Nape ni mwanzilishi wa CCJ

Mkuu CCM kama chama cha siasa lengo lake ni kuendelea kuongoza serikali, hawawezi kujimaliza wenyewe, na ndio sababu ya kujivua gamba.

Sasa wakati Nape akiendelea kuutangaza ujumbe huu, Mpinzani anakuja na kuanza kumfagilia bila kujua kuwa huyu jamaa alikuwa hapendezwi na mambo yalivyokuwa yanaenda ndani ya CCM na alikuwa na mpango wa kuunda chama cha kupingana na ile CCM ya Zamani, mkuu sio kumfanya aonekane ni mtu makini zaidi na anayejua analolifanya?huku sio kuufanya ujumbe wake wa CCM Mpya uaminike zaidi kwa wananchi?
Nape alifikiri siasa ni mchezo rahisi akawaparamia RACHEL wamemtoa jasho ngoma nzito kule sasa anataka kucheza kote kote nje na ndani anataka kucheza mziki wa Chadema mfupa uliowashinda kina Makamba yeye atauweza.
 
Mimi sioni shida ama taabu kwa Mtanzania yeyote kujiunga ama kuanzisha chama chochote cha siasa hapa nchini kwa sababu nchi yetu ni ya VYAMA VINGI VYA SIASA.

Hofu yangu ni kuwa kumbe vyama vingi hapa nchini havina dira wala uelekeo kwa vile katiba zao ni 'madesa' ya vyama vingine kutoka nje ya nchi kama Bw. TUNGU MPENDAZOE alivyoeleza bila kujikanyaga. Kwa hali hii nchi yetu itaendelea kuwa masikini siku zote! Sasa naanza kukubali kuwa sehemu kubwa ya wanasiasa ni watu waliofeli mitihani yao shuleni na kuamua kuingia kwenye siasa ndio maana hawana mawazo mapya kwa maendeleo ya nchi hii. Mazingira ya ANC ya huko Afrika Kusini ni tofauti mno na mazingira ya nchi yetu. Wazee wa CCJ waliibuka kwa mbwembwe na TUNGU aliwemo (MSc) naye akiinizwa mkenge na aikana NAPE hadi kudesa katiba za watu.

Ee Mwenyezi Mungu Taifa hili limekosea wapi hadi leo tuko hapa? Inua vijana wako wa kike na wa kiume wasaidie nchi hii, amen.
 
Vita umeanza mwenyewe, sasa unalia nini?
Nape unarusha mawe, Vita umeianzishaa!
Mawe warusha vyovyote, hata hauna malengo
Ulianza na Mafisadi, sasa umewagwaya

Mara Slaa mwana zuoni, jiwe ukamrushia,
Umekuwa kama chizi, Unarusha bila dira,
Dawa ya moto motoni, Dawa ya mawe unaipata,
Ulianza na Mafisadi, Aibu umeipata

Aibu umeipata, Mafisadi sasa wako
Sasa unawatetea, Magamba ni nguo zako
Umma hauna chelea, wanapima kwa vigezo
Ulianza na Mafisadi, sasa umetota jasho

Vita umeianzisha, subiri utaipata
Wameanza kupuuza, kumbe hauna dira
Dira yako yote tamaa, na uchu wa madaraka
Ulianza na Mafisadi, sasa unawatetea

Eti kwa ufinyu wako, wadhani bado twalala,
wataka kutuadaa, ili kutupumbaza,
Hatudanganyi kwa kanga, kwa chumvi wala kofia
Ulianza na Mafisadi, mbona wamekushinda

Shirikisha akilizo, Fikiri kabla ya kunena,
Mja na mwana vitendo, Tanzania ndio baba,
Tetea kwanza nchi yako, ndipo utaeleweka,
Mafisadi ulianza nao, sasa unawatetea.
Shairi limetulia mzee Nape kawashindwa kina RACHEL sasa anahaha na CDM atauweza mziki wa Chadema kwa mawazo yake alifikiri atajibiwa na Dr. wa ukweli ili amtoe Slaa kwenye focus yake matokeo anajibiwa na watu tofauti kabisa Slaa wala asihangaike naye. Namshauri Nape ahangaike na nyumba yake ni chafu kabla ya kushafisha ya jirani.
 
