Napinga kura za nje ya nchi

Napinga kura za nje ya nchi

Kwani walitakiwa wawe wapi kama sio bungeni?! Hawapo, hawezi kufanya shughuli ya bungeni. Period! Mnataka kuchanya na kura za mtaa wa Lumumba?

Nadhani kura ya marehemu aliyefariki jana pia mtaitaka, maana hii sasa upuuzi kwenda mbele.

Mkuu Petro, kutokuwepo utaratibu fulani nchini hakumaanishi kuwa utaratibu kama huo haufai. Ni sisi ndio tunaotunga sheria/kanuni na taratibu zenu na kama hivyo ndivyo tunaweza kurekebisha na kuboresha kukidhi matakwa na mahitaji.

Mwenyekiti 6 yupo sahihi kabisa, hatuwezi kukwamsha zoezi ambalo kimsingi limefikia ukingoni.

Pia, kwa wale waliotoka nje ya bunge kwa kupinga kama ndugu zako Ukawa, kanuni hii mpya haitawalazimisha kupiga kura.

Jamani waacheni wabunge wengi popote pale walipo washiriki katka zoezi hili la kihistoria.

Katiba itapatikana
Vifungu vitapitishwa
Na wananchi watapiga kura ya ndio

Mtake ni hivyo, msitake ni hivyo.
 
Kama akidi haitoshi tufanyeje na tumeshakula posho kiasi hiki? Tukisema kuwa imeshindikana si ndo watz watatuua kabisa? Tutachakachuaje kuwa 2/3 ya Zanzbar imepatikana bila mbinu hii ya maruhani kupiga kura? Afadhali tuchakachue kanuni ili tusepe kiulaini!! Kwa mtindo huu hata ukawa watasingiziwa kuwa wamepiga kura! Uhuni mtupu!!!!!!!!
 
Nchi imeharibiwa na tuliowaamini.

Wanafiki utawawajua tuu.

Mara sijui wanaodai uraia pacha wanataka kuja kuiharibu nchi.

Sasa hao unaowaamini ambao unadai wameharibu nchi wana uraia pacha?
 
Kama wewe sio mjumbe kanuni hazikuhusu.... Ni vyema usubiri wakati wako wa kura ya maoni kisha utaamua mwenyewe kupiga ukiwa jimboni au hauko jimboni.
 
Mimi si Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba. Lakini,kama mtanzania wa kawaida sana,nina haki za kutoa maoni juu ya jambo lolote lihusulo nchi yetu. Na leo,natumia haki yangu hii iliyopo chini ya Ibara ya 18 ya Katiba ya sasa kupinga kimaoni kuhusu Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba kupiga kura wakiwa nje ya nchi. Ninazo sababu mbalimbali za kupinga kimaoni suala hili.

Mosi, utaratibu wa kupiga kura kwa namna hiyo haukuwahi kuwepo na wala haupo hapa nchini mwetu. Kuanzia Katiba, Sheria za Bunge na hata Sheria Ndogondogo,hakuna suala kama hilo. Kwakuwa Bunge Maalum la Katiba linasimamiwa na Katiba ya sasa, Sheria ya Bunge Sura ya 83/2011 na Kanuni zake, sivyema kuleta jambo jipya lisilotambulika hata na Katiba ya sasa.BL halina upekee wowote wa kishera na kimantiki.

Pili, Bunge Maalum la Katiba lisilazimishe akidi. Kama Wajumbe hawapo basi.Waliopo wapige kura. Hakuna haja kuwatafuta popote walipo ili tu kukamilisha akidi ya wapiga kura na ya wakupitisha Rasimu. Hakuna cha kuwahi wala kuchelewa. Katiba ni yetu wenyewe. Twende taratibu.

Tatu, wananchi watataka kuona na kusoma nyuso za Wajumbe siku ya kupiga kura. Kupigia 'kifichoni' hakutaleta picha nzuri. Napinga suala hilo.

Nne, kura za walio nje zina utata huu au ule. Mjumbe aweza kushawishiwa na alipo au aliye naye huko na kupiga kura kutokana na ushawishi huo. Pia,itakwa ngumu kujua wangapi wamepiga na wamepigia upande gani. Napinga suala hili.

Kimsingi, kura za Wajumbe watakaokuwa nje ya nchi zisiruhusiwe. Kwanini ziruhusiwe sasa tu?

Mkuu hesabu ilishakosewa,tuwaache tu wapige maana kura ina ndiyo ina hapana na ina kuharibika.Nimewasikiliza leo aisee kuna sehemu moja nimeona kidogo wana logic,kuwa kama utasema walio nje wasipige basi hata wale wa ukawa hawatahesabika na wataohesabika ni wale 500 sasa kwa wajumbe mia tano waliobaki bungeni wana uhakika wa column kutimia.Tujipange kwa namna nyingine ila hapa kwenye kura tumezidiwa ujanja.
 
Mkuu hesabu
ilishakosewa,tuwaache tu wapige maana kura ina ndiyo ina hapana na ina
kuharibika.Nimewasikiliza leo aisee kuna sehemu moja nimeona kidogo wana
logic,kuwa kama utasema walio nje wasipige basi hata wale wa ukawa
hawatahesabika na wataohesabika ni wale 500 sasa kwa wajumbe mia tano
waliobaki bungeni wana uhakika wa column kutimia.Tujipange kwa namna
nyingine ila hapa kwenye kura tumezidiwa ujanja.

kyumana, hapa logic hakuna, kinachopingwa hapa ni kwamba kura inapaswa kupigiwa ndani ya chumba cha mpiga kura na sio kwamba usipokuwa ndani ya jengo wewe sio mjumbe wa BMK, usituzungushe tafadhari,,
 
Tukiwambia mje tuandamane mnabak kunyakunya tu. Acha magamba wafanye kaz yao
 
kyumana, hapa logic hakuna, kinachopingwa hapa ni kwamba kura inapaswa kupigiwa ndani ya chumba cha mpiga kura na sio kwamba usipokuwa ndani ya jengo wewe sio mjumbe wa BMK, usituzungushe tafadhari,,

Kabisa Mkuu
 
Leo wazi wazi nimemsikia akiwatahadharisha wajumbe kuwa sio vyema kuipigia kura ya hapana rasimu itakayopendekezwa kwa kigezo cha gharama. Yaani maono ya katiba kwa muktadha wa maridhiano kwake wala sio jambo la muhimu....yeye anataka kuonesha ubabe kuwa amefanikisha suala hilo ili apate sifa. Siku zotee waliopo nje ya bunge wamekuwa wakiambiwa warudi bungeni kwani huko ndipo maamuzi yatafanyika......sasa inakuwaje hawa watakaokuwa nje leo hii walazimishwe kufanya maamuzi hata wakiwa hija? Kila kitu kinafichwa kwenye kamati bila umma kuona nini kinafanyika huko ndani. Itoshe kusema kuna siri nzito inayofanywa na kiongozi huyu.... historia ni Mwalimu mzuri sana....na tusubiri
 
kyumana, hapa logic hakuna, kinachopingwa hapa ni kwamba kura inapaswa kupigiwa ndani ya chumba cha mpiga kura na sio kwamba usipokuwa ndani ya jengo wewe sio mjumbe wa BMK, usituzungushe tafadhari,,

Sawa lkn tukubali tu magamba yametuchapa bakora.Ujue mwisho ili tuseme akidi kuwa ilitimia au haikutimia si wanaangalia matokeo ya kura?
 
Mwenyekiti 6 yupo sahihi kabisa, hatuwezi kukwamsha zoezi ambalo kimsingi limefikia ukingoni.

Pia, kwa wale waliotoka nje ya bunge kwa kupinga kama ndugu zako Ukawa, kanuni hii mpya haitawalazimisha kupiga kura.

Jamani waacheni wabunge wengi popote pale walipo washiriki katka zoezi hili la kihistoria.

Katiba itapatikana
Vifungu vitapitishwa
Na wananchi watapiga kura ya ndio

Mtake ni hivyo, msitake ni hivyo.


Duh!
yani mtu apige kura kw akitu amabcho hakujadili? kwa mara ya kwanza niliona kw ajama yule wa hospitali.

pili, unasikiliza Bunge wewe? umemsikiliza sita leo akisema sio vifungu tena ila ni SURA kwa SURA, ili tuwahi Muda hautoshi.
 
CCM NI JANGA wameona hawawezi kufanikiwa bila kufanya huo unajisi wao wa kuruhusu waliopo nje kupiga kura mm napinga sana hili swala la kura kupigwa nje ya bunge la katiba ndo ccm wataibia kura huko lakini tutakuja kuwahukumu 2015
 
Lengo la kubadilisha hii kanuni ni kutaka kuchakachua akidi, hivyo orodha ya wapiga kura haitakuwa tena ya uhakika.
Ova
 
yangu macho taifa hilo litaingia kwenye machafuko ya kuchinjana kama mwenendo wa kupindisha pindisha mambo utaendelezwa na walio chakachua dhamana ya kuwaongoza watanzania. naichukia ccm na serikali yake kwa moyo wangu wote kwa mawazo na kwavitendo
 
Huna ulicho andika cha maana zaidi ya utashi wa nafsi yako na sio utaifa. Yaonekana umeleta mada hii kwa kutumika zaidi
ID yako na contents za andiko lako, vinapishana kwa umbali wa mbingu na dunia!

Hivi unayejiita Genius Brain, huoni kuwa hiyo kanuni iliyokuwa 'introduced' ya kupigia kura jambo zito la namna hii, hata kwa sms ya simu ya kiganjani, it is a joke of the century?!

Kinachoonekana dhahiri kufanywa na Sitta and his company maccm wenzake ni kutaka kuilazimisha hiyo katiba yao iliyokuwa drafted pale Lumumba, ipite by hooks and crooks!

Mwigulu Nchemba, mwanaccm mwenzao, alishawaambia kuwa lile bunge baada ya kutoka ukawa, 2/3 ya idadi ya wabunge ili katiba hiyo ipite, hiyo idadi haipo.

Naye AG Werema majuzi alipoongea na waandishi wa habari akalisisitiza hilo kuwa 2/3 ya wabunge wa kupitisha hiyo katiba haipo bungeni Dodoma, kwa hiyo akapendekeza yafanyiwe marekebisho madogo kwenye katiba ya sasa ya mwaka 1977, ili ziingizwe ibara ya kuwepo Tume huru ya uchaguzi, matokeo ya Urais kulalamikiwa mahakamani, iwapo atatokea mgombea ataona uchaguzi haukuwa free and fair na kuruhusu wagombea binafsi.

Hata JK alipokutana na ukawa waliafikiana kimsingi kuwa mchakato wa katiba usitishwe hadi baada ya uchaguzi mkuu wa mwakani.

Sasa iweje Sitta na wabunge wenzie wa magamba, wajifanye
'hamnazo kabisa' hadi kutaka kulazimisha mbinu za uchakachuaji ili mradi tu katiba yao ya Lumumba ipite?!

Kwa kweli hivi sasa kinachofanywa na maccm kimekuwa too much, kiasi ambacho inakuwa vigumu kwa sisi watanzania kuendelea kutolerate!
 
Ukienda Dodoma nje ya ukumbi wa Bunge kuna ulinzi mkali sana askari wameshika Bunduki, mbwa, farasi mabomu ya machozi n.k Duniani kote uliwahi kuona wapi katiba ya wananchi inayoandikwa hivo??Inayoandikwa ni katiba ya watawala (CCM) sio ya wananchi ndio maana wanaondika wanalindwa hivo. Katiba ya aina hiyo haina uhalali wowote na wala haikubaliki na haitaheshimiwa,,,,"Wananchi ndio chanzo cha mamlaka yote na serikali itapata madaraka yake toka kwa wananchi" Sasa iweje leo tuandikiwe katiba tusioipenda na maoni yetu yatupwe na ukiuliza unapigwa mabomu?? Watanzania tungekuwa makini na uchungu na nchi yetu wala hakuna haja ya kuandamana tungesubiri 2015 tuipumzishe CCM tuandike katiba yetu
 
Mkuu Petro, kutokuwepo utaratibu fulani nchini hakumaanishi kuwa utaratibu kama huo haufai. Ni sisi ndio tunaotunga sheria/kanuni na taratibu zenu na kama hivyo ndivyo tunaweza kurekebisha na kuboresha kukidhi matakwa na mahitaji.

