- Thread starter
- #41
Nape alifikiri siasa ni mchezo rahisi akawaparamia RACHEL wamemtoa jasho ngoma nzito kule sasa anataka kucheza kote kote nje na ndani anataka kucheza mziki wa Chadema mfupa uliowashinda kina Makamba yeye atauweza.Mkuu CCM kama chama cha siasa lengo lake ni kuendelea kuongoza serikali, hawawezi kujimaliza wenyewe, na ndio sababu ya kujivua gamba.
Sasa wakati Nape akiendelea kuutangaza ujumbe huu, Mpinzani anakuja na kuanza kumfagilia bila kujua kuwa huyu jamaa alikuwa hapendezwi na mambo yalivyokuwa yanaenda ndani ya CCM na alikuwa na mpango wa kuunda chama cha kupingana na ile CCM ya Zamani, mkuu sio kumfanya aonekane ni mtu makini zaidi na anayejua analolifanya?huku sio kuufanya ujumbe wake wa CCM Mpya uaminike zaidi kwa wananchi?