Nape JF sio sawa na Facebook

Nape JF sio sawa na Facebook

Saint Ivuga

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2008
Posts
55,028
Reaction score
59,657
Nape tunashukuru sana kwa kuja hapa JF, tunajua una kazi nyingi ila mtindo wako wa kuweka bandiko hapa na kukimbia sio fresh, hapa JF ukiweka bandiko lazima ulitetee, sio lazima ujibizane au ujibu watu /post zenye jazba au matusi.
Kuna post nyingi tu zenye hoja.
Hapa sio sawa na facebook, kule wamejaa watoto wa wakubwa na rafiki zako ambao siku zote watakusifia ila humu ndani hatusifii kila kitu , ukipiga kazi lazima tukusifie ila ukiharibu hatukuachi, kwa hiyo ukianzisha mada au thread usiikimbie hapa.
Amani iwe nawe:
Saint Ivuga @Mbagala kipati
 
Salam mheshimiwa!

Mimi Radio Producer napenda kukuandikia barua hii kwa hisia zangu ili kutoa mchango wangu kwako katika siasa ya sasa ambayo hata watoto wameielewa! Kwanza mimi sijui kabisaaa mambo ya undani kuhusu siasa ila napenda nikuelezea mtizamo wangu kwenye technologia ya mawasiliano!

1. Mkuu Nape mi nadhani umepewa heshima ya Ukatibu Enezi katika chama chako ili ufanye mambo mazuri ambayo yatakiletea sifa na uhai chama chako. Kwa mtu makini hiyo siyo nafasi ya kuonyesha ubabe au uwezo wa kuponda na kuharibu nguvu ya wapinzani, bila kutathimini athari zake kwa jamii. Ukweli kama alivyosema Mzee Mwanakijiji kwamba kazi ya chama pinzani ni kukisoa chama tawala na kumulika madhaifu yake ili kukidhoofisha na hatimaye kupewa dhaman ya kutawala na wanachi! Hata kwa chama tawala nadhani ni the same! Kwa kiasi umejitahidi kulifanyia kazi hilo make nimekuona kila ukisismama ukipata fursa ya kuponda upinzani unafanya hivyo. Lakini.......

2. Ijue vizuri teknolojia ya mawasiliano ya mtandao. Mtandao unaweza kukuharibia sifa zako sana! au kukuongezea sifa zako sana! Wataalamu wanasema kwamba moja ya negative effect za social network zinakuonyesha kwa jamii kiasi gani ulivyomweupe kichwani au ulivyo na nguvu kichwani! Nape nimesoma sana post zako nyingi hapa JF na hata kule Facebook hoja zako au topic zako unazotoa hata kwa mtu mwenye ufahamu wa kawaida anakuona wewe ni mtu wa kawaida sana! Wewe ni kiongozi mkubwa katika chama chako na hata nchi hii huwezi kuwa na post za ajabu ajabu kiasi hicho! Angalia wall zote za marais, hata watu wenye heshima uone kama utakuta post nyepesi kama zako. Moja ya post ulizopost ni hizi:-

Nape Nnauye
CHUO KIKUU CHA. DODOMA2 hours ago via BlackBerry · Like · kwenye facebook.
Majibu uliyoyapata unajua wewe!


post zingine:-
Nape Nnauye
Nimeona kikatuni mahali mtu mmoja kavaa kombati akiwaammbia wafiwa subirini msizike msubiri maandamano yetu hapa.......hii ni dhihaka au kweli?

Nape Nnauye
BINADAMU HAENDELEZWI ILA HUTENGENEZEWA MAZINGIRA MAZURI YA KUJIENDELEZA MWENYEWE"JK NYERERE

Nape Nnauye
TUSIKILIZE RADIO UHURU.....RADIO YA CHAMA CHETU

Hizi ni moja tu ya post zinazonifanya nikuone mtu wa kawaida sana! Angalia wall ya Obama, hata maraisi wengine kama inapost za kitoto kiasi hicho! Nape unajivunjia heshima! Halafu huoni hizo wall wanazokupostia watu zikiwa na matusi makubwa kiasi hicho?? Huoni kuwa jamiii iko kinyume nawewe zaidi? Je unatumia hoja gani sasa kujiweka vizuri katika jamii? Mafanikio huanzia katika jamii kama watu wengi wanakuponda jiulize cha kufanya ili hali hiyo iishe! WEWE BINAFSI UNAWEZA UKAWA MTU MZURI SANA LAKINI CHAMA KIKAHARIBU KABISA SIFA YAKO! Fikiria zaidi kaka yangu, sijaona hoja zako za kiuongozi!

