Nape ni mwanzilishi wa CCJ

Hii mada imenifurahisha kidogo labda na mimi nitoe mchango wangu kidogo.moja kwa moja nakubaliana na wale wanaomuona Nape Mnafiki kwa sababu.
1.Unapokua hukubaliani na sera za upande mmoja unachotakiwa ni kutundika madaruga yako na kwenda kule ambako unafikiri mtaongea lugha moja,na ndio maana sina shida na wale wanaohama kwa either kunyimwa madaraka ndani ya chama kwa kuonewa au vinginevyo.

2.Unapokua ndani ya fungate ya chama fulani maana yake ni kwamba umekubaliana nacho hivyo yapasa uendane na sera hizo,kama kuna usiyokubaliana basi uyamalizie humo.

3.Unapokua unatumikia chama,mwajiri au ni sehemu ya familia fulani yapasa kulinda haki ya kupata na kutotoa siri za upande uliopo kwani kwa kufanya vinginevyo wewe si mwaminifu,ni mtu hatari katika hiyo jamii.

Ujumbe wangu;
Nape kama hakukubaliana na CCM alipaswa kuachana nao(kuvua Gamba-maana halisi)halafu akaenda upande mmoja CCJ,au CDM tukajua anachokipigania,lakini sio kutoa siri za CCM ukazipeleka kuzianzishia CCJ,(hapo hakuna confidentility,)na huo sio uongozi.Unafiki ni kitu kibaya sana.Huwa unabeba kitu kinaitwa undumila kuwili.Unaloliongea sio unalolitenda na kumaanisha ,bali kuna jingine nyuma ya pazia.Kwa hiyo napata shida na wale wanaotaka kumpa ushujaa kijana huyu.

Na ndio maana kwa mwajiri mzuri unapotaka kazi kwako moja atataka kujua uzoefu wako,maana ya kwanza kujua kama umekutana na challenges kiasi gani ambazo utamsaidia pindi ukianza kazi,lakini la pili na la muhimu ulikotoka uliondokaje? Hapo ndio kwenye umuhimu mkubwa,kwani unapokua huendani na mwajiri wako utaomba kuacha kazi kwa kufuata taratibu husika bila kuharibu sifa ya mwajiri wako kwa sababu ulikua sehemu ya ile familia,mabaya au mazuri ni sehemu ya maisha yale,unatakiwa kuyaacha na kwenda kuanza maisha mapya.kama unapiga mawe piga ukiwa nje sio ndani,na ukipiga ukiwa ndani tuna haki ya kukufukuza.

Naomba nisiwachoshe nina mengi ya ku-mtima tutaongea wakati mwingine.kina NAPE NI WATU HATARI KWA TAIFA LETU.

- Not really kama kuna ambayo hukubaliani na chama chako you create a political crisis as what CCJ did, Mwalimu alipoona CCM inaanza kukosa mweleko aliwapigia kampeni kina Mrema, sasa utaita ule unafiki? No that is how National politics is played, unaweza ukatoka chama au ukabaki na kutafuta njia za kisiasa za kupata attention ya chama chako, Mpendazoe ndiye mtu wa hatari sana now ninaelewa kwa nini CCM walimtema!

ES!
 
- I mean ni Demokrasia at work, tatizo ni kama Mpendazoe kwa kujitoa CCM na kuingia Chadema amevunja sheria ya jamhuri au mnafiki, none ishu kama chama changu naona kinakosa mwelekeo ninayo haki ya kutumia kila njia za kisiasa kutafuta attention ya kusikilizwa na chama changu, kwani CCM haijui waliotaka kuanzisha CCJ?

- National politics ndivyo zinavyochezwa, CCM waliwajua sana wale wote walioshiriki CCJ, lakini inafanyika tathmin ya chama ya kisiasa, kuona umuhimu wao wakiachiwa watoke, chama kinaona haikwezi kua-afford, kwa hiyo wanaitwa na kuulizwa tatizo lao wanasema na sometimes wanapewa nafasi katika chama kurekebisha waanayoona hayafai, that is how national politics is played, Mpendazoe was not a threat to CCM wakamruhusu aondoke na wengine wote walioruhusiwa kuondoka, it has nothing to do na unafiki it is simply how national politics are played!


