The Analyst
JF-Expert Member
- Feb 26, 2011
- 464
- 246
Waheshimiwa wanaJF,
Salaams!
UPDATE:
Katibu Mukama ameamua kuwa wazi. CCM hawana orodha ya mafisadi wala hawajatoa siku 90 kwa mtu. "Kwa ujumla hakuna mwana-CCM msafi kama Mapacha watatu" aaaah!...ha..ha..haaaaah! Guys, I told you CCM ni nyoka kweli. Ndiyo maana hata Mwenyekiti wao hakuwa na mfano wowote mwingine katika kuelezea wanachokusudia kuwaaminisha wadanganyika isipokuwa mageuzi ya mara kwa mara ya nyoka kwa kuvua magamba tena alisahau kusema mwenye sumu kali.
Kama huzijui aina za sumu ya CCM (Nyoka wa magamba) fuatilia kauli za kuwapo udini, ukabila, ukanda nk. hapa nchini wakikusudia kuua nguvu za vyama vya upinzani. Hawa jamaa wakizidiwa wapo tayari hata kuwatumia viongozi wajinga wajinga wa dini ili kuanzisha vurugu ambazo zitasaidia kuwalinda wao na mali zao. Lakini bado naamini tunayo nafasi ya kutetea nchi yetu iliyopoteza mwelekeo. May the Almighty God save us from these people.
Time will tell, and God willing these people will pay for this one day. And they will pay so dearly that no one will ever try to imitate what they have done to our country. (end of update)
Tunaojua tabia ya unafiki wa CCM tuliposikia CCM inatarajia kuondokana na baadhi ya viongozi/wanachama wake wanaotajwa kuhusika na ufisadi mkubwa tulijua maigizo yanaanza hivyo tukakaa tayari. Watu wengi wameshabikia sana habari hiyo lakini wengine tunajua chama hiki kina unafiki mno kiasi kwamba hawa jamaa wasipotaka kuondoka wenyewe basi mambo yatafifia na kupotea.
Kama nakumbuka vizuri kelele zote kuhusu kuwapa watu hao siku 90, kuwaandikia barua nk. zimekuwa zikipigwa na viongozi wao wapya ndani ya Sekretarieti wengine hata bila kuulizwa sasa cha ajabu tayari wameshaanza kupingana wao kwa wao. Wengine wanasema siku 90 na kuwaandikia barua watuhumiwa wa ufisadi hayakuwa maazimio ya vikao vyao n.k n.k n.k
Habari ifuatayo kutoka Gazeti la Nipashe inaonesha hata anayepaswa kuandika hizo barua na lini zitaandikwa haijulikani. Hii inawezekana wapi kama si maigizoni tu? Mkiambiwa CCM wanajaribu kufanya kiini macho katika kushughulikia ufisadi mtasema mnadanganywa?
Barua za mafisadi wa CCM zaumiza Msekwa, Mukama
Na Joseph Mwendapole
23rd April 2011
Kila mmoja akwepa ni lini zitaandikwa
Wengine wawa mbogo, kuulizwa hayo
Wingu la ufisadi bado linazidi kuwaumiza vichwa viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), baada ya vigogo wa ngazi za juu wa chama hicho kuogopa kuweka wazi iwapo watuhumiwa wa ufisadi ndani ya chama hicho wameshakabidhiwa barua za kuwataka wajiondoe wenyewe.
Kila kiongozi aliyetafutwa jana kuzungumza iwapo tayari chama kimewaandikia barua za kuwataka wajiondoe kwenye chama hicho, aling'aka na kuelekeza aulizwe mwenzake.
Wa kwanza alikuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, ambaye alisema suala hilo halishughulikiwi na idara yake hivyo alielekeza aulizwe Katibu Mkuu wa chama hicho, Wilson Mukama.
Alisema kila idara inajukumu lake na kwamba ofisi yake ni ya kuzungumzia masuala ya chama, lakini si mambo yanayohusu masuala ya utendaji.
"Kila idara inawajibu wake, hilo haliko kwenye idara yangu, mimi ni msemaji wa chama nitafuatilia kujua kama zimeshaandikwa na kuwasilishwa kwa wahusika ila anayeweza kulisemea ni Katibu Mkuu," alisema na kuongeza:
"Jumatano watu wote wakiwa ofisini nitakuwa katika nafasi nzuri ya kulizungumzia hilo, nitafuatilia kujua kama zimeshaandikwa na kukabidhiwa kwa wahusika au la, lakini kwa sasa sijui lolote kuhusu hizo barua," alisema Nnauye ambaye kabla ya kushika wadhifa huo alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Masasi.
Alipotafutwa Naibu Katibu Mkuu Bara, John Chiligati, alisema anayeweza kulisema suala hilo ni msemaji wa chama, Nnauye kwa kuwa si kila mtu anaweza kuzungumzia masuala ya chama.
