Tatizo ni sheria zetu sio Lema.
ni haki yangu kisheria pia, kwani DOWANS inatokana na malipo ya mara moja au ni kama hivi milioni 80 x wabunge tulionao wanalipwa haya malipo ya kijinga + vigogo serikalinimzee kama kweli unauchungu na hii nchi huna haja ya kupiga kelele kwa ajili ya milioni 80,kwanza ni haki yake kisheria,pili ni vijisenti uki compare na mabilioni yanayoibiwa kila siku na serikali ya ccm,kuna mafisadi hapo kwenye serikali wanaiba mabilioni waziwazi,sasa mzee hebu anza na hao wezi ukimaliza rudi kwa lema
CTRL + Q to Enable/Disable GoPhoto.it
Vikwazo,
Swali lako liko too subjective na ndio maana hypothesis yako imefinyangwa kwenye personalization vs ruling hence rhetorics.
You could rephrased your argument and get an awful lot better responses worthy of your intentions.
E.g. kuna kanuni nyingi za bunge za kuendesha vikao na kamati za bunge zilizopitwa lna wakati na ambazo zinalitia hasara kila uchao. Je nini kifanyike?............
Nakubaliana na wewe 50%
sina tatizo na Lema kulipwa mshahara wake, hiyo ni haki yake ya msingi kabisa, Tatizo langu ni lema kulipwa posho (jimbo, mafuta etc etc) hizo sio haki zake na msingi, ni pesa inayotakiwa kwendana na shughuli ambayo kwa kipindi hiyo ilisimama, ni hakika kwamba Lema alizuiwa na mahakama kundelea kama mbunge wa Arusha na kwa misingi hiyo haya ghalama za mafuta na uendeshaji wa jimbo ( posho ya jimbo) ili koma, hiyo sio pesa ya Lema au mbunge yeyote kujikimu kwa
kisheria
mahakama inapo kurudisha kwenye kazi yako uwe mbunge au mfanyakazi mwingine
ni kuwa ulistahili kuwepo kazini kwa muda wote uliokuwa nje
kwa hio lazima alipwe stahiki zake zote na fidia juu
hiyo ni sheria na ni lazima alipwe
soma sheria ya ajira na mahusiano kazini
soma pia hukumu ya lema.
labda cha kuhoji hapa ni mafao makubwa wanayopewa wabunge
bila kukatwa kodi na fedha hizo hazionekanai majimboni
Hapa cha kuhoji ni hiyi posho yote, nashindwa kuelewa tunakwama wapi hizo posho ziko wazi yaani POSHO YA MAFUTA, POSHO YA JIMBO,
sasa tunashinda kuelewa nini kwamba hiyo ni hela ya mafuta anapokuwa ofisini? akuwa ofisini kwa miezi minane tunapa mafuta ya miezi minane iliyopita? usahihi huko wapi? au inakuwa sahihi kwa sababu ni sheria zilizosimamiwa na ccm hivyo tunufaike tu, sasa swali ZAMA ya UFISADI ni ipi?
sio kila kitu tulaumu CCM
Tanzania ni mwanachama wa World Trade Organization
na ni signatory wa ILO
kwa hivo sheria zetu tumecopy kwao na ndivo hivo ilivo worldwide
Ubunge ni kazi kama kazi zingine na haki ya mtu inapokiukwa na baadae kutenguliwa na mahakama anahesabika hana hatia
sheria yetu ya kazi ni best law we have,wananchi walipewa muda wa kutoa maoni yao
ndio bunge likairidhia
sijaona ni kipi cha kuilaumu CCM hapa
na ukisema unapinga malipo ya lema pekee basi upinge na malipo yote wanayolipwa wafanyakazi wanaorudishwa makazini baada ya madai yao kuidhiniswa na mabaraza ya kazi.