Es!


Penye red:

CCM inawajua fika, na isipoanza kuwataja wengine, basi ingojee kuumbuliwa zaidi na Mpendazoe, ambaye bila shaka ataendelea kuwataja wale wengine. CCM haijui ifanye nini katika hili suala maana wale wengine ambao haijawataja Jk tayari amewapa vyeo -- sijui kwa nini. Hawa ni Sitta na Mwakyembe. Pia yuko ule Makonda wa UVCCM mkoa wa Kilimanjaro.

Nionavyo mimi hii tutaona mengi katika hii pandora box aliyoifungua Mpendazoe na utabiri wangu ni kwamba hii ndiyo mwisho wa Nape. Nape angekuwa sharp na witty, angetambua hilo kuweza kutokea na angeweza ku-preempt -- kwa yeye kusema kwamba alijifanya kujiunga CCJ ili kupata siri ya vigogo gani wa CCM wanaisapoti au walikuwa tayari kujiunga na chama hicho. Angalau hapo Nape angepona.

Lakini pia huenda ni kweli alipewa kazi hiyo na chama chake CCM kuifanya (even though this is highly unlikely) lakini baadaye JK alikosa ujasiri (kama kawaida yake) ya kuchukuwa hatua ya kufaa kuwatimua vigogo wote waCCM wale walijihusisha na CCJ.

By the way -- Where is mzee wetu Mwanakijiji? Aliishabikia sana CCJ na bila shaka anaelewa mengi. Huu siyo wakati wa kumwaga yale yaliyojiri? Come on MMKJJ!!!
 
Wewe william ni mjinga kati ya wajinga. Hivi umeelewa anachokizungumza mpendazoe au ni ushabiki wako tu wa siasa za baba yako Malacella!!!

- Unajua mtu mjinga huwa ni vigumu sana kujiona, na huwa ni rahisi sana kukimbilia kuita wengine wajinga ungeongelea ujinga wako kwanza ambao unajionyesha wazi na haya maneno yako! Nini hoja yako?

Es!
 
Penye red:

CCM inawajua fika, na isipoanza kuwataja wengine, basi ingojee kuumbuliwa zaidi na Mpendazoe, ambaye bila shaka ataendelea kuwataja wale wengine. CCM haijui ifanye nini katika hili suala maana wale wengine ambao haijawataja Jk tayari amewapa vyeo -- sijui kwa nini. Hawa ni Sitta na Mwakyembe. Pia yuko ule Makonda wa UVCCM mkoa wa Kilimanjaro.

Nionavyo mimi hii tutaona mengi katika hii pandora box aliyoifungua Mpendazoe na utabiri wangu ni kwamba hii ndiyo mwisho wa Nape. Nape angekuwa sharp na witty, angetambua hilo kuweza kutokea na angeweza ku-preempt -- kwa yeye kusema kwamba alijifanya kujiunga CCJ ili kupata siri ya vigogo gani wa CCM wanaisapoti au walikuwa tayari kujiunga na chama hicho. Angalau hapo Nape angepona.

Lakini pia huenda ni kweli alipewa kazi hiyo na chama chake CCM kuifanya (even though this is highly unlikely) lakini baadaye JK alikosa ujasiri (kama kawaida yake) ya kuchukuwa hatua ya kufaa kuwatimua vigogo wote waCCM wale walijihusisha na CCJ.

By the way -- Where is mzee wetu Mwanakijiji? Aliishabikia sana CCJ na bila shaka anaelewa mengi. Huu siyo wakati wa kumwaga yale yaliyojiri? Come on MMKJJ!!!

- Mkuu angalia neno la Nape, Mpendazoe angejiuliza CCJ ilikufaje, unalielewa hilo neno maana yake kwa National politics?

- CCJ ilikufaje?


Es!
 
Kwa hiyo unachotuambia ni nini? Fine alikuwa mwanzilishi wa CCJ then what. Kwa sababu hata yeye alishiriki akiwa bado yuko CCM, je huo siyo unafiki. Kwa nini hakubaki ndani ya CCJ ili aijenge na kuifanya iwe maarufu badala ya kuhamia CDM? Hivi vyama ni kama mitumbwi ya kukuvusha ng'ambo kwa usalama. Lakini lililo la msingi ni kwamba yeye Nape yuko CCM na anatetea sera au misimamo ya chama chake , kama ambavyo na yeye Mpendazoe ana haki ya kutetea sera na misimamo ya Chadema.