"Chama kinamzungumzaji wake ambaye ni Nape, mtafute Nape maana kila mtu akianza kuzungumza mambo ya chama itakuwa vurugu, ukimpata yeye atakueleza vizuri," alisema.
Alipotafutwa kuzungumzia suala hilo, Katibu Mkuu wa chama hicho, Wilson Mukama, alikuwa mkali na kuelekeza kuwa aneyefaa kuulizwa ni Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Pius Msekwa.
"Hayo unayoniuliza sikuwahi kuagiza yafanyike na wala si wajibu wangu, mtafute Makamu Mwenyekiti ndiye atakueleza, kwanza kwa sasa niko kijijini kwangu kuna mambo mengine nafanya," alisema Mukama na kukata simu.
Alipotafutwa Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Pius Msekwa aligeuka mbogo na kuhoji mwandishi anatafuta habari hizo kwa ajili ya kuzipeleka wapi.
Baada ya kuulizwa iwapo chama hicho kimeshawaandikia barua watuhumiwa wa ufisadi, Msekwa alikuwa mkali na kumweleza mwandishi kuwa masuala hayo ni ya ndani ya chama na hayamhusu.
"Hizi habari unatafuta za nini wakati hazikuhusu, unajua kuna habari za kuandika na zingine si za kuandika, hizi ni za kwetu ndani ya chama na hazikuhusu unataka za nini kwaheri," alisema Msekwa na kukata simu.
Wiki iliyopita, Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ilimuagiza Katibu Mkuu wa chama hicho, Wilson Mukama, kuwaandikia barua viongozi wanaotakiwa kujiuzulu kuwafahamisha kwamba, kama hawatafanya hivyo kikao kijacho cha NEC kitawafuta uongozi.
Watuhumiwa hao wa rushwa na ufisadi wakiwemo wajumbe wa NEC taifa, wamepewa muda wa miezi mitatu sawa na siku 90 wapime uzito wa tuhuma zinazowakabili, wajiuzulu wenyewe.
Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Pius Msekwa, alieleza msimamo huo mjini Dodoma wakati wa mkutano wa kuwatambulisha wajumbe wa sekretarieti mpya akiwemo Katibu Mkuu, Wilson Mukama.
Hatua hii ni mchakato wa CCM kujivua gamba. Tayari wajumbe wa Sekretarieti na Kamati Kuu walikwisha kujiuzulu na kutoa fursa ya kuteuliwa wengine. Maamuzi yaliyofanyika Dodoma wiki mbili zilizopita.
CHANZO: NIPASHE
Salaams!
UPDATE:
Katibu Mukama ameamua kuwa wazi. CCM hawana orodha ya mafisadi wala hawajatoa siku 90 kwa mtu. "Kwa ujumla hakuna mwana-CCM msafi kama Mapacha watatu" aaaah!...ha..ha..haaaaah! Guys, I told you CCM ni nyoka kweli. Ndiyo maana hata Mwenyekiti wao hakuwa na mfano wowote mwingine katika kuelezea wanachokusudia kuwaaminisha wadanganyika isipokuwa mageuzi ya mara kwa mara ya nyoka kwa kuvua magamba tena alisahau kusema mwenye sumu kali.
Kama huzijui aina za sumu ya CCM (Nyoka wa magamba) fuatilia kauli za kuwapo udini, ukabila, ukanda nk. hapa nchini wakikusudia kuua nguvu za vyama vya upinzani. Hawa jamaa wakizidiwa wapo tayari hata kuwatumia viongozi wajinga wajinga wa dini ili kuanzisha vurugu ambazo zitasaidia kuwalinda wao na mali zao. Lakini bado naamini tunayo nafasi ya kutetea nchi yetu iliyopoteza mwelekeo. May the Almighty God save us from these people.
Time will tell, and God willing these people will pay for this one day. And they will pay so dearly that no one will ever try to imitate what they have done to our country. (end of update)
Tunaojua tabia ya unafiki wa CCM tuliposikia CCM inatarajia kuondokana na baadhi ya viongozi/wanachama wake wanaotajwa kuhusika na ufisadi mkubwa tulijua maigizo yanaanza hivyo tukakaa tayari. Watu wengi wameshabikia sana habari hiyo lakini wengine tunajua chama hiki kina unafiki mno kiasi kwamba hawa jamaa wasipotaka kuondoka wenyewe basi mambo yatafifia na kupotea.
Kama nakumbuka vizuri kelele zote kuhusu kuwapa watu hao siku 90, kuwaandikia barua nk. zimekuwa zikipigwa na viongozi wao wapya ndani ya Sekretarieti wengine hata bila kuulizwa sasa cha ajabu tayari wameshaanza kupingana wao kwa wao. Wengine wanasema siku 90 na kuwaandikia barua watuhumiwa wa ufisadi hayakuwa maazimio ya vikao vyao n.k n.k n.k
Habari ifuatayo kutoka Gazeti la Nipashe inaonesha hata anayepaswa kuandika hizo barua na lini zitaandikwa haijulikani. Hii inawezekana wapi kama si maigizoni tu? Mkiambiwa CCM wanajaribu kufanya kiini macho katika kushughulikia ufisadi mtasema mnadanganywa?
Barua za mafisadi wa CCM zaumiza Msekwa, Mukama
Na Joseph Mwendapole
23rd April 2011
Wingu la ufisadi bado linazidi kuwaumiza vichwa viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), baada ya vigogo wa ngazi za juu wa chama hicho kuogopa kuweka wazi iwapo watuhumiwa wa ufisadi ndani ya chama hicho wameshakabidhiwa barua za kuwataka wajiondoe wenyewe.
Kila kiongozi aliyetafutwa jana kuzungumza iwapo tayari chama kimewaandikia barua za kuwataka wajiondoe kwenye chama hicho, aling'aka na kuelekeza aulizwe mwenzake.
Wa kwanza alikuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, ambaye alisema suala hilo halishughulikiwi na idara yake hivyo alielekeza aulizwe Katibu Mkuu wa chama hicho, Wilson Mukama.
Alisema kila idara inajukumu lake na kwamba ofisi yake ni ya kuzungumzia masuala ya chama, lakini si mambo yanayohusu masuala ya utendaji.
"Kila idara inawajibu wake, hilo haliko kwenye idara yangu, mimi ni msemaji wa chama nitafuatilia kujua kama zimeshaandikwa na kuwasilishwa kwa wahusika ila anayeweza kulisemea ni Katibu Mkuu," alisema na kuongeza:
"Jumatano watu wote wakiwa ofisini nitakuwa katika nafasi nzuri ya kulizungumzia hilo, nitafuatilia kujua kama zimeshaandikwa na kukabidhiwa kwa wahusika au la, lakini kwa sasa sijui lolote kuhusu hizo barua," alisema Nnauye ambaye kabla ya kushika wadhifa huo alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Masasi.
Alipotafutwa Naibu Katibu Mkuu Bara, John Chiligati, alisema anayeweza kulisema suala hilo ni msemaji wa chama, Nnauye kwa kuwa si kila mtu anaweza kuzungumzia masuala ya chama.
"Chama kinamzungumzaji wake ambaye ni Nape, mtafute Nape maana kila mtu akianza kuzungumza mambo ya chama itakuwa vurugu, ukimpata yeye atakueleza vizuri," alisema.
Alipotafutwa kuzungumzia suala hilo, Katibu Mkuu wa chama hicho, Wilson Mukama, alikuwa mkali na kuelekeza kuwa aneyefaa kuulizwa ni Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Pius Msekwa.
"Hayo unayoniuliza sikuwahi kuagiza yafanyike na wala si wajibu wangu, mtafute Makamu Mwenyekiti ndiye atakueleza, kwanza kwa sasa niko kijijini kwangu kuna mambo mengine nafanya," alisema Mukama na kukata simu.
Alipotafutwa Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Pius Msekwa aligeuka mbogo na kuhoji mwandishi anatafuta habari hizo kwa ajili ya kuzipeleka wapi.
Baada ya kuulizwa iwapo chama hicho kimeshawaandikia barua watuhumiwa wa ufisadi, Msekwa alikuwa mkali na kumweleza mwandishi kuwa masuala hayo ni ya ndani ya chama na hayamhusu.
"Hizi habari unatafuta za nini wakati hazikuhusu, unajua kuna habari za kuandika na zingine si za kuandika, hizi ni za kwetu ndani ya chama na hazikuhusu unataka za nini kwaheri," alisema Msekwa na kukata simu.
Wiki iliyopita, Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ilimuagiza Katibu Mkuu wa chama hicho, Wilson Mukama, kuwaandikia barua viongozi wanaotakiwa kujiuzulu kuwafahamisha kwamba, kama hawatafanya hivyo kikao kijacho cha NEC kitawafuta uongozi.
Watuhumiwa hao wa rushwa na ufisadi wakiwemo wajumbe wa NEC taifa, wamepewa muda wa miezi mitatu sawa na siku 90 wapime uzito wa tuhuma zinazowakabili, wajiuzulu wenyewe.
Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Pius Msekwa, alieleza msimamo huo mjini Dodoma wakati wa mkutano wa kuwatambulisha wajumbe wa sekretarieti mpya akiwemo Katibu Mkuu, Wilson Mukama.
Hatua hii ni mchakato wa CCM kujivua gamba. Tayari wajumbe wa Sekretarieti na Kamati Kuu walikwisha kujiuzulu na kutoa fursa ya kuteuliwa wengine. Maamuzi yaliyofanyika Dodoma wiki mbili zilizopita.
CHANZO: NIPASHE