Drifter
JF-Expert Member
- Jan 4, 2010
- 5,369
- 5,512
Ukiona chadema wanakusifia lazima utakuwa umekosea sehemu-J.P.Magufuli
Bila shaka wewe kila amkosoaye Magufuli na "protégées" wake kama Makonda kwa chochote kile lazima awe CHADEMA. Ni dalili za kuweweseka kufikia kuona hata maadui wasioonekana na hata mtu kutaka kukimbia kivuli chake. Mara sijui tuzime mitandao ya kijamii; tufukuze wasaliti n.k. Hadi mnajikuta mmebaki wachache tena mnaoangaliana kwa shaka na tahadhari.
Nape hakuamka asubuhi moja tu na kuamua kufanya alichofanya. Kuna mawimbi yanapita chini kwa chini (undercurrents). CHADEMA hawahusiki zaidi ya kuwa watazamaji tu.