Hii siyo contest ya loyalty kwa chama hiki au kile, na ndiyo maana leo tunaona mwanasiasa huyu yuko kule na kesho yuko huku. Hata hiyo loyalty hupimwa wakati ukiwa ndani ya hicho chama na siyo baada ya kuondoka. Je Mpendazoe anataka kutuambia kwamba alipokuwa CCM kwa miaka yote hii hakuwa na loyalty na kwamba jicho lake lilikuwa kwenye upinzani? Naweza kuelewa frustrations za Mpendazoe hasa baada ya vigogo wenzanke kumchuuza ahame na wenzake watamfuata halafu wakamtosa lakini in politics kupima upepo huwa imo. Nani alijua leo hii Ntagazwa angekuwa huko aliko au Dr. Slaa huyu? Katika siasa haya yote hutokea na yanapotokea mtu hutakiwa kila la heri kule aendako na akishindwa na kurudi hasutwi. Waone Makongoro Nyerere, Wasira, Nsazugwanko na hao akina Mpendazoe, Shibuda, Kahigi, Slaa, Ntagazwa na wengine wengi.


- Strong analysis, saafi sana!

Es!
 
ndo raha ya kimbelembele......................napeeeeeeeeee,,,,,,,, ingia CHADEMAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA

Nani anamtaka. Tunataka watu makini wenye kuchuja pumba na mchele! Huyu anatema pumba tuu nani azoe bomu! Akae huko huko atajua mbivu na mbichi mwaka huu.
 

- This is very interesting, maana looking at the times lini CCJ ilikufa na lini Nape ameenda kuwa DC Masasi haikubaliani kabisa, however Mpendazoe angeenda mbele zaidi kwamba anamuonaje Marando? Mtei ambaye naye alitokea CCM? anamuonaje Dr. Slaa ambaye naye alitokea CCM na alijitoa tu baada ya kunyimwa nafasi ya kugombea ubunge Karatu? anamuonaje Shibuda? Seif Hamadi? Na yeye mwenyewe anajionaje?

- Point yake ni nini hasa kwamba ni makosa kwa kiongozi kubadili au kutaka kubadili mawazo ya kisiasa? I am lost hapa!
, I mean talking about unafiki wa kisiasa? Nani ni mnafiki hapa?


William @ NYC, USA.

Mkuu mjadala huu umetekwa na partisan interests kiasi cha kwamba watu hawataki tena kufanya reasoning, kama hiyo reasoning itamaanisha watu kukubali hili au lile mradi aliyetoa hoja anakuwa perceived kuwa wa chama hiki au kile. Hakuwa uhusiano kati ya harakati za Nape kwenye CCJ na kupewa kwake u-DC maana kama ulivyosema, it took months toka wakati wa harakati za CCJ mpaka hapo alipoukwaa u-DC na hapo katikati alishiriki kura za maoni za kuwania ubunge kwa tiketi ya CCM. Wakati wote huo Mpendazoe alikuwa ameshatoka CCJ na kuelekea Chadema na hata kushiriki kwenye kura za maoni Segerea na kushindwa na Rachel Mashishanga na hata kutaka kukimbilia jimbo la Kinondoni. In my view obsession ya Mpendazoe ilikuwa ni ubunge bila kujali ni wapi.

Hoja ni kwamba, hata kama Nape alishiriki kuiasisi CCJ, hakuna wakati hata mmoja aliosimama popote pale ku-renounce CCM au kumsema vibaya Rais na wakati huo wote alikuwa mjumbe wa NEC-CCM. Hapa unafiki unaingiaje? Kwa kutohama kutoka CCM kwenda chama kingine baada ya kuanguka kwa CCJ? Kama ni hivyo basi asiishie kwa Nape, awataje na wengine ambao tunajua walikuwa watoke Chadema pia. Nape amekuwa mpambanaji dhidi ya ufisadi wa ndani ya CCM na alikuwa very clear juu ya hao anaowahusisha na ufisadi na hakuna hata wakati mmoja alipata kutamka kwamba JK ni mmoja wao, sasa hicho kinachoitwa kuzawadiwa cannot arise. Tunaweza kusema if anything, aliyezawadiwa ni Mpendazoe aliyepewa nafasi ya kugombea baada ya kushindwa kwenye primaries.
 
