Nape Nnauye: Tumehujumiwa..

Nape Nnauye: Tumehujumiwa..

kwanini NEPI ASIJE MWENYEWE HAPA KUTUELEZA MSIMAMO WA CHAMA CHAKE. YEYE SI NDIO AFISA HABARI WA CCM(ITIKADI NA UENEZI) ?
 
Kila jambo na wakati wake hongera CHADEMA kwa ushindi huo,waongo wameumbuka.Tuwape vijana nguvu na mbinu bora za kuikomboa nchi yetu hasa elimu ya uraia.
 
Kinachoiua haraka ccm ni harakati zao za kukinusuru chama hali ya kuwa hawaujui msukosuko gani unakisibu. mpaka sasa hakuna anayejipanga kusimamia matakwa ya wananchi, wanalazimisha matakwa ya chama kwa wananchi. KITAKUFA HAKIKA.
 
Niliwai sema,Nape atambue kuwa CCM sio yake ina watu wake..na wale waliokuja kwenye kampeni ndio wana-CCM..chama kinashikiliwa na genge moja la kimafia.
 
Ni kweli kauli ya SENDEKA ya kuendekeza ukabila na ile ya LUSINDE kumwaga matusi zaidi ya mlevi wa gongo hata kama mimi ningekuwa mpiga kura wa Arumeru nisengekipigia kura chama cha namna hiyo.

Wawatumie watu wenye staha na lugha njema kwenye kampeni zao


hawana hata mmoja anaekubalika kwa wananchi ni uchakachuaji tu
 
CCM mkome kuiba kura, pale ambapo uchaguzi ni jimbo moja upinzani unaweza kuweka nguvu yote kulinda kura, CCM haiwezi kushinda kamwe. Labda kwenye uchaguzi mkuu ambapo upinzani una uwezo mdogo wa kulinda kura nchi nzima
 
Nape, atambue kuwa huo ndio ukweli kuhusu CCM. Siamini kauli yake kuwa wamehujumiwa, ni matunda ya harakati za kupata nafasi iliyo nono ndani ya chama chenu. Hata kabla ya matokeo naamini Nape alikuwa anajua kuwa chochote kinaweza kutokea ktkt uchaguzi wa arumeru. rejea uchaguzi wa 2010, Nasari alikuwa jirani sana kupewa nafasi, na inawezekana mfumo kandamizi wa CCM unaobebwa na nguvu za dola ulichangia kumfanya ashindwe. Kwa hiyo sio ajabu yeye kushinda. Igunga CCM ni kama ilishindwa kwa kurejea nafasi ya CHADEMA kwa mwaka 2010. Hiyo sio hali njema kwao kama hawatajipa muda wa kutafakari na kujitambua, wataendelea kupoteza ushawishi katika siasa za nchi hii na wapiga kura watendelea kuwakataa tena kwa nguvu kubwa kuliko hii. Angalia matokeo ya Udiwani utapata picha halisi CHADEMA wameshinda viti vilivyokaliwa na CCM hapo kabla. Kuna nini hapo?
 
Hawa CCM kweli wamepoteza uwezo kuona uhalisia wa mambo. Fikiria mgombea wa CCM jimbo la Karatu 2010 alikuwa anajigamba kuwa atambwaga Dr. Slaa, kweli ni akili hiyo? Slaa na umaarufu wake tangu 1995 pale Karatu na mambo mazuri yaliyofanyika ya maendeleo ndani ya kipindi cha ubunge wake pale Karatu, pamoja na masuala ya kitaifa makubwa sana aliyoyaibua bungeni Dodoma, bado yule mgombea wa CCM ambaye ndio kwanza anaanza siasa ametoka serikali eti anao ubavu kumbwaga Slaa, na aliposhindwa, anasema eti Chadema wamemuibia kura. Kweli Chadema waiibie CCM yenye vyombo vyote vya dola? inawezekana wapi? Ni kukosa uwezo wa kuona uhalisia wa mambo
 
Aje basi ajibu hoja kwamba ''ccm imeshindä arumeru inasubiriwa kutangazwa'' atangaze basi tuone
 
Nilambe nisilambe!!!!! mkuda anadeki!!!! mitusi tupu hii mijamaa tena mbele ya kadamnasi ya watoto. Kweli inanikumbusha kipindi cha mnara wa babeli watu walipokuwa wanakufuru kisha wakawa wanaongea lugha gongana na mpango wao mbovu ukakwama. ccm should pave way now for fresh air of democracy
 
Hawawezi kukosa kisingizio. Najuwa hawatasingizia kuibiwa kwa kura zao, manake mwizi ni vigumu kuibiwa. Watasingiziana wao kwa wao, kulaumiana wenewe napengine lazima kuna magamba flani yatalazimika kujivua. Aibu tupu. Huenda wakamtupia lawama Lowasa.

Ama kweli mwisho wa aibu ni aibu kubwa, watajibeba tu mwaka huu, cdma waleeeeeee wanasonga mbele
 
Nape kapatia haswa, ni kweli kulikuwa na watu wasiokubalika kwenye jamii katika uchaguzi, ndio maana hawakushinda. Igunga 'walishinda" kwa sababu Nape hakupanda jukwaani kupiga kampeni! isitoshe Chama cha matusi, hakikubaliki ktk jamii! Hizo ni salaam kwa bwana matusi Lusinde!
 
Mkiacha kujifanya hamjui kwamba watu wamewachoka basi mtajua kwanini mnashindwa hata igunga mlishindwa ila mlilazimisha
 
:yo:Mwisho CCM umefika,watu wameshachoka na maisha duni kila kukicha!
Kilichobaki ni mazishi na matanga ya CCM 2015 pale CDM wakichukua nchi
Believe or not, Mkapa ,Wasira na makada wenzake watawaambia nini
tena watanzania kwa matusi waliyokuwa wanaporomosha kwenye kampeni
DIE SLOWLY CCM!!!!!!
 
Back
Top Bottom