Watu hawajui tu. Tatizo hakuna aliyewahi kusema na ukisema unaitwa marioo etc, so inabidi kuwa siri kati ya wanawake hao na wanaume wao wa umri mdogo. kimya kimya
Ni raha sana sawa. Ila mtihani ni gia ya kuanzia kumtongozea.
Lazima uanze na shikamoo dada ama shikamoo mama kwa kuwa kakuzidi umri.
Halafu sasa ndiyo ifuate sijui 'ooh mama nina shida'
Ukiulizwa una shida gani, ndouanze kuzungusha lugha! 'Ooh sipendi kulisemea hapa labda unipe namba ya simu'
Super mkomao keshakusoma mwanzo na mwisho wa uelekeo wako, atakwambia simu bovu huku kakukazia macho akikutathimini!
Ndo hapo utapoanza kuropoka! 'Ooh mama siku nyingi natafuta muda wa kuliongelea suala hili, lakini nakosa....kiukweli ninakupenda'
Ana-serch authentication code yako ili aone kama yaliyomo yamo!
Atakutega 'wee kijana hivi mabinti zangu makamo yako hauwajui?
Unajibu 'ninawajua'
Anakuambia kwanini usiende kwa mabinti zake, badala yake unamfuatafuata yeye mbona hauna adabu?
Ndipo unapojibu 'kesi ya mama haimfungi mtoto'...'kwa hiyo nimekupenda wewe na si mwanao'.
Anakujibu 'mimi nitakuamini vipi, je kama unataka kutuchanganya?'
Wewe unajibu kwa kujiapiza.... 'haki ya Mungu mama me nakupenda wewe na sina tabia hiyo'
Anatabasamu huku anakusoma kwa ustadi mkubwa!
Anakupa masharti magumu ya kuingia kwenye penzi lake kama ifuatavyo, akihofia uwezekano wa kumchanganya yeye na wanaye vijana wenziyo...'Sitaki unapofika nyumbani uniamkie shikamoo', amkia 'za leo' ama 'za sahizi' na nitakutambulisha rasmi kwa wanangu kwamba sasa wewe ni baba yao'.
Mh! Nilikuwa najaribu kutengeneza gia ambayo hukuwezesha wewe kuwaingia kina mama watu wazima na kufanikisha kuwanasa!
Maana wengine ni wakorofi na vikienda vibaya unaweza kulambwa matusi mpaka ukaomba radhi.
Hongera kuukwea mbuyu kwa kuukumbatia, maana si kazi nyepesi kama wengi tunavyodhania.
Shida ya pili ni hao wanaye unaolingana nao makamo!
Wanakuita baba akiwepo mama yao ili kunridhisha.
Lakini kama hayupo, utaitwa kwa jina lako kavu huku yakicheka. Dah!
Mzee una kazi weye!