Jamani jamani,NAPE ndo kituko cha mwaka! Kumbe aliasisi ccj? Ndo uyo uyo aliyeomba kugombea ubunge pale Ubungo kupitia chadema,wakagundua ni kilaza wakasema hapana,ubungo tuna simba wa ukweli MNYIKA, nape alikula ela ya EPA akiwa na Jitu patel, nape ndo anayevujisha siri za NEC ya ccm?duh! Mi nlikuwa najiuliza kwa nini hata hotuba ya Rais jk inakuwapo jf siku mbili kabla ya yeye kuitisha vyombo vya habari! Wakati wapinzani mpaka siku ya kuongea na media huwezi kujua wataongelea nini! Nape ndo anasema mafisadi watafukuzwa wakati katibu mkuu anasema ccm haina list ya mafisadi! Nape analipwa mshahara wa dc na wa katibu mwenezi wa ccm! Nape ni wa ajabu kweli. Nape ahaminiki. Nape ni tapeli. Nape nape nape!
 
Nape ajifunze toka kwa Lowassa. Siku zote Lowassa amekuwa anaongelea sera na si issue za mtu mmoja mmoja tena personal isssues. Hivi Nape hajiulizi pamoja na 'wingu' zito linalomzunguka Lowassa kwa nini haongelewi sana kwenye mikutano ya hadhara? Na sio tu Nape, ni vigumu sana kwa kiongozi yeyote toka ccm (hata wa kata) kuanzisha siasa za mambo binafsi maana wana 'skeleton' wengi mno kwenye makabati yao.

Sikio la kufa... - And I am sure kuna mambo zaidi ndani ya kabati la Nape.
kwa nini? hata mimi sijui mkuu
 
Shairi limetulia mzee Nape kawashindwa kina RACHEL sasa anahaha na CDM atauweza mziki wa Chadema kwa mawazo yake alifikiri atajibiwa na Dr. wa ukweli ili amtoe Slaa kwenye focus yake matokeo anajibiwa na watu tofauti kabisa Slaa wala asihangaike naye. Namshauri Nape ahangaike na nyumba yake ni chafu kabla ya kushafisha ya jirani.

Naomba hilo shairi limfikia popote alipo!
 
acheni kumsakama Nape....Stephen Wassira alikuwa nani na saivi ni nani? Hizo ni siasa tu na kwenye siasa uadui haudumu
nape kuwa mwanzilishi wa ccj hakuna tatizo lolote mbona hata muasisi wa ccm hayati mwalmu jk nyerere aliwahi kusema ya kwamba ccm sio mama yake hivyo mkumbukw ya kwamba ajira kuu ya napa ni siasa hajawahi kufanya kazi nyingine Zaidi ya siasa kwa hiyo kama aliona ya kuwa hakuwa amepewa alichokuwa anataka kwa wakati ule alikuwa na kila sababu ya kutafuta mahali pa kujishikiza
 
sasa ndio naelewa kwa nini Makamba alimfungia duniani hadi mbinguni, wengi hatukumuelewa yule mzee kumbe alikuwa anamjua vizuri nape ni mtu wa aina gani, pia ninapata picha kuwa Makamba kwa nini aliamua kuharibu chama, inawezekana kabisa mwenyekiti wake hakuwa anamsikiliza kwenye masuala muhimu ya kujenga chama, kwa tuhuma hizi inatosha kwa Nape kuachia ngazi kwa kuwa nae ni GAMBA,
 
Kati ya vitu ambavyo haviwezi kuvumilika katika jamii ya waungwana ni usaliti, tuhuma ambazo zimetolewa na Fredy Mpendazoe za kuwa wewe ni mmoja wa waanzilishi wa CCJ ni mbaya mbaya na mbaya zaidi ni kitendo chako cha kudhoofisha chama cha mapinduzi kwa kutoa SIRI za vikao vya chama, Najua mwenyekiti wako atakuita na atakwambia upime mwenyewe uzito wa tuhuma hizi, ila nakushauri kama kijana mwenzetu usisubiri uitwe, uchukue hatua stahiki za kuachia ngazi kwenye nafasi zote za uongozi ndani ya chama.
 
Huna lolote, kwani tuhuma za Nape dhidi ya Chadema si alitoa akiwa Singida? Au wananchi wa Singida wameendelea kuliko wa Mbamba Bay? Hakika CCM inaelekea kufa maana ubaguzi na dharau kwa wananchi imeshamiri kiasi hiki.Iwe Mbamba bay au Dar ujumbe umefika na ndio maana wewe uliyepo mjini umepata taarifa hii. Halafu kwamba Nape hakupata nafsai ya kujibu wewe sio mfuatiliaji au unaleta ushabiki. Hivi kuwa CCM akili lazima zihamie tumboni? Siku zenu zinahesabika

Acha hoja za kitoto, ebu nionyeshe hapo alipopewa nafasi ya kuzijibu hizo tuhuma za EPA na Kuomba Kugombea Ubunge kwenye habari hii?

Nilichosema..kuna changamoto nyingi sana zinawazunguka watu wa Mbambabay na mazingira yao,hoja hizo zingezungumza zaidi zingewafanya watu wa Mbambabay walione tumaini la kesho kupitia Chadema, lakin kwa kuipoteza nafasi hiyo kwa kumuongelea CCJ ambaye ata hawamjui ni kitu gani,ni kuipoteza nafasi hiyo muhimu. Ni muhimu sana kuyasoma mazingira ya watu.
 
Kwa hiyo unachotuambia ni nini? Fine alikuwa mwanzilishi wa CCJ then what. Kwa sababu hata yeye alishiriki akiwa bado yuko CCM, je huo siyo unafiki. Kwa nini hakubaki ndani ya CCJ ili aijenge na kuifanya iwe maarufu badala ya kuhamia CDM? Hivi vyama ni kama mitumbwi ya kukuvusha ng'ambo kwa usalama. Lakini lililo la msingi ni kwamba yeye Nape yuko CCM na anatetea sera au misimamo ya chama chake , kama ambavyo na yeye Mpendazoe ana haki ya kutetea sera na misimamo ya Chadema.

Hii siyo contest ya loyalty kwa chama hiki au kile, na ndiyo maana leo tunaona mwanasiasa huyu yuko kule na kesho yuko huku. Hata hiyo loyalty hupimwa wakati ukiwa ndani ya hicho chama na siyo baada ya kuondoka. Je Mpendazoe anataka kutuambia kwamba alipokuwa CCM kwa miaka yote hii hakuwa na loyalty na kwamba jicho lake lilikuwa kwenye upinzani? Naweza kuelewa frustrations za Mpendazoe hasa baada ya vigogo wenzanke kumchuuza ahame na wenzake watamfuata halafu wakamtosa lakini in politics kupima upepo huwa imo. Nani alijua leo hii Ntagazwa angekuwa huko aliko au Dr. Slaa huyu? Katika siasa haya yote hutokea na yanapotokea mtu hutakiwa kila la heri kule aendako na akishindwa na kurudi hasutwi. Waone Makongoro Nyerere, Wasira, Nsazugwanko na hao akina Mpendazoe, Shibuda, Kahigi, Slaa, Ntagazwa na wengine wengi.

Kwenye red... Hahahaaa yaelekea Nape kaka yako ww.... unasikia kuaga dunia aisee na hii habari... JK alishagundua kuwa nape anapenda sana madaraka yaani ana uchu kiduku wa madaraka... atahama kama wakimtoa thats is
 
Nape alifikiri siasa ni mchezo rahisi akawaparamia RACHEL wamemtoa jasho ngoma nzito kule sasa anataka kucheza kote kote nje na ndani anataka kucheza mziki wa Chadema mfupa uliowashinda kina Makamba yeye atauweza.

Ninachokiona sasa ni Chadema kuanza kuucheza muziki wa Nape, sasa naanza kuiona Chadema nayo ikianza kukaba baada ya kushambulia kwa muda mrefu.
 
Kwa hiyo unachotuambia ni nini? Fine alikuwa mwanzilishi wa CCJ then what. Kwa sababu hata yeye alishiriki akiwa bado yuko CCM, je huo siyo unafiki. Kwa nini hakubaki ndani ya CCJ ili aijenge na kuifanya iwe maarufu badala ya kuhamia CDM? Hivi vyama ni kama mitumbwi ya kukuvusha ng'ambo kwa usalama. Lakini lililo la msingi ni kwamba yeye Nape yuko CCM na anatetea sera au misimamo ya chama chake , kama ambavyo na yeye Mpendazoe ana haki ya kutetea sera na misimamo ya Chadema.

Hii siyo contest ya loyalty kwa chama hiki au kile, na ndiyo maana leo tunaona mwanasiasa huyu yuko kule na kesho yuko huku. Hata hiyo loyalty hupimwa wakati ukiwa ndani ya hicho chama na siyo baada ya kuondoka. Je Mpendazoe anataka kutuambia kwamba alipokuwa CCM kwa miaka yote hii hakuwa na loyalty na kwamba jicho lake lilikuwa kwenye upinzani? Naweza kuelewa frustrations za Mpendazoe hasa baada ya vigogo wenzanke kumchuuza ahame na wenzake watamfuata halafu wakamtosa lakini in politics kupima upepo huwa imo. Nani alijua leo hii Ntagazwa angekuwa huko aliko au Dr. Slaa huyu? Katika siasa haya yote hutokea na yanapotokea mtu hutakiwa kila la heri kule aendako na akishindwa na kurudi hasutwi. Waone Makongoro Nyerere, Wasira, Nsazugwanko na hao akina Mpendazoe, Shibuda, Kahigi, Slaa, Ntagazwa na wengine wengi.