3. Post ya katuni ya kombati. Kwa mimi hata kama ningekuwa balozi wa kitongoji nisingeweza kupost hoja ya hivyo wakati taifa lina msiba! Vifo vilivyotokea Mara ndugu yangu vinaumiza mno hasa kwa walengwa! Jiulize hata kama ungekuwa wewe ukatokwa na mtoto wako kwa hali hiyo ungepost post ya hivyo kweli? huu ni wakati wa kufikiria mara 3 zaidi kabla ya kusema chochote! Ni wakati ambao wafiwa wanahitaji maelezo ya kuridhisha na ya msingi! Unatakiwa kuwa na Empathies na Sympathies! Uchukulie kama msiba wako! Toa maneno yasiyo ya kisiasa wakati huo linda nafsi yako! Kadri unavyotoa maneno makali na ya kuumiza ndivyo unavyopata laana za wanachi na kudharauliwa! Kaka yangu Nape kaa chini basi kaka ufikirie vizuri uanze moja, ulivyoanza watu wengi wamekuwa kinyume hautafanikisha kile chama kimedhamiria!

4. Mtandao, Kaka yangu sijui elimu yako kuhusu mtandao iko level gani, lakini nakuomba kaa na watalaamu wa mitandao badili matumizi ya mtandao haraka iwezekanavyo. Hata facebook ingebidi ujitoe ni sawa tu au utengeneze page siyo kutumia kama hivyo unavyotumia! Mtu yeyeote anakupostia matusi tu kwenye wall yako anakudhalilisha mno kaka! Weka privacy yako kwenye Fb iwe kubwa! social network ziko hivi:- Walio kwenye mtandao wanaweza kuwa watatu hao wakitoka wanamarafiki zao wataenda kuwaambia yaliyotokea na hao watatu watafanya hivyo hivyo! Unachoandikiwa ama kuandika kinasomwa na wengi mno kaka yangu! Hata hapa JF, wewe kila hoja ukitoa watu wanakuponda tu ulishawafanyia nini? Hao wanaokupinga hapa wanafuatwa na jamii nyuma usitarajie jamii nayo itakukubali hamna! Kuna picha uliweka kwenye mtandao umebeba kanga za CCM wanaume wanakugombea wanataka wapate hata moja, NI AIBU KUBWA KWA TAIFA NAYAWEZA KUWA LAANA KWAKO! Wewe uliona fahari sana kuwa unafanya kazi, hebu fikiria angekuwa mzazi wako anajitoma kiasi hicho kugombania kamga ungefurahi? Wanachi wanahitaji kupewa haki yao sasa hivi sioyo vitenge wala kanga! Watanzania ni matajiri kwa vitu vya asili walivyopewa na Mungu, lakini leo wewe ndo unaneemeka na wao unawapelekea kanga???? ni tusi kubwa hilo kaka yangu! Kaka badili msimamo wako! jisikie Utanzania wa Watanzania maskini ili uwasaidie!

Namalizia kwa kusema Nape mtandao unakuharibia sifa zako, waachie wanaojua kuutumia vinginevyo wewe binafsi utapoteza heshima yako maisha yako yote!

Sina nia mbaya mwana wa mtu kama nimekukera leave me Alone.
Radio Producer.
 
You are hopeless, ccm wamejitia kuvamia hizi social networks waache yawakute unamtahdharisha wa nini? Acha ayakoge matusi hadi avuliwe nguo za ndani
 
Kwanza mimi naona nape ni mwepesi mno kwa nafasi aliyopewa, Alitakiwa kwanza kuelewa itikadi ya CCM kabla ya kuanza kuzungumza sana. Sasa amesoma nini kwa Azam. Anasema nini kuhusu azimio la Arusha, ana mtazamo gani kuhusu siasa ya ujamaa. Hii ni kabla ya kurudi kwanye neno Gamba. Huyu kijana ajifunze kujipanga kama akina mnyika na Zito. Amekuwa ni kijana wa kukurupuka, na nina wasiwasi ataachwa katikati kwenye mataa. Mukama ndo hivyo keshamtema, kwamba hakuna aliyepewa siku tisini, sasa amehamia vyama vya upinzani. Vipost vyake kwenye JF ndio kabisaaa, vinamuonyesha alivyo na mapungufu katika falsafa. Ushauri huu ni mzuri, kwa maana anakwenda shimoni.:A S 103:
 
