Chikaka Sumuni
JF-Expert Member
- May 16, 2013
- 1,337
- 770
Wakuu,
Kwa zaidi ya siku 10 nilikuwa likizo nyumbani Mbulu. Nikaamua kutumia likizo yangu Dongobesh ambako kulikuwa na uchaguzi wa Udiwani. Kama mnavyojua tuliwashinda ccm kirahisi. Na nitaeleza zaidi mbinu iliyotumika kuwashinda kirahisi kwenye uzi mwingine.
Hata hivyo, kwa leo naomba kupata ufafanuzi kutoka kwa Nape Nnauye katibu mwenezi wa CCM Taifa kuhusu kauli aliyoitoa Mbulu tarehe 15/6/2013, kata ya Dongobesh katika mkutano wa hadhara uliofanyika karibu na ofisi za CCM. Naomba ufafanuzi wa kauli yake hiyo, kwa sababu kwangu mimi inaleta utata mkubwa sana kwa kuzingatia kilichotokea siku hiyo hiyo Arusha tena kwa mtu ambaye yeye alimtaja kwa jina - yaani Freeman Mbowe.
Nanukuu kauli Nape Nnauye katika mkutano huo wa hadhara uliofanyika baada ya Mbowe Kuondoka kutokana na watu wote kuhamia kwa Mbowe na Nape Nnauye kulazimika kusubiri Mbowe aondoke kwanza ndiopo afaye mkutano.
katika mkutano wake Nape Nnauye alisema;
kwanza nawapa pole kwa kuachiwa mavumbi na helikopta ya CHADEMA. Kabla Mbowe hajapaa nilimwandikia meseji kwenye simu yake. Nilimwambia kuwa watu wa Arusha wamechoka na Maandamano sasa wanataka amani. Nikamwambia utaikuta aibu yako Arusha.
Maswali,
kwa kuwa jumamosi siyo siku ya uchaguzi, uchaguzi ni siku inayofuata, mimi nikajiuliza ni aibu gani atakayoikuta Mbowe Arusha jumamosi ya 15/6/2013? Maana angesema kuwa Kesho (jumapili ya 16/6/2013) ningefikiri kuwa Nape Nnauye anazungumzia aibu ya CHADEMA kushindwa uchaguzi. Mbowe Arusha alikutana na Mabomu ambayo kuna kila dalili kuwa yalimlega yeye na Lema. Swali langu ni Je, mabomu hayo ya Arusha ndiyo aibu ya Mbowe aliyoizungumizia Nape Nnauye huko Dongebsh Mblu?
Pili, Nikiunganisha kauli hii ya Nnauye na kauli ya Mwigulu Nchemba kwamba msipoichagua CCM Arusha mtakufa, halafu nikaunganisha dots zangu na kauli ya Mbowe kuwa anaushahidi wa video wa Polisi kuhusika na tukio la mauaji ya Arusha, mwishowe nikahitimisha kwa kauli ya Waziri mkuu Pinda kwamba bomu hilo lilitengenezwa China na huwa linatumiwa na wanajeshi kujilinda, napata jibu langu la uhakika moyoni. Sijui wewe.
Je kuna mtu amlirekodi hotuba ya Nape hapo Dongobeshi? Nadhani ushahidi huu ni tosha kuunganisha dots. Yaani kama mpaka hatua hii CCM hawajakubali kwamba Mungu amewakataa basi wasibirie muziki wake kamili pia.