Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,346
- 26,138
Mimi si Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba. Lakini,kama mtanzania wa kawaida sana,nina haki za kutoa maoni juu ya jambo lolote lihusulo nchi yetu. Na leo,natumia haki yangu hii iliyopo chini ya Ibara ya 18 ya Katiba ya sasa kupinga kimaoni kuhusu Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba kupiga kura wakiwa nje ya nchi. Ninazo sababu mbalimbali za kupinga kimaoni suala hili.
Mosi, utaratibu wa kupiga kura kwa namna hiyo haukuwahi kuwepo na wala haupo hapa nchini mwetu. Kuanzia Katiba, Sheria za Bunge na hata Sheria Ndogondogo,hakuna suala kama hilo. Kwakuwa Bunge Maalum la Katiba linasimamiwa na Katiba ya sasa, Sheria ya Bunge Sura ya 83/2011 na Kanuni zake, sivyema kuleta jambo jipya lisilotambulika hata na Katiba ya sasa.BL halina upekee wowote wa kishera na kimantiki.
Pili, Bunge Maalum la Katiba lisilazimishe akidi. Kama Wajumbe hawapo basi.Waliopo wapige kura. Hakuna haja kuwatafuta popote walipo ili tu kukamilisha akidi ya wapiga kura na ya wakupitisha Rasimu. Hakuna cha kuwahi wala kuchelewa. Katiba ni yetu wenyewe. Twende taratibu.
Tatu, wananchi watataka kuona na kusoma nyuso za Wajumbe siku ya kupiga kura. Kupigia 'kifichoni' hakutaleta picha nzuri. Napinga suala hilo.
Nne, kura za walio nje zina utata huu au ule. Mjumbe aweza kushawishiwa na alipo au aliye naye huko na kupiga kura kutokana na ushawishi huo. Pia,itakwa ngumu kujua wangapi wamepiga na wamepigia upande gani. Napinga suala hili.
Kimsingi, kura za Wajumbe watakaokuwa nje ya nchi zisiruhusiwe. Kwanini ziruhusiwe sasa tu?
Mosi, utaratibu wa kupiga kura kwa namna hiyo haukuwahi kuwepo na wala haupo hapa nchini mwetu. Kuanzia Katiba, Sheria za Bunge na hata Sheria Ndogondogo,hakuna suala kama hilo. Kwakuwa Bunge Maalum la Katiba linasimamiwa na Katiba ya sasa, Sheria ya Bunge Sura ya 83/2011 na Kanuni zake, sivyema kuleta jambo jipya lisilotambulika hata na Katiba ya sasa.BL halina upekee wowote wa kishera na kimantiki.
Pili, Bunge Maalum la Katiba lisilazimishe akidi. Kama Wajumbe hawapo basi.Waliopo wapige kura. Hakuna haja kuwatafuta popote walipo ili tu kukamilisha akidi ya wapiga kura na ya wakupitisha Rasimu. Hakuna cha kuwahi wala kuchelewa. Katiba ni yetu wenyewe. Twende taratibu.
Tatu, wananchi watataka kuona na kusoma nyuso za Wajumbe siku ya kupiga kura. Kupigia 'kifichoni' hakutaleta picha nzuri. Napinga suala hilo.
Nne, kura za walio nje zina utata huu au ule. Mjumbe aweza kushawishiwa na alipo au aliye naye huko na kupiga kura kutokana na ushawishi huo. Pia,itakwa ngumu kujua wangapi wamepiga na wamepigia upande gani. Napinga suala hili.
Kimsingi, kura za Wajumbe watakaokuwa nje ya nchi zisiruhusiwe. Kwanini ziruhusiwe sasa tu?