Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,899
Nape Mnauye wakati akiongea na vyombo vya habari mjini Dodoma leo ambako vikao vya Chama cha CCM vikiendelea amebadilisha kuali mbiu ya awali aliyokuwa akizunguka nchi nzima kutangaza majina ya wanaotakiwa kuachia ngazi . Leo kaja na mpya kwamba vyombo vya habari vilipotosha ukweli wa maana ya kuvua magamba kwa maana ya kubadilika na wala si kuwafukuza watu. Hii imekaaje?
Waliopinga kwamba Nape hakuongea hayo, hapa ni ushahidi zaidi kutoka gazeti la Habari leo, pamoja na kuchakachua habari lakini ukweli umebaki kama mada hii ilivyo
GAZETI LA HABARI LEO LIMEANDIKA HABARI HII KAMA IFUATAVYO
Kichwa cha habari: Kujivua gamba si Lowassa, Chenge, Rostam pekee
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimewataka wanachama wake na wananchi kuondoa wasiwasi kuhusu vikao vyake vya juu vinavyofanyika Dodoma.
Chama hicho kimesisitiza kuwa, dhana ya ‘kujivua gamba' ambayo inaendelea, haihusu watu watatu tu, ni pana, iliyosheheni mageuzi kuanzia chini hadi juu.
Chama hicho mbali na kukiri kuwa vikao hivyo vilivyoanza Jumamosi na kutarajiwa kumalizika Alhamisi vimesababisha hisia kali kwa wanachama, kimeonya kuwa hakitavumilia upotoshwaji wa habari kuwa ‘kujivua gamba' kunahusu watu watatu, wakati kuna mengi zaidi ya hilo.
Akizungumza jana na waandishi wa habari katika ofisi za makao makuu ya CCM mjini hapa, Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM, Nape Nnauye,alisema habari zinazotolewa zimekuwa zikipotosha kuwa vikao hivyo vinashughulikia watu watatu kwa maslahi aliyosema hajui ni ya nani.
Mpaka sasa watu wanaolengwa na habari hizo kuwa 'watavuliwa gamba' alizosema zinapotoshwa, ni Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge na aliyekuwa Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz.