Naomba ushauri:
Wengi wanadhani nimependa kuwa hivi au tunaopenda wenzetu wa jinsia moja
tumetaka,La hasha!
Mimi ni mrembo sana,kuanzia sura,umbo,nina akili lakini pia nimekuzwa
familia ya dini sana.Nikiwa sekondari form 2 nilitokea kumpenda sana
dada mmoja yeye alikuwa Advance.Alinipenda sana pia ,ila kuliishia
kukumbatiana tu.
Nikiwa Advance nilipendwa na binti mmoja,niliogopa sana maana alikuwa
ananipa care kupita kiasi.Uhusiano ulifika mbali zaidi mpaka nikawa
mtumwa wa mapenzi.Sikuweza kula wala kufanya chochote bila yeye.
Nilikuja kugundua alianza uhusiano mpya hivyo tukaachana soon
nilipomaliza A level.Nikiwa chuo nilipata boyfriend kwa mara ya kwanza.
Nilijaribu sana kuwa nae karibu maana alinipenda sana na alinipa kila
kitu.Sikuwa najisikia mapenzi hata kidogo.Wengi waliniona nina bahati
maana alikuwa mzuri sana,mchapa kazi na ana akili zaidi ila tu
hajatulia.Nililigundua hilo nikiwa ndani ya uhusiano.Japo kila
nikimkamata anasema wanawake ndio wanamtaka ila hana time nao.Pamoja na
yote kwa kweli alinipenda.
Maombi yangu kwa Mungu yalikuwa na mimi niweze kuwa in love na
mwanaume.Niliomba sana na kufunga.Nilijitenga na wanawake.
Nilipomaliza chuo niligundua jamaa alikuwa bado hajatulia tukaachana
japo mwenyewe mapenzi hayakuwa kihivyo.Mara nyingi nilikuwa namkumbuka
my x,nilikuwa mnyonge sana.Nilijihisi kwa huyo bf mimi nilikuwa kama sex
mashine.
Nilikuwa mwaminifu sana ndani ya mahusiano.Baadae tukaachana, mimi
nikaamua kumdate mke wa mtu.Alinipenda mwenyewe .Sikuwahi kumwambia
chochote juu yangu.Ila kila wakati aliniita mpenzi,honey darlin na
kunikiss kila mara.Tulifall in love ila nilijilaumu kwa kuwa sikutamani
niwe na mwanamke tena ila sasa uhusiano na wanaume ulikuwa mgumu
,napendwa ila kupenda hakukuwepo.
Nikaona nitavunja ndoa ya watu nikawa namkimbia.Nikajikuta nafall tena
kwa mke wa mtu ambae alikuwa rafiki yangu.
Kila wakati aliniletea zawadi na kuniambia ananifeel sana.Tulidate kwa
muda kidogo nikaanza kumkwepa maana alianza kumchukia mumewe.Akiamka
break ya kwanza kwangu.Ananipeleka hoteli za kifahari.Ila pia alikuwa
kanizidi sana umri.
Nilipata shida sana kujitoa kwenye penzi lake maana aliapa kuniua
nikimuacha.Alinipenda kiasi cha kujitoa ufaham.Nilifanikiwa kumkwepa
karibia miezi 8 hivi.Namba ya simu nikabadili.
Tangu wakati huo naendelea kupata shida maana nimekuwa heart
breaker.Nikiumizwa tu na boyfriend kidogo huwa sirudi tena.
Nasali sana hii hali iniondoke lakini wapi.Naumia sana,Sijui
nifanyeje.Najua ni kinyume cha jamii na pia dini.Ila mimi sipendi pia
hali hii.
Mimi sio tom boy na hata mtu akiniona hawezi kudhani.Nimejikuta napendwa
na wanawake wengi ,sijui kwanini pia,huwa sijawahi kumtongoza mwanamke
yeyote ila wao hunianza.
Ninapokuwa na mwanamke kwenye mahusiano nasikia raha na moyo unarelax.
Nifanyeje?
Hii ni simulizi ya ukweli kutoka Masaki.