Mwenyekiti 6 yupo sahihi kabisa, hatuwezi kukwamsha zoezi ambalo kimsingi limefikia ukingoni.

Pia, kwa wale waliotoka nje ya bunge kwa kupinga kama ndugu zako Ukawa, kanuni hii mpya haitawalazimisha kupiga kura.

Jamani waacheni wabunge wengi popote pale walipo washiriki katka zoezi hili la kihistoria.

Katiba itapatikana
Vifungu vitapitishwa
Na wananchi watapiga kura ya ndio

Mtake ni hivyo, msitake ni hivyo.

Kweli ni la historia kwa vitimbwi tulivyo viona ktk kutunga katiba ya Sitta!
 
Tutambue kuwa nchi haiko kwenye mikono salama huu ni wendawazimu sidhani kama mh sita anajua nini maana ya kazi maalumu huyu ni msomi mzuri na mwanasheria mzuri lakini usomi wake hauna hata chembe ya faida kwa watanzania ni huyu huyu sita aliyesema bungeni ni mahali pa kuandaa katiba leo anakuwa wakwanza kubadilisha kanuni ili katiba itungiwe barabarani kwa hili UWAPO POPOTE SEMA HAPANA KWA JOHN SAMWEL SITTA NA HII INADHIHIRISHA AKIPEWA NCHI AKILALA ATABADILISHA SHERIA ILI AFANYE ANAYOYATAKA SASA KAMPENI RASMI YA "OPERATION HAPANA KWA SITTA" NAOMBA MNIUNGE MKONO
 
Mimi si Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba. Lakini,kama mtanzania wa kawaida sana,nina haki za kutoa maoni juu ya jambo lolote lihusulo nchi yetu. Na leo,natumia haki yangu hii iliyopo chini ya Ibara ya 18 ya Katiba ya sasa kupinga kimaoni kuhusu Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba kupiga kura wakiwa nje ya nchi. Ninazo sababu mbalimbali za kupinga kimaoni suala hili.
Mosi, utaratibu wa kupiga kura kwa namna hiyo haukuwahi kuwepo na wala haupo hapa nchini mwetu. Kuanzia Katiba, Sheria za Bunge na hata Sheria Ndogondogo,hakuna suala kama hilo. Kwakuwa Bunge Maalum la Katiba linasimamiwa na Katiba ya sasa, Sheria ya Bunge Sura ya 83/2011 na Kanuni zake, sivyema kuleta jambo jipya lisilotambulika hata na Katiba ya sasa.BL halina upekee wowote wa kishera na kimantiki.
Pili, Bunge Maalum la Katiba lisilazimishe akidi. Kama Wajumbe hawapo basi.Waliopo wapige kura. Hakuna haja kuwatafuta popote walipo ili tu kukamilisha akidi ya wapiga kura na ya wakupitisha Rasimu. Hakuna cha kuwahi wala kuchelewa. Katiba ni yetu wenyewe. Twende taratibu.
Tatu, wananchi watataka kuona na kusoma nyuso za Wajumbe siku ya kupiga kura. Kupigia 'kifichoni' hakutaleta picha nzuri. Napinga suala hilo.
Nne, kura za walio nje zina utata huu au ule. Mjumbe aweza kushawishiwa na alipo au aliye naye huko na kupiga kura kutokana na ushawishi huo. Pia,itakwa ngumu kujua wangapi wamepiga na wamepigia upande gani. Napinga suala hili.
Kimsingi, kura za Wajumbe watakaokuwa nje ya nchi zisiruhusiwe. Kwanini ziruhusiwe sasa tu?

Tatizo six na baadhi ya wajumbe wanalazimisha akidi kwa maana ya kutaka kuweka historia ya kutengeneza katiba bila kujali ubora wake.
HAWA HAWANA NIA YA KUTUPATIA KATIBA MPYA, WANA NIA YA KUSIFIWA NA KUPONGEZWA KWA KUANDIKA KATIBA !
 
Back
Top Bottom