa malaika na hajawa mtakatifu bado kwa hiyo alikosea kama mwanadamu.

Na alikiri wazi wazi bila kificho, japo alifanya mengi mazuri kimsingi na yanahitaji kupongezwa lakini alikosea vile vile na kosa kubwa alilofanya kubwa kabisa ni kuuwa mipaka ya Tanganyika, kosa la pili ujamaa na kujitegemea na kosa la tatu ni mfumo wa chama kimoja.

Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.
Tumekusikia. Ila kujitegemea halijawahi kuwa kosa katika dunia huru. Waulize Wamarekani.
 
Kosa lingine alitunyima elimu,na kuleta siasa ambazo hazina kichwa wala mguu wa ujamaa na kujitemea ambayo hakika ndiyo imewafanya watanganyika kuwa mazezeta mpaka leo watu hatujui hii nchi inafuta mfumo gani wa ujamaa au ubepari halafu kuuwa mpaha wa tanganyika hakika inanichoma sana na kuua pia jina la tanganyika hakika mimi binasfi sio kiongozi ninayemmind
Umekosa elimu wewe? Lazima umesoma enzi za Mwinyi.
 
Back
Top Bottom