Antonio de Guzman
JF-Expert Member
- Jun 20, 2016
- 7,942
- 15,707
Vumilia tu maana kama ni mume muda ukifika atatokea tu.1.Inategemea na umri maana anaweza kuwa mdogo sana na yenyewe hiyo ni ishu nyingine.
2.niko mwanza
3.mpendwa wangu niombe nini kingine.
Ha ha haa anamuomna Mungu hafu anajificha ndani bila shaka tusingelima kama ni rahisi ki hivyo anahitaji watu pmUmri wako bado mdogo dadangu, na mahitaji yako makubwa sana.
Unapoomba kwa Mungu usitegemee mwanaume atashuka kutoka mbinguni.
Jiweke katika mazingira ya kutongozeka, usinune nune kua na tabasamu muda wote na ujitahidi ku-socialize...
Kama umeamua kuomba, omba kwa bidii Mungu wetu (hata kwetu mashetani) ni mwaminifu na atakupatia hitaji la moyo wako. Usipate hofu 'mwanangu' utashinda kwani wakati wako bado hujawadia.
Sarah, mke wa Ibrahim alikuja kupata mtoto hata baada ya menopause kupita. Wewe ni nani hadi ukate tamaa mapema hivi.
Btw, hata mimi nipo mkoa uliopo. Nafikiri tunaweza kuonana kwa ushauri zaidi.
Wako mtiifu
- Satan -
-gracias-
NitakuPM nisijemwaga mchele kwenye kuku wengi [emoji6] [emoji6]Aisee, tatizo lako unazunguka sana, hicho kipindi kigumu ndo kipi icho?
Sent using Jamii Forums mobile app
Ndugu yangu ingekuwa ni kuhama roman ningeshahama siku nyingi sana enzi natafuta kazi maana nilikaa 4years bila kazi. Na mimi kusoma biblia ni jambo ambalo ninafanya toka zamani kwani angalau huwa inanitia moyo pale ninapokuwa nimeshidwa kabisa. Nashukuru pia.Dad yangu biblia ni kitabu kigumu sana sio cha kutafsiri kirahisi kwa kusoma mstari mmoja au miwili.
Mimi nakushauri futa kabisa mawazo ya kuhama kanisa Katoliki kisa kuolewa. Pia jaribu kuwasiliana na chama cha kitume cha Karismatiki Katoliki katika parokia unayosali lazima kipo ili wakusaidie na kukuongoza katika kumuomba Mungu katika jambo hili.
Kuna mtu ka comment eti wazee wa PM wapo kazini.Nimecheka kama mazuri.Hii post hii post!!
Haha kwa hao wenzako mbona hata wazo la watoto kwao halipo anaeweza kuishi kama hao mbona shida hana hongela sana kwa kuishi kupitia wenzakoNi huku bongo tu wenzetu walioendelea hawawazi umri najua unasema kwetu wanawake but it doesn't care ka unaji stress kisa umri you won't enjoy this life
Sent using Jamii Forums mobile app
[emoji23] [emoji23] [emoji23]NitakuPM nisijemwaga mchele kwenye kuku wengi [emoji6] [emoji6]
Unastahili kuchekwa mana sijui unamatatizo gani wewe hadi ukose marafiki chuo hadi kazini amboa wangekuelewa msimamo wako pole sana[emoji28][emoji28][emoji28] ila munachekesha saa ingine eti.
Ngoja kwanza tumalize hili la mleta uzi ndio tutaanza mashauri ya tatizo langu[emoji12][emoji23] [emoji23] [emoji23]
Ngoja nisubirie hiyo PM inayotarajiwa kutumwa mwakani mwezi kama huu.
Sent using Jamii Forums mobile app
Asante ndugu kwa moyo wako.Hapana Dada.ujue syo we tu. Mimi mwenyewe ninapokuwa natazamia kufikia hatua flani huwa nakuwa mvumilivu mpaka nachoka naamua kufanya maamuzi tofauti siku ambayo naenda kufanya hayo maamuzi mapya lile lengo la zaman ndpo linakuja .hapo ndpo ninapoaamini kuwa mungu huwa hawahi wala hachelewi ila hufika wakat mwafaka.wakati ule mwanadamu anapokata tamaa. Amini hauko mbali kulifikia lengo lako .Kama namuona shemeji(mmeo) ni mtu Bora na sahihi na ana endana na wewe, ana vokupenda sasa hadi wivu.