Mimi huwa nashangazwa kidogo na namna mijadala inavyogeuka kuwa vita binafsi kati ya wachangiaji na kuwa a name calling contest. Yuko mtu aliyekasirishwa sana na mchango wangu na nimeishia kuitwa a bitch kwa sababu tu nimehoji ubaya wa Nape kushiriki katika kuunda CCJ. Sasa hivi nahusishwa kinasaba na Nape, lakini wale waliochangia kwa namna ya kusapoti hoja za Mpendazoe ni wazuri na hata majina yao ni malaika na watakatifu. Come on! Hivi ni lini ustaarabu utapewa nafasi? Nimesema vyama ni come outfit tu ambazo zaweza kuvaliwa kutegemeana na mazingira ya wakati huo na objective ya yule aliyevaa hiyo outfit. Wengine wanaiita hiyo kama political tribalism ambayo athari zake ni chanya mradi tu huyo mtu anatekeleza kile anachokisimamia kwa manufaa ya wananchi. Ukienda Kenya, Raila Odinga ambaye ni doyen wa opposition politics alikuwa katika mapambano na Kanu na Moi na hatimaye akaanza harakati za kuunda Ford, baadae akaenda Ford Kenya, then NDP halafu akarudi Kanu (iliyomuweka kizuizini kwa zaidi ya miaka 8) halafu akaishia LDP, NARC, ODM-K na kisha ODM. Hii yote aliifanya ili kufikia malengo aliyojiwekea kisiasa.

Hoja hapa ni kwamba kwa wanasiasa, kuhama vyama au kuanzisha vyama ili kufikia malengo haiwezi kuwa dhambi na ndiyo maana Mpendazoe aliondoka CCJ alipoona hapati alichokusudia na wala haonekani kuwa ni Tinkerman au Hopper. Sasa hata kama kungekuwa na ushahidi kwamba Nape alikuwa ameandaliwa kuwa Mwenyekiti wa CCJ, that would not be a capital offence and it wouldn't disqualify him from holding a post within CCM. What if he had decided to defect to Chadema. Would he be 'punished' the way he is being punished now.

Mijadala humu iakisi hoja na hoja iwasilishe level of maturity expected of the contributors ili na wao wachangiaji wazitendee haki computer zao, air time na muda wao wa thamani. Kamwe isigeuke uwanja wa vita au uwanja wa ku-demonstrate maradhi yetu ya kichwa.

- Saafi sana, mkuu hii ndio JF wewe weka hoja na sio siri uko juu sana kwa hoja so! weka hoja mkuu kuna tunaozikubali maana zimeshiba sana hoja zako!

Es!
 
- The main goal is to win the elections!

Es!
Yes you win the election then what is next, that is stupid idiology i can say, ndiyo maana viongozi wengi wa kiafrika wanashindwa kuendeleza nchi zao hawajui hata kilichowapeleka pale hawana action plan yeyote waliyopanga kwa kipindi chao ndiyo maana unaweza kuta mtu anatoa ahadi za ma-trion wakati nchi haina uzalishaji wowote kwa kutegemea kukopa asipotimiza matokeo yake ni kuanza kuongoza kimjini mjini au kuanza kutumia vyombo vya dora ili abaki madarakani.
 
Yes you win the election then what is next, that is stupid idiology i can say, ndiyo maana viongozi wengi wa kiafrika wanashindwa kuendeleza nchi zao hawajui hata kilichowapeleka pale hawana action plan yeyote waliyopanga kwa kipindi chao ndiyo maana unaweza kuta mtu anatoa ahadi za ma-trion wakati nchi haina uzalishaji wowote kwa kutegemea kukopa asipotimiza matokeo yake ni kuanza kuongoza kimjini mjini au kuanza kutumia vyombo vya dora ili abaki madarakani.

