Nape Nnauye: An exemplary leader!

Nape Nnauye: An exemplary leader!

Exemplary
Imenibidi ni Google. Nimesoma sana toka std 4 mpaka chuo nje ya nchi. Lakini hili neno ndo nakutana nalo leo.

serving as a desirable model; representing the best of its kind.

"an award for exemplary community service"
 
VILAZA WA CCM

UKAWA wakikosoa mtu au jambo,

"Yaani hawa UKAWA wanapinga kila kitu kinachofanywa na CCM"

Nape kafanya vizuri, UKAWA wakimsifia

"Yaani hawa UKAWA vigeugeu sana, juzi tu walikuwa wanamponda leo wanamsifia"

My Take: Watanzania wengi Vichaa
 
Dah... Watanzania ni wajinga jamani tuseme ukweli ndio maana ccm inawabinuabinua inavyotaka!

Hivi Nape leo wa kusifiwa kwa lipi hasa?
 
Public Administration aliyoisoma naona anaitendea haki huku uraiani
 
Ukiwa Majukumu, Mipaka ya Kazi basi pia upewe Mamlaka juu ya hayo unayojasimamia. ( Responsibility and Authority). Nape amekuwa anatembea kwenye Eneo lake la Kazi na Hadidu zake za Rejea za Kazi yake. Kweli inatamwinua. Mwisho wa siku itajulikana nani ni mtetezi wa Watanzania
 
VILAZA WA CCM

UKAWA wakikosoa mtu au jambo,

"Yaani hawa UKAWA wanapinga kila kitu kinachofanywa na CCM"

Nape kafanya vizuri, UKAWA wakimsifia

"Yaani hawa UKAWA vigeugeu sana, juzi tu walikuwa wanamponda leo wanamsifia"

My Take: Watanzania wengi Vichaa
Mkuu binadamu tunatawaliwa na kitu inaitwa rational conduct , na si unazi kutokana na ushabiki wa kisiasa.

Hata mimi ni mpenzi wa Mh Magufuli lakini matendo ya Makonda yamekiuka viwango vya kiuongozi ulliotukuka nchini.

Hatuingii katika ushabiki katika suala la Makonda lakini tunamsifu Nape for calling a spade, a spade.

Na vile vile Nape kachukua hatua kwa utaratibu wa uwazi na wa haki katika kuonyesha madhaifu ya Makonda, ambaye ni vigumu kusema kuwa hakutendewa haki.
 
2.jpg


Nimeheshimu sana msimamo wa Nape Nnauye, kijana mdogo(kwangu) ambaye amesimamia si tu kauli yake bali hata kwa vitendo kuonyesha udhaifu uliotokea katika eneo lake na kuchukua hatua stahiki kulielezea, kuchunguza na hatimaye kama aivyosema , kukabidhi kwenye mamlaka husika.

Mtu kuwa mkweli, ni mpenzi wa Mungu.

Unafiki, woga wa kutumbuliwa hausaidii sana mbele ya ukweli.

Nape ameonyesha jinsi ambavyo amekuwa consistent katika suala zima linalo mkabili Makonda.

Kama tungekuwa na viongozi kama Nape, kutokubali kuwa waoga hata pale wanaofanya madudu katika maeneo yao ya utawala ni wakubwa, tungekuwa mbali kiuwajibikaji.

Vyeti feki vina eneo lake, wenye eneo hilo wako kimya kama maji ya mtungi, wanajitukanisha kwa kweli.

Hata leo, Nape aidha akiondolewa au kujiuzulu, mfano chanya utakuwa umewekwa katika uongozi wa Taifa.

Watu kama hawa huja kwa nadra.

Big up Nape Nnauye, mwana wa Moses.
He is doing well now,lakini huko nyuma alikera sana.Inaelekea ameachana na uchumia tumbo,labda ilikuwa utoto.
 
Siku zote huwa namchukia sana tena na kumdharau mtu yeyote hata akiwa mzaz wangu asiyeona makosa yake, na kutumia mada huo kutukana wanaomwambia amekosea,, huyo mtu hunabudii kumfuta kati ya viumbe ulivyowahi kutuna navyo,,,. Budget ya jiji la dsm inaweza kuwa kubwa zaid ya wizara ya habari na michezo haukuwepo urazima wa kulinganisha vitu hivi maana kodi za wanach ndio walengwa. Kama ni kwelii ujumbe uliosambaa jana kuhusu kwann wazr afatlie kilichofanyika clouds ulitoka kwa rc wa dsm ntakuwa wa kwanza kutazama vyeti vyangu upya na ntahamin Bashite ni Bashite
 
hongera sana kaka NAPE keep it up, mungu atazidi kukusimamia, uko tofaut kabisa na viongoz wengine ambao ni wanafiki na wasalit pia....... inaskitisha wazir wa mwenye dhaman na jesh la polis ameamua kukaa kimya
 
Now nape amekuwa kiongozi mzuri sana kwa utendaji wake ktk wizara yake amekuwa jasiri xaxa hivi kila kitokeacho akikiona co anakizungumzia bila kukipindisha big up Nape
 
Cjui hii jamaa inaungwa mkono na nani huko ccm manake wengine wote hawawezi kusimamia misimamo yaoo mbele ya mkuluu
Ila jamaa huenda kagundua tofauti ya job na work
Manake job ni huo uwazir
Na work ni ubunge wake
So cyo kesi kupoteza job nikabaki na work
 
Nape ni hafanyi mambo kwa kuiga bhana, ni kiongozi aliyeivishwa sana na Waasisi wa Taifa Hili hususani mzee Uwazi na ukweli
 
Kwa hili la leo Nape kaonyesha ukomavu wa hali ya juu.

Big up Nape.... Mbingu imeshuhudia ukipingana na mipango ya ibilisi. komaa hivyo hivyo
 
Ukiona chadema wanakusifia lazima utakuwa umekosea sehemu-J.P.Magufuli
Sina hakika sana kama wote wanaomsifu Nape hapa ni Chadema mi nadhani wapo pia wasiokuwa na vyama na pia wapo baadhi wa CCM. Ishu ni kuwa mitizamo tunatofautiana, si kila anayetofautiana nawewe ama na rais basi ni chadema, that is big noooo! Binafsi sina chama kabisa.
 
Back
Top Bottom