Kwanza mimi naona nape ni mwepesi mno kwa nafasi aliyopewa, Alitakiwa kwanza kuelewa itikadi ya CCM kabla ya kuanza kuzungumza sana. Sasa amesoma nini kwa Azam. Anasema nini kuhusu azimio la Arusha, ana mtazamo gani kuhusu siasa ya ujamaa. Hii ni kabla ya kurudi kwanye neno Gamba. Huyu kijana ajifunze kujipanga kama akina mnyika na Zito. Amekuwa ni kijana wa kukurupuka, na nina wasiwasi ataachwa katikati kwenye mataa. Mukama ndo hivyo keshamtema, kwamba hakuna aliyepewa siku tisini, sasa amehamia vyama vya upinzani. Vipost vyake kwenye JF ndio kabisaaa, vinamuonyesha alivyo na mapungufu katika falsafa. Ushauri huu ni mzuri, kwa maana anakwenda shimoni.:A S 103:

Yaani jaman muonaoweza fungueni facebook ya Nape muangalia hizo post anazopata toka kwa watu! Namhurumia kwa sababu hakuna anachojenga! mtazamo wake binafsi ndio shida hapo baadae! Make ameshajivunjia heshima sasa atapataje kibali kenye jamii tena?? Aangalie kukubalika katika jamii na si kwa CCM. maana kuna siku CCM watatoka madarakani je atafanya nini kwenye chama kitakachokuwa madarakani? Pole Nape tizama mbali zaidi!
 
Muache aendelee kuumpa matumaini Kama mhonjwa wa ukimwi huku akijua aliyoyafanya nyuma.Ktk page zake facebook nimekuwa nikipita huko mara kwa mara hakuna cha maana anachoandika nyingi zimezidiwa na mipasho Kama ya kwenye taarabu.Pili dharau anayoionyesha waziwazi mbele ya jamii kupitia post zake ktk mitandao juu ya viongozi wa upinzani ndio anajimaliza kabisa.Unaleta dharau kwenye vifo vya Wstanzania?nani ataluvumilia na kukupenda?labda punguani.Go to hell ccm go tunaitaka Tanzania yetu
 
Muache aendelee kuumpa matumaini Kama mhonjwa wa ukimwi huku akijua aliyoyafanya nyuma.Ktk page zake facebook nimekuwa nikipita huko mara kwa mara hakuna cha maana anachoandika nyingi zimezidiwa na mipasho Kama ya kwenye taarabu.Pili dharau anayoionyesha waziwazi mbele ya jamii kupitia post zake ktk mitandao juu ya viongozi wa upinzani ndio anajimaliza kabisa.Unaleta dharau kwenye vifo vya Wstanzania?nani ataluvumilia na kukupenda?labda punguani.Go to hell ccm go tunaitaka Tanzania yetu
Nape si unaona watu wanavyokupa feedback, kama unajua kutumia maoni ya watu chukua haya hapa kajifunze kuadapt
 
Nape si unaona watu wanavyokupa feedback, kama unajua kutumia maoni ya watu chukua haya hapa kajifunze kuadapt

Acha kupigia maiti gitaa, hawezi kujiadapt coz anatafuta platform mpya baada ya kunyang'anywa ile aliyoingia nayo katika wadhifa mpya ya kuwapa RACHEL siku 90 kujiondoa katika CCM. Alipaswa kujiuzulu baada ya Katibu Mkuu wa CCm kukanusha kuwa hakuna majina yaliyotajwa katika vikao vya CC na NEC ya CCM ilihali Mukama hakuhudhuria vikao hivyo. Badala yake Nape aliishia kulalamika mbele ya wahariri kuwa majina yalitajwa na kuibuka na staili mpya ya kuiponda CHADEMA hakujua kuwa nondo zake za CCJ zilikuwa jikoni. Sasa anatakiwa kujivua Gamba yeye na akina RACHEL kwa kuisaliti CCM.
 
You are hopeless, ccm wamejitia kuvamia hizi social networks waache yawakute unamtahdharisha wa nini? Acha ayakoge matusi hadi avuliwe nguo za ndani

hajui falsafa ya kujivua gamba itafuatiwa na ya kujivua nguo.
 
Acha kupigia maiti gitaa, hawezi kujiadapt coz anatafuta platform mpya baada ya kunyang'anywa ile aliyoingia nayo katika wadhifa mpya ya kuwapa RACHEL siku 90 kujiondoa katika CCM. Alipaswa kujiuzulu baada ya Katibu Mkuu wa CCm kukanusha kuwa hakuna majina yaliyotajwa katika vikao vya CC na NEC ya CCM ilihali Mukama hakuhudhuria vikao hivyo. Badala yake Nape aliishia kulalamika mbele ya wahariri kuwa majina yalitajwa na kuibuka na staili mpya ya kuiponda CHADEMA hakujua kuwa nondo zake za CCJ zilikuwa jikoni. Sasa anatakiwa kujivua Gamba yeye na akina RACHEL kwa kuisaliti CCM.