- It happens everywhere in the world, ask Obama where is the change? the main goal ya chama chochote cha siasa duniani ni kushinda uchaguzi kwanza!

Es!
 
CCJ yamuumbua Nape
• Alitumika kuandaa katiba, kupokea fedha, kutafuta ofisi ya CCJ


SIRI za Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye, zinazomhusisha na mipango ya kuwahi kukigeuka chama chake na kuanza taratibu za kujiunga na Chama Cha Jamii (CCJ), zimezidi kuanikwa na wale aliokuwa nao katika mipango hiyo.

Baada ya wanasheria na wajumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mabere Marando na Profesa Abdallah Safari, kumtaja Nape kuwa mmoja wa wana CCM wanafiki, jana ilikuwa ni zamu ya Fred Mpendazoe kueleza kile alichokiita "unafiki, usaliti na uhaini wa Nape Nnauye ndani ya CCM anayojifanya kuipigania."

Mpendazoe aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Kishapu kwa tiketi ya CCM katika Bunge lililopita, alijitoa mapema mwaka jana na kujiunga na CCJ kabla ya kuhamia CHADEMA.

Akihutubia mamia ya wakazi wa mji wa Mbamba Bay katika mfululizo wa maandamano na mikutano ya hadhara ya CHADEMA inayoendelea kwenye mikoa ya Nyanda za Juu Kusini, Mpendazoe alisema sasa ameamua kuliambia taifa ukweli kuhusu Nape Nnauye ili umma wa Watanzania uepuke kudanganywa na propaganda za CCM zinazotolewa na kijana huyo.

Huku akiweka wazi kuwa yeye ni mmoja wa waanzilishi wa CCJ, Mpendazoe alisema kelele zote anazopiga Nape kuitetea CCM leo hii ni za kinafiki kwani tayari alishakiona chama hicho hakifai na akashiriki katika mipango yote ya kuanzisha CCJ.

Akitoa mfano wa jinsi Nape alivyoshiriki katika kuanzisha CCJ, Mpendazoe alisema kijana huyo alishiriki kuandika katiba ya chama hicho.
Alisema ndiye aliyepewa jukumu la kutafuta nakala za katiba za vyama vingine tawala nchini Afrika, ili kupata katiba nzuri ya kuigwa katika kuandika Katiba ya CCJ.

Aliwaambia wakazi wa Mbamba Bay kuwa Nape alilitekeleza vizuri jukumu hilo, kwani alifanikiwa kuipata Katiba ya Chama cha ANC kinachotawala Afrika Kusini, ambayo alisema ndiyo iliyotumika kwa kiasi kikubwa katika kuandika Katiba ya CCJ.

"Huyu Nape anayepiga kelele za kuitetea CCM kujivua gamba ni mnafiki mkubwa pengine kuliko wanafiki wote hivi sasa. Nathibitisha kwa wananchi wa Mbamba Bay na Watanzania wote kwa ujumla kwamba Nape Nnauye alishiriki kuanzisha CCJ. Nilikuwa naye; tulikuwa wana CCM sita. "Nape ni mhaini ndani ya CCM kwa sababu alishakula njama za kutaka kuiangusha, tofauti na Nape, mimi nilijiamini mapema na nilijitoa CCM mapema baada ya kuona hiki chama hakiwafai Watanzania.

Sasa leo wanajivua gamba halafu Nape wanampa cheo. Niwaulize, hivi kati ya Nape na Lowassa yupi ni mbaya na kwa CCM? Ni Nape aliyeona CCM haifai na kushiriki kuanzisha CCJ ili kuiangusha au ni Lowassa?" alihoji Mpendazoe na umati ukajibu "Wote hawafai." Kisha aliendelea:
Tulifanya naye vikao vyote vya siri hadi tukaanzisha CCJ, leo anaitetea CCM, ni mnafiki mkubwa", alisema Mpendazoe na kushangiliwa.

Katika hotuba yake hiyo iliyoonekana kuteka hisia za mamia ya wasikilizaji, Mpendazoe alisema CCJ ilianzishwa kwa siri kubwa na Nape alishiriki kikamilifu katika kuhakikisha mawasiliano yao yote yanakuwa ya siri kwani walifungua mtandao maalumu wa kuwasiliana kwa internet.
Hata hivyo, alisema baadaye wenzake waliufuta mtandao huo baada ya kubadili mawazo dakika za mwisho, hasa baada ya kuahidiwa vyeo na Rais Kikwete.

