NAPE naamini kabisa ya kuwa wewe ni kijana wa chama tawala unaekubalika kwa watanzania kwa kiasi kikubwa hilo halina ubishi. NINGEFURAHI SANA kama ungetoa ufafanuzi kwa kile kinachoaminika ya kwamba umenyanyapaa kabila fulani mbele ya waandishi wa habari. SIO SIRI hizi taarifa za kunyanyapa kabila fulani zimetushtusha hata sisi ambao tumekuwa tukikuamini ya kuwa wewe ndio kijana pekee ndani ya CCM mwenye kuweza kuvuta kadamanasi (ORATOR)
Nimeamua kuja mwenyewe. Nashangaa wakati mwingine maana ni hapa ndo watu walisema Nape kashazibwa mdomo kama vile yale ni maamuzi ya Nape binafsi.
Jana nimewakumbusha tu watuhumiwa na wapambe wao si busara kujifariji kuwa maamuzi yatabadilishwa nje ya vikao, na vikao vyenyewe ni lazima iwe ama NEC au Mkutano Mkuu(Congres) na si vinginevyo.
Kuna hoja hapa eti kwamba Nape anabwabwaja tu, hakuna vitendo, let's be objective,hivyo vitendo ni vipi? Taarifa ya utekelezaji wa maamuzi haya itatolewa kwenye kikao kijacho cha NEC na si siku 90 kama wanavyojaribu kueleza hapa. Tumelieleza sana hili la siku,WAANDISHI TENA BAADHI ndo walitafsiri siku tisini kutoka kwenye ratiba ya vikao vya NEC ambavyo Dodoma tulikubaliana tentively tunaweza kukutana July ndo wakahesabu na kusema siku tisini. Lakini hakuna kikao kinakutana exactly kwa muda ulopangwa,kuna flexibility.
Ushauri subirini NEC ikutane mtuseme tukishindwa kufukuza.