Akimaliza mkutano UDOM atakuja asome
 
Producer mbuzi, ushauri kaa nao mwenyewe, we sema upewa ulfu ngapi na rostam uje ulete upuuzi wako hapa
 
Producer mbuzi, ushauri kaa nao mwenyewe, we sema upewa ulfu ngapi na rostam uje ulete upuuzi wako hapa

Kama wewe ndio Nape pole sana maana huwezi kuadvance hata siku moja! Nimeuweka hapa ushauri wako ili hata watu wengine wachangie hoja zikujenge ujirekebishe! Kama unang'ang'ania na hali uliyonayo na huoni kuwa ni ugonjwa na hutaki kupokea feedback ni bora urudi darasani kwanza ukasome Advance Communication.
 
Nape si unaona watu wanavyokupa feedback, kama unajua kutumia maoni ya watu chukua haya hapa kajifunze kuadapt
Mkuu sijakubaliana na wewe kuhusu kuacha kutumia Mitandao ila namshauri nape atumie kama katibu mwenezi wa ccm, asifanye ujinga kabla hata hajapost anaweza kushauliana na wenzake kwanza! but kwa sasa naona kama yupo chini sana huwezi ukaenda kupata mawazo ya kujenga kwa Nape, anaweza kuangalia post za Zitto Kabwe, Dr Slaa, Mnyika, Malecela jr, n.k halafu awe anapost kama wao na asikimbie kwenye mijadala hiyo, kama afanyavyo sasa. JF SI YA KITOTO KAMA FACEBOOK WALIOPO HUMU NIWATU WANAOJUA MAMBO NA KUYATAFAKALI! sasa inakuwa afadhali ya M.S tena wakati yeye ni Kiongozi, na nibora asingeandika jina lake tujue ni jinga flani hv!
 
Kama wewe ndio Nape pole sana maana huwezi kuadvance hata siku moja! Nimeuweka hapa ushauri wako ili hata watu wengine wachangie hoja zikujenge ujirekebishe! Kama unang'ang'ania na hali uliyonayo na huoni kuwa ni ugonjwa na hutaki kupokea feedback ni bora urudi darasani kwanza ukasome Advance Communication.
wabongo njaa zitawaua, we sema umepewa ngapi uje hapa ulete ukatuni wako.
 
Mkuu sijakubaliana na wewe kuhusu kuacha kutumia Mitandao ila namshauri nape atumie kama katibu mwenezi wa ccm, asifanye ujinga kabla hata hajapost anaweza kushauliana na wenzake kwanza! but kwa sasa naona kama yupo chini sana huwezi ukaenda kupata mawazo ya kujenga kwa Nape, anaweza kuangalia post za Zitto Kabwe, Dr Slaa, Mnyika, Malecela jr, n.k halafu awe anapost kama wao na asikimbie kwenye mijadala hiyo, kama afanyavyo sasa. JF SI YA KITOTO KAMA FACEBOOK WALIOPO HUMU NIWATU WANAOJUA MAMBO NA KUYATAFAKALI! sasa inakuwa afadhali ya M.S tena wakati yeye ni Kiongozi, na nibora asingeandika jina lake tujue ni jinga flani hv!
Umenena kweli kabisa kiongozi!
 
Producer mbuzi, ushauri kaa nao mwenyewe, we sema upewa ulfu ngapi na rostam uje ulete upuuzi wako hapa


huyu ni moja wa vijana wake aliowaajiri kwa ajili ya jf.......
 
RACHEL, hawa wamekisaliti vipi CCM? Mimi nadhani hatuwezi kuwaweka hawa sehemu moja na SIMWANA. Nadhani mkubwa wao aliogopeshwa na mlisho nyuma kuwa CHEL walikuwa na muswada kuwa sio lazima Rais akalie kiti cha chama. Hivyo akaanza kutafuta njia ya kuwatoa kabisa lakini kumbe aliyepewa usukani wa kuendesha hilo jahazi hajakomaa vizuri. Na hili litarudi tu kung'ata mkiani!
Tunatumia muda mwingi kwa kuwajadili akina RACHEL badala ya kuangalia matatizo ya wananchi na jinsi serikali inavyoyatatua au inavyoshindwa kuyatatua ili tutoe hukumu ya kweli 2015 badala ya kuwajadili watu wachache ambao kwa mawazo yangu mmoja wao akipewa nchi hii ataipeleka mbali kwa maendeleo kwani ni mtu ambayo anafuatilia mambo na hapendi porojo. Hao wanaoitwa wasafi ni akina nani ndani ya CCM? Hakuna hata mmoja, shida tu ni kwamba ndani mwao wamezidiana uwezo wa kuongoza na kuwa na mali.
 
Back
Top Bottom