Ileje
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,796
- 12,239
Itakumbukwa mwaka 2019 aliyekuwa Katibu mkuu wa CCM Bw. Bashiru aliwapuuza na kuwafananisha na mpira wa chandimu makatibu wakuu waliomtangulia Makamba na Kinana. Aidha aliwaambia wahamie upinzani kama hawawezi kwenda na kasi ya CCM mpya.
Haya yalitokea baada ya Wazee hawa kulalamika kuwa simu zao zimedukuliwa na wafuasi wa Magufuli aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM. Wengine ambao Bashiru aliwashughulikia ni January Makamba na Nape Nauye ambao wote hivi sasa ni mawaziri katika serikali ya Samia.
Mwingine aliyenyolewa bila maji na wembe wa Bashiru ni Benard Membe hadi akahamia ACT Wazalendo.
Haya yalitokea baada ya Wazee hawa kulalamika kuwa simu zao zimedukuliwa na wafuasi wa Magufuli aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM. Wengine ambao Bashiru aliwashughulikia ni January Makamba na Nape Nauye ambao wote hivi sasa ni mawaziri katika serikali ya Samia.
Mwingine aliyenyolewa bila maji na wembe wa Bashiru ni Benard Membe hadi akahamia ACT Wazalendo.