Alisema hata pale ilipolazimu kukutana, yeye, Nape pamoja na wengine, walikuwa wakipendelea kukutana kwenye vinywaji eneo la Mlimani City jijini Dar es Salaam ili wasitiliwe shaka na maofisa Usalama wa Taifa aliosema walikuwa wakiwapeleleza wana CCM wote waliohisiwa kula njama za kuanzisha chama kipya.

Mpendazoe aliyewahi kuwa msemaji wa CCJ taifa kabla ya chama hicho kunyimwa usajili wa kudumu, alisema Nape alibadili mawazo ya kujiunga CCJ dakika za mwisho baada ya Rais Jakaya Kikwete kumuahidi na hatimaye kumteua kuwa mkuu wa Wilaya ya Masasi. Alibainisha kuwa kitendo hicho kinaonyesha jinsi kijana huyo asivyo na msimamo na alivyo na uchu wa madaraka.

"Lengo letu la pamoja lilikuwa ni kupinga uongozi mbaya wa CCM na ufisadi tukiwa nje ya CCM, maana haiwezekani kupambana na ufisadi ukiwa ndani ya CCM. Ukifanya hivyo unakuwa adui. Lakini kumbe mwenzetu ndani ya moyo wake kilichomsukuma kuanzisha CCJ ni kukosa cheo kikubwa ndani ya CCM.

Sasa hilo sikulijua, nililijua baada ya Rais Jakaya Kikwete kumteua kuwa Mkuu wa Wilaya ya Masasi. Hapo alibadili mawazo ya CCJ. Ni kijana msaliti, mnafiki na asiye na msimamo, hafai kuongoza watu, ana uchu wa madaraka … kama si kupewa ukuu wa wilaya Nape asingekuwa CCM leo. "Alikuwa anatazama tu majaliwa ya tumbo lake. Huyu naye ni fisadi lakini hajavuliwa gamba, wanafiki watupu", alisema Mpendazoe na kuamsha shangwe zaidi.

Aidha, alieleza kuwa ili kuwaepuka maofisa Usalama wa Taifa, wakati mwingine walikuwa wakifanya vikao vyao vya kuanzisha CCJ ndani ya gari pamoja na Nape akiwepo.

Alieleza zaidi kuwa Nape akiwa idara ya mambo ya nje ya CCM katika ofisi ndogo ya chama hicho Lumumba jijini Dar es Salaam, ndiye aliyekuwa akiiba siri za CCM zilizohusu kuwafukuza wote waliohisiwa kuwemo kwenye mpango wa kuanzisha chama kipya cha siasa.
Alieleza kuwa Nape anayemjua yeye ni mtu asiyeukubali uongozi wa Rais Jakaya Kikwete katika chama na serikali, kwani katika vikao vyao vya mwanzoni kabisa walivyoazimia kuanzisha CCJ, kijana huyo alikuwa akimkosoa Kikwete na kuelezea udhaifu wake.

"Na ndiye tuliyekuwa tukimtuma kwa wafadhili kupokea fedha za kuanzishia CCJ. Ndiye aliyetafuta pango la ofisi ya CCJ. Kwa kuwa yeye alikuwa kijana zaidi, alifanya mambo mengi ya kufuatilia kwa siri taratibu za uanzishwaji wa chama.

"Kikwete anaongoza chama feki, CCM ina watu ambao walishamdharau kama Nape na ambao wanamuona ni kiongozi dhaifu…lakini kwa sababu mwenyewe aliwapa vyeo bila kuwajua, leo wamelazimika kubakia ndani. Mimi siwezi na ndiyo maana leo nipo CHADEMA nikiendeleza dhamira ile ile ya kuwanusuru Watanzania na ufisadi," alisema na kushangiliwa tena.

Aliwataka wakazi wa Mbamba Bay kutorudi nyuma na kurubuniwa tena na CCM inayosema imejivua gamba, kwani suala hilo limejaa usanii na unafiki mkubwa. Alisisitiza kuwa kote alikopita na CHADEMA amejiridhisha kuwa chama hicho sasa ndiyo kipenzi na tumaini pekee la Watanzania.

