Nape: Usalama wa Taifa hausaidii nchi, wamekalia kusikiliza simu za watu

kwa maneno yako haya,je na mimi nikisema usalama wa taifa hawana meno/faida maana wanafanya kazi ambayo haifatiliwi ikiwasilishwa kwa vyombo vinavyohusika,je nitakua nimekosea nikisema kiboreshwe

Ni ukweli mkuu hawana meno kwasababu kama wanaweza kutoa taarifa tu lakini wasiweze kubadilisha madhara ambayo tunaweza kuyapata kama taifa! Kazi yao ina maana gani? Ila wanaweza kuwapoteza watu au kuteka watu ambao hawana madhara yoyote kwa taifa simply tu watawala hawataki/hawapendi kusikia maoni/mawazo tofauti ...too low.
 
Duuh, huyu babu, ndio vichwa hivi Msigwa anasema vinaongoza watu wanaowazidi upeo

MBUNGE NNAUYE, HOJA: Usalama wa Taifa ubadilishiwe majukumu kisheria ili watumike kuzuia ufisadi mkubwa nchini badala ya kazi za kusikiliza maongezi ya watu kwenye simu

WAZIRI MKUCHIKA, MAJIBU: Kazi ya Usama wa Taifa ni kuishauri serikali kimya kimya!
 
Majibu ya captain hayo, Hii ndio TZ.
Tumesikia mara ngapi chief wa CIA akitoa taarifa???

What does the director of the CIA do?
About CIA. ... The act also created a Directorof Central Intelligence (DCI) to serve as head of the United States intelligence community; act as the principal adviser to the President for intelligence matters related to the national security; and serve as head of the Central Intelligence Agency.Dec 19, 2006
About CIA — Central Intelligence Agency
Welcome to the CIA Web Site — Central Intelligence Agency › about-cia
MORE RESULTS

Kama una ushahidi director was CIA akitoa taarifa jinsi alivyoishsuri nchi katika mambo ya uchumi itafaa sana ili watu tufahamu kwa urahisi hoja yako.
 
Mkuchika ana majibu ya siasa ili kumridhisha Mkuu madudu yote ya bandarini mpaka leo mita ya kupima mafuta haijafungwa wao wapo busy na kusoma meseji na kusikiliza Simu kweli Tanzania inarudi nyuma miaka ndio inabadilika tuu...
 
Lakini hilo jukumu ni la kila mtanzania kuhakikisha anatoa taarifa ya kupandishwa ndege kwa Twiga kusafirishwa kwenda nchi za mbali.

Ni kila mtanzania ana wajibu huo wewe mimi, wana JF na wananchi wote kwa ujumla.

Tena kwenye hili la masuala kama Twiga na Makinikia ni watanzania wenyewe walohusika kusuka mipango yote.

Sasa hapo utangoja aje mwanaTISS aje kumuangalia Twiga akipaa au utatoa taarifa kwa vyombo vyote polisi TISS au jeshi kwamba kuna dhuluma itafanyika kwenye uwanja wa ndege?

TISS ni sehemu ya watanzania na sasa hivi wanaonekana wanafanya kazi zao bila kubughudhiwa.

Hizi kelele za watu wanatekwa au wanajiteka au kushambuliwa nafikiri yanataka yaaminishwe tu kwamba ni TISS ndo wanaohusika.
Mkuu,
Naona bado unaiamini hiyo kauli na sidhani wewe hadi umri wako huyo umeshawahi kufanyo lolote la kuripoti uhalifu.
Kwa mfano ulioweka wa twiga hivi ni kweli unaamini hadi TISS wapewe taarifa? Polisi nao na vitengo vyao? Hao wanyapori nao? Usiishi kwa kauli za kihenga katika zama za leo ambazo kunateknolijia kubwa. Ukubali kuna watu tuliowaamini ama wamejiaminisha kuwepi kwa ajili yetu hawatimizi hizo wajibu.zao.
 
Hao usalama wa taifa sasa hivi wanashinda huku kwenye mitandao ya kijamii kutishia wakosaoji na kuharibu mijadala inayaoikosoa serekali na hasa pale rais anapokosolewa. Ikifika jioni wanakwenda bar kutongoza mabar maid na kuishia kujisifia kwamba wanaijua sana serekali, huku wakati mwingine wakilewa kuonyesha vijibastola vyao.


Who cares mkuu?? Nchi ya majuha, nani anajali usalama wa watu wewe. Huo usalama ni wa sisiem na sio taifa bana.
 
Namshangaa sana Nape...........!!!! wakati akikomaaa na jambo hilo la Usalama wa Taifa jimboni kwake Mtama baadhi ya Wakulima wa Korosho wanalia bila hata kupata Msaada kwani wamedhulumiwa pesa zao za Mauzo ya Korosho na Chama cha Msingi Mtama............Na kama kweli Mhe Nape ni Msafi na Mchapa kazi lishughulikie jambo hili linalowaumiza Wananchi wako wa Mtama bila hata kupata Msaada............!!!!

chama cha Ushirika MTAMA waiba Pesa za Wakulima
 
Usalama wa taifa karibu wote ni member humu JF kwa kutumia ID bandia, kila siku wanashinda humu kusaka umbeya, kuunganisha taarifa, kuitetea serikali na kuna wakati utawakuta lile jukwaa la MMU wakikata stress zao.

Ukiwemo wewe mwenyewe.
 
Tuache ushabiki, hivi hawa usalama wanakuwaga wapi hadi watu wanapiga dili vza escrow, EPA, iptl, makinikia, makontena kuibwa bandarini et al?
.kwann tusikubali kwamba enzi za mwl bosi wa usalama alikuwa marehem Imran Kombe huyu bosi aliiweka vzr kazi yake kiasi cha kufanya usalama kuwa na heshima.

Baada yake, usalama zaid ya kujisifia mm mtu wa serikal mara ooh mm najua hivi ama vile hawana kingine zaidi. Siri zinavuja, wahamiaji Haram wanaingia kila uchwao, vichanga vinakufa huko mnh wao wapo tuu. Hii ni aibu
Nape bado analia na uwaziri ndugu hahahaha
 
Idara hii hapo awali ilikuwa Idara takatifu, adilifu, kimbilio,saidifu, lkn leo watu wakiona Nissan nyeupe wanajawa hofu kama sio kukimbia. Na hiyo yote inatokana na sababu moja tu, idara imenajisiwa na siasa.
 
Back
Top Bottom