Sent using Jamii Forums mobile app
Nani alikwambia mme hatafutwi? Unajua ni wanawake wangapi wameolewa kwa jitihada zao? 35yrs ndo kikomo cha kubeba mimba kama hajawahi kuzaa so yupo ukingoni kama pesa anazo anaweza kujitolea mahari akaolewa na mwanaume suruali ila kama mkwanja hana anaweza olewa na mwanaume wa kawaida tu wapo wengi mtaani ikifika wkend abebe beseni la matunda atembee mitaa yenye vijana wengi huku akiwauzia matunda ya kila aina atatongozwa mpaka ashangae na Hao hohehahe ndo waoaji wenye pesa wanakula ujana tuUjue hyo 32 alivopanic atazoa had visivozoeleka kuna Dada namfahamu kashahangaika kote huko kila mahali hapati, sasa ndo asifurahie maisha, ifikr mahali Watanzania hasa wanawake wenzangu lazima maisha yaendelee, walioko huko ndani kwenye wa naishi kwenye mateso mume hatafutwi huja mwenyewe baada ya kuona vtu vitakavompendeza
Sent using Jamii Forums mobile app
Unanifaa sana tatizo huwa siamin sana wanawake wa mitandao niko sirius wala sitanii na namshunuru mungu nimejenga nina kazi nzuri tuu ila sijahamia na mimi kinachoniumiza kichwa ni kama wewe ninapata wapi mwanamke wa kuishi nae nikijiangalia nilivyojibana hadi nilipofika kimaendelea nafika mahali naogopa hata kuoa maana kila siku rafiki zangu wananikatisha tamaa eti diku nikioa tuu narudi nyuma upya hicho ndo kinachonisumbua je?ni yupi nitaempata ambae atakuwa kama mimiHabari za jumapili wana jamii.
Mimi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 32 kwa sasa. Napitia katika changamoto kubwa sana.
Hapo mwanzo kipindi ninasoma niliona si vyema kujiingiza katika mahusiano ya kufanya mapenzi kwani niliona yatanivuruga na ningejikuta napitia katika mahusiano mengi kitu ambacho sijawahi kukipanga maishani.
Nikamaliza chuo vizuri namshukuru Mungu.katika kutafuta ilikuwa ngumu kidogo nilitafuta mpaka nikakata tamaa nikaomba Mungu mpaka nikaona inatosha. Katikati ya kukata tamaa nikamuomba Mungu basi anipe kitu kimoja kwanza mme au kazi. Ila la kazi ndio nililoliwekea msisitizo kwani kwa kipindi hicho familia yangu ilikuwa inapitia changamoto nyingi kwa hiyo nikaona kazi itanisaidia kupunguza changamoto ama la basi niolewe ili nipunguze mzigo kwa familia yangu.
Siku isiyotarajiwa nikaitwa interview na nikapata kazi nzuri ambayo sikuwahi hata kufikiria wala kuiwaza.
Nikashukuru Mungu na kuanza maisha mapya ya kazi na kusaidia familia yangu. Nikajikita kwenye kumuomba Mungu anijalie mme mwema atakayenifaa na kuongoza familia tutakayoipata katika misingi ya imani ta dini ya kikristo. Sikubagua kabila wala atakuwa mkirsto wa aina gani maadamu awe anaabudu jumapili maana mimi nilikuwa tiari kuhama katoliki ili tulee familia yetu tukiwa na muongozo wa dini moja.
Sikuwahi kudhani nitafikia huku maana mpaka sasa imekuwa ngumu kama ni Mungu hachelewi ama hawahi basi kwangu mimi kwa sasa imekuwa ni shida kubwa. Nimefunga novena nimesali sana mpaka naona nimeanza kuathilika nahili swala. Mwaka jana tarehe moja nikaona basi kama mme wangu hayupo nipate tu mwanamme nitakae zaa nae lakini awe mkirsto maana siko tiari kumtenga baba na mtoto wake hata kama hamhudumii, nikiamini kuwa uwezo wa kulea mwenyewe ninao hata kama watoto watakuwa zaidi ya mmoja niko tiari kupambana na maisha. Nikaona kwa sababu nitakuwa pekeangu nikaanza kuwekeza ili watoto wangu wanikute nimejiandaa. Na penyewe Mungu akaona wakati wangu bado.
Mwaka huu mwezi wa pili akatokea mme wa mtu kitu ambacho sijawahi hata fikiria kuwa kunasiku nitaangukia huko, Mwanzoni nilitaka tuzungumze mapema kabla hatujazoena sana matakwa yangu lakini akawa mtu wa kuona nampangia sheria mapema na kudai hizo mipango ninazotaka kupanga nae tukiwa hatujafika mbali ni mipango gani. Nikaona isiwe tabu.
Ikafika siku ya kukutana nikamwambia mimi sijawahi kabisa hakuamini na nikamwambia kama anajiamini aendelee ila ajue atakuwa na deni la kulipa, akatafakari akaona viatu ni vikubwa akaondoka.
Chenga zikaongezeka nikajiuliza ni nini shida, tukapanga tukutane ili tuone hatima ni nini kati yetu. Akaja na kudai yeye hayuko tiari kutoa bikira ya mtu asiye na mpango nae. nikamuelewa na nikaona yuko sahihi.Nikamuuliza wewe ulivyoanza ulitegemea mimi ni mti sina hisia za kufanya mapenzi akadai alijua anajihusisha na mapenzi ya kila mtu ana mtu wake hivyo wanakutana kulizishana tu. Akaniambia nahitaji nini hasa kwake nikamwambia kama ulishaona hisia zangu unadhani nahitaji nini? Niliona nisianze kutaja shida niliyonayo kwanza nimsikilize yeye ndio na mimi niseme ya kwangu. Yeye akadai aliona ni mahusiano ya kula na kuondoka. Akaniambia kama niko tiari ataweka sheria za kutuongoza za maandishi ili baadae tusijekupeana shida. Nikamwambia sheria zako utazoniwekea nitazifuata vilivyo japo najijua ninawivu lakini wewe ni mme wa mtu tiari nitavumilia. Akaja na sheria na mipango mingi sana asee.sheria nyingi nilivyotafakari nikaona nyingi zinamlenga mtoto ambaye mimi ndio ninayemhitaji zaidi. na yeye akaona labda ni mmoja tu wakati mimi nishajipangia wakunitosha kabisa. Kwa maelezo yake nikaona hayuko tiari kuwa na mtoto nje ya familia na nikitokea kumpata basi nitoe mimba ama atamchukua. Nilichoka viungo vyote. Akaniuliza unalolote nikamwambia nizungumze nini wakati sheria zimekuwa ngumu.
Haki ya Mungu yaani natamani siku zirudi nyuma nizunguke na wanaume kama wafanyavyo wengine. Hukukujitunza kwangu kunanifanya nilie kila siku na kuomba Mungu usiku kucha kisa nilimtunzia mtu bikira. Jamii inayonizunguka itanitia wazimu maana swali la unaolewa lini limenichosha kabisa. Basi kama siolewi hata mtoto tu ni shida kumpata.
Kwasasa ninashida na mtoto kuliko maelezo na niendako nadhani nitawehuka. Msaada wenu tafadhalini sana.
NB. Hapo mwanzo nilifunga novena kwa muda wa mwaka mmoja na kuomba na kukabidhi mwili wangu uwe kwa ajili ya mtu mmoja tu ambaye ndio atakayekuwa mme au baba wa watoto wangu. Ndio maana inaniwia vigumu kuingia mahusiano mbalimbali.
jf inakufungulia duniaNaam kiongozi..
Upogo? hem ngoja niongeze moto ntarudi njia ingineNaam kiongozi..
Pole sana dada usikate tamaa kabisa endelea kusaliSasa hivi naona kama umri unaenda sana hivyo nahofia kukosa mtoto kabisa. Tatizo kubwa nililonalo ninapenda sana watoto na kwa sasa namhitaji kuliko ninavyoweza zungumza.
Umepotea sana kiongozi hata # hazipo kwa hewaUpogo? hem ngoja niongeze moto ntarudi njia ingine