Ndio hapo kwenye argument mkuu
VIKWAZO..je hiyo 5m inatakiwa kutumika na kila mbunge kila mwezi jimboni kwake??je kuna uwezekano wa mbunge kuilimbikiza kwa miezi 12 ikafikia milioni 60 na kuenda basi kufanya hayo maendeleo jimboni??..
Je hii 2.5 million ya mafuta...haya ni mafuta ya kwenda wapi hasa??je ni safari za mbunge kutoka nyumbani kwenda bungeni tu kila siku??je ni mafuta yanayotumika pia kwenye safari za kibunge jimboni??.,..je anaweza kuyalimbikiza na kuyatumia wakati autakao hapo baadaye?vipi asipoyatumia kabisa?tumfanyeje?...hakika ninayo idadi kubwa sana ya wabunge ambao huwa wanafika majimboni baada ya miaka mitano..
na pia katika kazi zetu za kawaida zisizo za kibunge,..wakati mfanyakazi akiwa na mkataba wenye kipengele kinachoruhusu kulipwa masurufu ya mafuta,,mwezi atakaokuwa likizo huwa anastahili kuendelea kulipwa hayo masurufu?..
baada ya kujadili haya nadhani ni vema mjadala wetu ukawa mpana zaidi..unaohusu stahiki wastani za wabunge..je tuweke utaratibu gani wa malipo ili kama taifa tusiingie tu hasara hasa pale wabunge wanapoonekana dhahiri kutotekeleza majukumu yao stahiki??...mfano wa wale waliopata ubunge na kwenda kuishi marekani.....