jaribu kutafuta hukumu za mahakama kuu ya kazi utajiridhisha zaidi
kwa lema haina tofauti sana kwani anastahili kupewa kila kilicho chake na bunge
Si vibaya kuangalia kiwango cha posho ya mafuta pia kulinganisha na uhalisia maana kwanza hawafiki majimboni hawa jamaa alafu hizo 2.5m zinatumikaje kwa wale ambao kukanyaga jimboni mpaka kuwe na ujio wa rais au kiongozi wa juu. In this case ndio maana mdau akahoji kuhusu hii sheria which means amejaribu kufungua macho wana jamvi kuliangalia hili kwa jicho lingine mwisho wa siku kila mtu atapiga kelele kulingana na mtazamo wake maana hata mie haingii akilini mshahara wa mbunge ni 2.5 alafu posho anazopata ni mara 3 ya mshahara (kwanini tusiseme tu mshahara wa mbunge ni 7million (ili TRA wapitie chao maana hizi posho huwa sidhani kama zinakatiwa kodi hivyo ni vyema tu mshahara ungekuwa juu kuliko kutudangaya eti mshahara ni huo alafu posho kibao) alafu posho zake ni 3 million. Au kuna haja gani mbunge akapewa fedha za jimbo, kama anapewa anafanyaje retirement ili kuonyesha namna ya zilivyotumika.
Mara nyingi kanuni zinatungwa pale ambapo kuna dosari kulingana na hali halisi ya maisha ya jamii flani, hivyo hata hili lililotokea kwa Lema ni kwamba kanuni zilikuwa kimya, mie naona hapa kama ni mabadiliko kuwe kuna auditng ya matumizi ya haya mafuta in this case automatically kama litatokea kama la Lema itaonekana hakuna haja ya kuchukua hiyo posho ila kwa kuwa hao waliokuwepo walichukua posho kama vile inavyochukuliwa posho ya nyumba ambayo mtumishi anapewa bila kuambiwa alete viambatanisho basi sheria inamruhusu Lema kuchukua hizo posho.
Kwa hiyo kamanda yuko HAPPY na sheria za magamba kwa kuwa mnufaika au? sasa ukamanda hapo utakuwa wa jambo gani? bado ni ukanda wa ukombozi?:violin::iamwithstupid::boink:Wewe ni kiazi kwelikweli hivi hao CCM ndio wamekutuma uposti hapa huo utumbo wa kuku??, hiyo ni halali ya Kamanda Lema kulipwa hizo stahili zake zote na hii ni kwa mujibu wa sheria za nchi hii inayoongozwa na magamba a.k.a CCM,naamini na wewe ni mwanachama wa CCM hivyo basi hizo ndizo sheria zinazopitishwa na serikali ya CCM kwa kura nyingi za ndiyo hapo mjengoni na wabunge wako wa CCM wanazipenda kweli kweli, hivi unajifanya kipofu au kiziwi kuwa hujui jinsi wabunge wako wa CCM walivyopitisha sheria ya Takrima?,EPA?,Richmond,na kadhalika. Ama kweli wewe ni kiazi kwelikweli kama sio kauzu.:music::A S 12::bange:
Kwa malipo ya DOWANS hayakupigwa? mbona tunatumia ugongo wa samaki? haya malipo yamepingwa kila kona, na kesi zipo mahakamani, so Lema ni aina nyingine ya dowans? if so ndio maana napinga
Ungepinga malipo ya mafao ya Lowasa kama waziri mstaafu au waziri aliyefukuzwa kwa ufisadi!
aiseeeee babayangu nikulize swali moja dowans inalipwa au hailipyi
Tusichangeanye argument ya ubunge wa lema kuwa kwenye hold kwa makosa ya mahakama, hapa tunatakiwa kupambana na mahakama kwa kufanya huo uzembe,Mkuu Vikwazo, I support your idea japo haitsadia sana Lema kukataa pesa hiyo. Sheria na mfumo wa kutunga sheria na watunga sheria ndo wametufikisha ktk hoja kama hizi. Lema nivyema alipwe pesa hiyo na ikiwezekana zaidi hiyo. Nasema hivyo kwa sababu zifuatazo:
1) Kimsingi hakukuwa na sababu za ubunge wa Lema kuwa on hold for so long. Na waliochelewesha kesi ya Lema kwa mda huo walidhani wanamkomoa Lema kumbe sivyo.
2) Lema aliteseka kisaikolojia, kuna watoto wengi yatima alikuwa akisomesha....bado hizo pesa anazigitaji kufanya hivyo.
Sidhani kama chama kilichoko madarakani na chenye wabunge ambao wametunga sheria nyingi za kunufaisha watawala wataweza kubadilisha mfumo kama unavyopendekeza. Mkuu kama kweli unauchungu wa kubadilisha mfumo huu ni sasa.