Napoteza Rafiki yangu jamani nisaidie

Napoteza Rafiki yangu jamani nisaidie

Sina pa kwenda

Senior Member
Joined
Nov 18, 2010
Posts
113
Reaction score
15
Habari zenu wanajamvini, majuzi nilitoa hela Tigo pesa 500,000 nkampa huyo rafiki yangu azihesabu coz nilikuwa nadrive zen achukue mkopo anaotaka maana aliniambia hana hela anataka nimkope, kwenye gari kulikuwa na dada mwingine sasa wakati yule shost anahesabu hela akanipa laki mbili yeye akachukua laki tatu sasa ikafika muda wa malipo nkambwambia unajua nakudai laki tatu akasema no nilichukua laki mbili nkwambia tumuulize yule dada mwinigne ambae alikuwepo akasema alinipa mie laki mbili na yeye kuchukua tatu,

Basi nkasema nimeingia hasara laki kwa urafiki ni issue ndogo sana nkapotezea sasa jana mchana nkawa nampigia simu as you friends coz tulizoea kusalimiana nkakutana simu haipatikani sasa jioni tulipoona nkamuuliza vipi mbona nimekupiga mchana sijakupata akaniambia nimekublock kozi unaleta njaa zako na kunisingizia kama ulikuwa unataka kunikopa si ungesema kuliko kunisingizia umenipa laki tatu daaah nilijisikia vibaya sikujibu kitu kbs! Hivi jaman mtu kama huyu unamfanyaje? Mie nkajisemea kimoyomoyo Mungu kama nimekosea mie show me ila kama ni yeye amuonyeshe coz siwez kupoteza urafiki coz of 100,000/= maana siku nyingine huwa tunapeana hela tunanunuliana vitu! Yaan kakasirika as if kweli nimemsingizia
 
Uvumilivu katika kila jambo ni jambo la lazima sana katika mahusiano yoyote.

Thamani ya mtu haiwezi kulinganishwa na pesa au ujinga anaokufanyia, msamehe msonge mbele
 
hata kwenye bible imeandikwa na ukikopesha usifikiri kurudishiwa tenda wema nenda zakoooo
 
Huyo ana lake jambo! Angekuwa mumeo au mkeo ungemkalisha chini akasema yake moyoni,ila rafiki achana naye!
 
Kwanza Pole kwa kupotelewa na pesa.Nakushauri umfuate physically na kuomba msamaha au tumia mtu wa karibu aongee naye myamalize.Mwambie samahani hata kama yeye ndio amekukosea.pia kumbuka makosa ni sehemu ya maisha ndio maana hata sisi wanadamu tukikosa kwa God anatusamehe na kusahau kabisa.
 
Habari zenu wanajamvini, majuzi nilitoa hela Tigo pesa 500,000 nkampa huyo rafiki yangu azihesabu coz nilikuwa nadrive zen achukue mkopo anaotaka maana aliniambia hana hela anataka nimkope, kwenye gari kulikuwa na dada mwingine sasa wakati yule shost anahesabu hela akanipa laki mbili yeye akachukua laki tatu sasa ikafika muda wa malipo nkambwambia unajua nakudai laki tatu akasema no nilichukua laki mbili nkwambia tumuulize yule dada mwinigne ambae alikuwepo akasema alinipa mie laki mbili na yeye kuchukua tatu,

Basi nkasema nimeingia hasara laki kwa urafiki ni issue ndogo sana nkapotezea sasa jana mchana nkawa nampigia simu as you friends coz tulizoea kusalimiana nkakutana simu haipatikani sasa jioni tulipoona nkamuuliza vipi mbona nimekupiga mchana sijakupata akaniambia nimekublock kozi unaleta njaa zako na kunisingizia kama ulikuwa unataka kunikopa si ungesema kuliko kunisingizia umenipa laki tatu daaah nilijisikia vibaya sikujibu kitu kbs! Hivi jaman mtu kama huyu unamfanyaje? Mie nkajisemea kimoyomoyo Mungu kama nimekosea mie show me ila kama ni yeye amuonyeshe coz siwez kupoteza urafiki coz of 100,000/= maana siku nyingine huwa tunapeana hela tunanunuliana vitu! Yaan kakasirika as if kweli nimemsingizia

Hivi bado kuna urafikiwa hivi hadi leo!na mi mamluki yote hii!!!!!???urafiki wa kutiana hasara kwangu noo!
 
Yani bado huoni kama huyo sio rafiki unabaki kusema hutaki kupoteza urafiki? Kama hujui kusoma hata picha pia huelewi?
 
achana nae,ni njaa zinamsumbua ndo maana anakosa ubinadamu kwa kiasi hicho,any way lkn malipo hapahapa duniani.
 
Ana stress huyo,, usimdai wala usimtafute,,potezea atakutafuta mwenyewe stress ikiisha
 
Aisee usilazimishe urafiki achana naye,leo kwa vile unamdai anajifanya anakuja juu,mkisahau akipata tatizo tena utaona anaanza kukubembeleza umkopeshe,achana na naye urafiki hauna maana sometimes,kuliko rafiki heri hata ambaye si rafiki yako akusaidie maana marafiki wanaleta sana ujuaji.
 
Marafiki huwa hawanuniani marafiki hupeana makavu live kisha life linasonga na urafiki unaendelea.

Sasa urafiki wake kwako una manufaa gani kama ana tabia ya udhulumati?
 
Kwakweli nimepoteza hela nyingi kwa kukopesha marafiki now days nikiamua kumpa nampa lakin usijiwekee mia kurudishiwa
 
ana miaka mingapi huyo rafiki yako? marafiki kama hao wazuri wakususie mke kwa hasira,
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom