- Thread starter
- #21
Nakuuliza wewe chuki binafsi!
Kwamba !
Kinana (mzee wa kusafirisha ndovu)
Na
Nape
(Mzee wa goli la mkono).
Walikuwa wanafufua chama kilichouwawa na nani?
Wauwe wao halafu wafufuwe wao?
Muwe mnatunza kumbukumbu vizuri.
Bashiru aliongoza tume iliyoundwa kukusanya na kuorodhesha mali zote za CCM.
Mmojawapo wa watuhumiwa waliokutwa na ubadhirifu mkubwa ni huyo Nape Nauye ambaye alikuwa ameficha mpaka V8 mpya za chama nyumbani kwake.
Achilia mbali uuzwaji wa kifisadi mitambo ya Tanzania printpark na Chanel Ten TV.
Yoote hayo JPM alisamehe.
Huyu Kinana yeye alifikia mahali mpaka akasajili meli na kuitumia kusafirisha meno ya tembo toka nchini kwenda ughaibuni.
Mpaka pale ilipokamatwa na Interpol .
Sauti za yeye kumkashifu marehemu JPM zilivuja mitandaoni,lakini JPM alisamehe.ingekuwa ni huyu mama sijui ingekuwaje?
Yule Bulembo yeye shule za iliyokuwa TAPA, jumuia ya wazazi aliziuza kama mali yake.
Mfano hai kule Musoma kuna kesi iko mahakamani hivi tunavyoongea. Ni sekondari ya Isango.
Sasa hawa leo ndio watetezi wa Mh Samia?
Ushindi mkubwa wa kihistoria kwa CCM ulitokea chini ya uongozi wa hao unaowaita Mapimbi.haijawahi kutokea.
Watanzania tuna laana ya wizi unafiki, na uvivu na hatupendi ukweli na wakweli wake.
Huo ndio uhalisia
....acheni kuishi kwa visasi
2025 sio mbali na hakika CCM na mama yao huyu watawajua Watanzania wa leo.
MUNGU IBARIKI AFRIKA NA UWABANIKE WANAFIKI WA AFRIKA.
TANZANIA IWE NA AMANI mengine yatajinyoosha yenyewe kama ambavyo katiba mpya inaelekea kujileta yenyewe.
Pole sana nadhan ni wakat uanze kuamin mwemdazake kafa maana naona bado huamin ndo team yenu inapewa bye bye hamien upinzani