"Mimi sitarudi nyuma kama Nape, nitasonga mbele na CHADEMA, tumekwenda kwenye vijiji na miji mingi, CHADEMA ndiyo tumaini pekee la Watanzania….ndugu zangu tusirudi nyuma, huu ndiyo wakati wa kujikomboa. Kila haki na wakati wake…tusiipoteze fursa hii," alisema. Wakati Mpendazoe akitoa tuhuma hizo juzi, Nape alikaririwa na vyombo vya habari kuwa hajawahi kushiriki katika CCJ huku akiwatuhumu wanaomhusisha nayo wanafanya hivyo kwa lengo la kumchafua.

Mkuu,
Shukrani kwa kuweka taarifa nzima maana ktk kuanzisha tread ulikuwa na haraka ya kuposti na kuacha paragraphs zenye uzito mkubwa ktk habari ya Nape 'kuibomoa' CCM akiwa ndani na bado anaendelea na kazi hiyo kwa wadhifa mkubwa zaidi ndani ya CCM, maana sijapata kusikia habari kuwa Nape aliwahi kujitoa CCM.

Na sisi wataka mabadiliko ya CCM iondolewe ktk kushika dola, habari hii ni nzuri kwetu ya jinsi CCM wanavyomalizana wenyewe.
 
wewe mtetezi wake huwezi kuona tatizo sababu wote mnaongozwa na njaa wengine wanaongzwa na nia na dhamira ndio maana Mpendazoe anashangaa nape yule yule leo amegeuka na kuanza kumsifia jk aliyekua anamtukana kwamba hana uwezo wa kuongoza ama baada ya kupewa ukuu wa wilaya tu na kupewa uenezi mara uwezo wa jk umepanda ghafla Biblia inasema heri adui kuliko mnafiki nape ni hatari kwa taifa anaweza kufanya chochote ili apate madaraka, hongera cdm kwa kuzidi kuwaanika hawa wachumia tumbo ili umma uwajue, ndio maana alichukua pesa kwa jeetu patel kwa ajili ya kampeini zake za nec

Mwenzetu umejaaliwa matusi ya reja reja na hatuwezi kukubadilisha. Inawezekana kabisa hapo ulipo hata mlo ni tatizo na mimi naomba nikuambie tu kwamba huyo Nape simfahamu personally lakini hapa niko driven na issues bila kujali ni Nape au mwingine yeyote. My reasoning does not revolve around personalities unless personality is an issue.

Tunarudia tena kusema kwamba Mpendazoe has alot of more important issues to address that revealing his bitterness about how he thinks he was duped into jumbping ship to found CCJ. He should recover and continue serving wananchi honourably! If he thinks Nape is wrong discussing people within Chadema, he (Mpendazoe) shouldn't have allowed himself to stoop as low. My feeling remains that the useless sideshows would end if the leaders from across the political devide decide to re-trace their route and serve what is in the best interest of wananchi.
 
Huu utaratibu Wa kila anayekosoa Chama chetu tunamuandama kwa style ya character assassination Nadhani sio mzuri unafanya CDM ionekane kazi yake kuchafua watu. Ushauri wangu ni kujibu tuhuma kuliko kuandama watu. Huyu Mpendazoe alikuwa wapi kuyasema haya? Ataibuka mwingine naye ataandamwa vivyo hivyo ....
 
Siasa tamu sana! Kumbe Nape ana uchu wa madaraka kiasi hicho? Shame upon you Nape! Unaidhalilisha CCM

Yaani Nape alipohongwa u-DC kwenda Masasi tu akabadili mawazo ya "kizalendo" aliyokuwa nayo!
 
Kama Nape ni mwanzilishi mmojawapo wa CCJ basi ni mtu jasiri mwenye kupenda mabadiliko na hilo halina tatizo lolote kama mabadiliko aliyokuwa akiyataka kupitia CCJ atayafanikisha kwa nafasi yake ya uongozi CCM. CCM haina shida na watu walioihama kwani hata waziri Wassira aliwahi kuwa mpinzani na sasa mjumbe wa kamati kuu.
 
Back
Top Bottom