Nape: Mkapa aliniambia nisithubutu kutoka CCM pamoja na kukata tamaa

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,445
7,813
Nape Nnauye yuko msibani na anaongelea uhusiano wake na Mkapa, amesema alianzia U-DC wilaya ya Masasi, nyumbani kwa Mkapa na alimpika vizuri sana kisiasa na utendaji.

Aliingia kamati kuu 2002 Mkapa akiwa mwenyekiti na kusema alikuwa na misimamo katika kuongoza vikao vya chama.

Mwisho anasema kuna kipindi makombora yalikuwa mengi sana na alikata tamaa. Mkapa akamuita Mvomero, alikuwa na mashamba yake huko na kumwambia asithubutu kutoka CCM, makombora yatapita.
 
nyumbani kwa Mkapa na alimpika vizuri sana kisiasa na utendaji.
Alimpika atumie goli la mkono? Alimpika kujivunia madaraka? rubbish! Asitoke CCM kwani itadumu madarakani milele? Anajua kesho ikoje? Huo ni uongo na kama kweli alimwambia hivyo, naye ana mapungufu makubwa!
 
Back
Top Bottom