Sijaona unafiki wowote wa MPENDAZOE kwa maana mtu mnafiki ni yule anayejifanya kuwa na mawazo sawa na aliko ilihari anafanya mambo yanayopingana na alipo. Sasa kama azima ilikuwa ni kuondoka CCM basi Mpendazoe alifanikisha hilo na ana kila sababu ya kupongezwa kwa kuyakimbia maozo ya CCM na kutafuta mahari pa kuweza kutafuta usawa katika kuliendeleza taifa. Huyo Nape ndo mnafiki na ataendelea kuwa mnafiki kwa maana aliyajua yaliyo mabaya ya CCM na akata kuondoka kwa sababu ana uchu wa Madaraka kama walivyosema hapo juu aliamua kubaki humo ndani na huku roho yake ikimsunta kuwa mahari alipo si mahari pema hata kidogo.

Mpendazoe hakuondoka CCJ kwa sababu ya kutapatapa ila kwa hira walizofanyiwa na msajili wa vyama vya siasa anayeongozwa na fikra pungufu na zinazokufa kila kukicha za CCM kwa kukihujumu chama cha CCJ. Sasa kwa mpiganaji kama unaona sehemu moja unayojaribu inashindikana unatafuta another alternative. Upiganaji wa Mpendazoe ndo huo tunaouona wa kuweza kutafuta in anyhow njia ya kuweza kuwatumikia watanzania katika chama chenye mwelekeo wa kulikomboa taifa.

Kwa tafsiri yako ulitaka abaki kwenye chama ambacho Tendwa aliapa na Makamba kwamba hakitaweza kusajiliwa Tanzania. Hiyo ni sawa na mvuvi hodari aliye baharini baada ya dhoruba kutokea na mtumbwi wake kutobolewa kubaki humo eti aoneshe uhodari wake ilihari mtumbwi unazama. Ataonesha uhodari wake kwa kuogelea na kutafuta mitumbwi isiyozama ili aendeleze uhodari wake wa uvuvi. Kabla hajafanya hivyo hufanya awezalo ili auzibe lakini kama haiwezekani huondoka kusalimisha maisha yake na uhodari wake kama alivyofanya Mpendazoe alipopigana kukiokoa CCJ lakini kwa sababu juhudi zake zilishindwa na nguvu ya Dora akaamua kuogelea kutafuta mitumbwi isiyozama ingawa wengine wasiohodari walienda kwenye mitumbwi iiliyotota na ambayo itazama muda si mrefu(Mwenyekiti CCJ= CCM)
 
nape kuwa mwanzilishi wa ccj hakuna tatizo lolote mbona hata muasisi wa ccm hayati mwalmu jk nyerere aliwahi kusema ya kwamba ccm sio mama yake hivyo mkumbukw ya kwamba ajira kuu ya napa ni siasa hajawahi kufanya kazi nyingine Zaidi ya siasa kwa hiyo kama aliona ya kuwa hakuwa amepewa alichokuwa anataka kwa wakati ule alikuwa na kila sababu ya kutafuta mahali pa kujishikiza

?????????????
 
Ninachokiona sasa ni Chadema kuanza kuucheza muziki wa Nape, sasa naanza kuiona Chadema nayo ikianza kukaba baada ya kushambulia kwa muda mrefu.
Kumbe hujui hata kazi ya katibu mwenezi kwa sasa Nape hajui hata aanze na lipi aache lipi badala kueneza sera za chama chake anabaki kujibizana na kina Mpendazoe kama si kutapatapa ni nini unaweza kutuambia kaishia wapi na kina RACHEL.
 
Kwenye red... Hahahaaa yaelekea Nape kaka yako ww.... unasikia kuaga dunia aisee na hii habari... JK alishagundua kuwa nape anapenda sana madaraka yaani ana uchu kiduku wa madaraka... atahama kama wakimtoa thats is

Mimi huwa nashangazwa kidogo na namna mijadala inavyogeuka kuwa vita binafsi kati ya wachangiaji na kuwa a name calling contest. Yuko mtu aliyekasirishwa sana na mchango wangu na nimeishia kuitwa a bitch kwa sababu tu nimehoji ubaya wa Nape kushiriki katika kuunda CCJ. Sasa hivi nahusishwa kinasaba na Nape, lakini wale waliochangia kwa namna ya kusapoti hoja za Mpendazoe ni wazuri na hata majina yao ni malaika na watakatifu. Come on! Hivi ni lini ustaarabu utapewa nafasi? Nimesema vyama ni come outfit tu ambazo zaweza kuvaliwa kutegemeana na mazingira ya wakati huo na objective ya yule aliyevaa hiyo outfit. Wengine wanaiita hiyo kama political tribalism ambayo athari zake ni chanya mradi tu huyo mtu anatekeleza kile anachokisimamia kwa manufaa ya wananchi. Ukienda Kenya, Raila Odinga ambaye ni doyen wa opposition politics alikuwa katika mapambano na Kanu na Moi na hatimaye akaanza harakati za kuunda Ford, baadae akaenda Ford Kenya, then NDP halafu akarudi Kanu (iliyomuweka kizuizini kwa zaidi ya miaka 8) halafu akaishia LDP, NARC, ODM-K na kisha ODM. Hii yote aliifanya ili kufikia malengo aliyojiwekea kisiasa.

Hoja hapa ni kwamba kwa wanasiasa, kuhama vyama au kuanzisha vyama ili kufikia malengo haiwezi kuwa dhambi na ndiyo maana Mpendazoe aliondoka CCJ alipoona hapati alichokusudia na wala haonekani kuwa ni Tinkerman au Hopper. Sasa hata kama kungekuwa na ushahidi kwamba Nape alikuwa ameandaliwa kuwa Mwenyekiti wa CCJ, that would not be a capital offence and it wouldn't disqualify him from holding a post within CCM. What if he had decided to defect to Chadema. Would he be 'punished' the way he is being punished now.

Mijadala humu iakisi hoja na hoja iwasilishe level of maturity expected of the contributors ili na wao wachangiaji wazitendee haki computer zao, air time na muda wao wa thamani. Kamwe isigeuke uwanja wa vita au uwanja wa ku-demonstrate maradhi yetu ya kichwa.
 
Mimi sioni shida ama taabu kwa Mtanzania yeyote kujiunga ama kuanzisha chama chochote cha siasa hapa nchini kwa sababu nchi yetu ni ya VYAMA VINGI VYA SIASA.

Hofu yangu ni kuwa kumbe vyama vingi hapa nchini havina dira wala uelekeo kwa vile katiba zao ni 'madesa' ya vyama vingine kutoka nje ya nchi kama Bw. TUNGU MPENDAZOE alivyoeleza bila kujikanyaga. Kwa hali hii nchi yetu itaendelea kuwa masikini siku zote! Sasa naanza kukubali kuwa sehemu kubwa ya wanasiasa ni watu waliofeli mitihani yao shuleni na kuamua kuingia kwenye siasa ndio maana hawana mawazo mapya kwa maendeleo ya nchi hii. Mazingira ya ANC ya huko Afrika Kusini ni tofauti mno na mazingira ya nchi yetu. Wazee wa CCJ waliibuka kwa mbwembwe na TUNGU aliwemo (MSc) naye akiinizwa mkenge na aikana NAPE hadi kudesa katiba za watu.

Ee Mwenyezi Mungu Taifa hili limekosea wapi hadi leo tuko hapa? Inua vijana wako wa kike na wa kiume wasaidie nchi hii, amen.

Umeweza kuangalia sheria za nchi yako na kulinganisha na sheria za nchi nyingine? mbona zote madesa au simbi kwa wanaSUA. Angalia sheria ya ushirika ya Kenya na sheri ya Ushirika ya Tanzania..nenda uangalie rasimu ya sheria ya kuanzisha tume ya kukusanya maoni ya kurekebisha katiba kama wao wanavyosema na ile ya Kenya...Nenda uangalia curriculum za vyou vyako vikuu na uangalie na zile za vyou vya Uingereza....

Ukimaliza hapo sasa utakuwa na jibu
 
jamae, nape hayuko peke yake. Mnakumbuka kipindi kile jk anautaka urais? Ccm ilikaribia kuvunjika kwa tetesi kuwa jk angekihama. Hata hivyo si kama namtetea huyu dogo. Nataka kuonyesha unafiki wa siasa. Leo kauli za shitambala mnazisikia? Kauli za tambwe mnazisikia? Kauli za ngawaiya mnazisikia? N.k n.k. Jk alimaliza pale aliposema, akili za kuambiwa... Malizia
 
Back
Top Bottom